Mazao jamii ya maharage ni fursa nzuri ya biashara

Mazao jamii ya maharage ni fursa nzuri ya biashara

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Mazao jamii ya maharage ni maharage, kunde, choroko, mbaazi, njugumawe nk. Kutokana na idadi ya wasio kula nyama duniani kuongezeka soko la mazao haya limeongezeka sana. Mazao haya hutumiwa na watu wa dini na race zote.

Licha ya mabara mengi kuwa watumiaji wazuri wa mazao haya, Afrika ya Magharibi na Kaskazini ambako kuna idadi kubwa ya Waisalmu, mwezi wa Ramadhani mazao haya ni keki ya moto.

Changamoto kubwa ni kuyaanda mazao haya katika ubora. Yasiwe na vumbi, mawe na yawe katika vifungashio bora, imara na vya kuvutia.

Kabla ya covid pandemic nilibahatika kufika Morocco, nilishangaa kuona kunde kutoka China ziko dukani. Nilikumbuka kuwa sehemu kubwa ya Morocco ni jangwa lakini pia niliwaza yaani Mchina amepata hili soko na sisi Waafrika hatulioni.

Kunde za Wachina zilifungwa katika ujazo wa nusu kilo na kilo moja. Zilikua safi na zinavutia kwakweli katika macho ya mnunuaji.

20210419_090552.jpg

 
Njoo kwetu Kigoma uone maharage wanavyo yauza, bakuli kubwa la kilo moja na nusu wanauza kwa sh,2800/=, Niambie kama kwenu huko Dar soko lipo niwaleteeni
Kitu cha msingi ni wafanyabiashara kupanga mikakati ya kusafirisha mazao haya kwa treni. Shughuli kama hizi huzalisha ajira. Mkiwa na godown Dar litatoa ajira kwa vibarua kadhaa.
 
Ili uweze lazima pia uyaandae katika mazingira ambayo sumu za kuua wadudu isiwe katika kiwango cha juu.

Vinginevyo sahau. Watakula wabongo tu.
 
Ili uweze lazima pia uyaandae katika mazingira ambayo sumu za kuua wadudu isiwe katika kiwango cha juu.

Vinginevyo sahau. Watakula wabongo tu.
Kufanya organic farming, unatumia majivu kuua wadudu.
 
Dah kwa hiyo ukipiga majivu kumbe unaua wadudu nilikuwa sijui
Bibi yangu hakwenda shule alitumia njia hii kutunza mimea yake. Akiona mashina mawili yameshambuliwa anabeba majivu. Alifanya hivi kwa magonjwa yote.

Nilitaka kuwauliza wataalamu wa kilimo uhusiano uliopo kati ya majivu na wadudu wanaoshambulia mazao.

Njia nyingine aliyotumia ni kung’oa mimea iliyoshambuliwa na kuichoma Moto. Hakutumia kemikali kabisa.
 
Haitakulipa
Hapa 1kg ni 2400
Kwa kusafirisha nje ya nchi unapata mashine za kuchambulia na kufungia. Kama mtaji wa kununua mashine huna unatangaza vibarua, anaekuja unampa debe na ungo, anahahihisha ametoa mabovu na mawe yote na kupepeta.
 
Kwa kusafirisha nje ya nchi unapata mashine za kuchambulia na kufungia. Kama mtaji wa kununua mashine huna unatangaza vibarua, anaekuja unampa debe na ungo, anahahihisha ametoa mabovu na mawe yote na kupepeta.

Kwa nje inaweza ikamlipa
Nadhani kuna fursa nyingi masoko ya kimataifa

Changamoto ni uthubutu
Taarifa sahihi
Na bidhaa sahihi
 
Kwa nje inaweza ikamlipa
Nadhani kuna fursa nyingi masoko ya kimataifa

Changamoto ni uthubutu
Taarifa sahihi
Na bidhaa sahihi
Ni kweli kabisa kwasababu hii 2,400 kwa kilo haifiki hata 1$ . Tatizo letu lingine ni kuandaa bidhaa katika ubora. Korosho ziko wahi kurudi kwakua zilikua a na kokoto
 
Tatizo la bongo Sky Eclat Ni uwekezaji. Kuna uwekezaji mdogo kuanzia kwenye uzalishaji mpaka processing. Naweza kusema 60% ya wakulima wanalima chini ya vieka 5. wengi Sana eka 1-2 baaasi. Hapa Ni Lazima aforce kuweka high profit margin ili apate kitu. Ndio maana unakuta Kama huyo mchangiaji hapo juu alivyosema kuwa Kigoma wanauza 1.5 kg kwa 2500 sawa na 1,000/kg wakati DSM (ambapo Ni jiji la larger consumers wa mazao) Ni 2,000/kg.

Kwa sababu ya mtu mmoja mmoja kuzalisha kidogo kidogo gharama za kusafirisha kuunganisha mzigo zinakuwa juu sana. Ukumbuke pia wakulima hawasafishi vizuri Wala kuweka katika grades. Ukianza pia na kugrade ndipo usishangae kukuta grade 1 Ni 20% ya mzigo mzima, 60% Ni grade II. Hapa Sasa utakuta mazao ya Tanzania Yana Bei juu mno, Kama ilivyo kwenye mahindi. Mahindi ya Zambia Ni mazuri mno na Bei chini kidogo kuliko ya Tanzania. Soya ndio balaa lake bila angalau 1,200/kg mkulima anaona Bora atupe.

Suluhisho Ni Ushirika/Co-operatives societies. Kupitia ushirikani ndipo uhamasishaji wa kilimo unafanya, mazao yanaweza kukusanywa kwa Pamoja, kusafishwa inavyotakikana, kutafuta soko.

Tatizo jingine Ni wanasiasa na Serikali kuingilia kazi za Co-operative society mfano la mkuu wa wilaya ya Songwe.

Ushirika uliopo Sasa hivi umejaa wazee wasio na ubunifu, hawana soft marketing skills na hawajui hasa kazi ya Ushirika.

Now najifunza canning process, inshallah mwenyezi Mungu akijaalia in 5 years niwe nafunga njugu mawe.
Anayetaka njugu mawe kutoka Bukoba zipo karibu kukomaa, tutafutane.
JPEG_20210418_110455_7690349432620423500.jpg
 
Hivi sijui kwa nini wazungu wanapenda kuweka nyanya kwenye maharage, na sukari. Hii ladha ya nyanya na sukari kwenye maharage inanchefuaa!
 
Tatizo la bongo Sky Eclat Ni uwekezaji. Kuna uwekezaji mdogo kuanzia kwenye uzalishaji mpaka processing. Naweza kusema 60% ya wakulima wanalima chini ya vieka 5. wengi Sana eka 1-2 baaasi. Hapa Ni Lazima aforce kuweka high profit margin ili apate kitu. Ndio maana unakuta Kama huyo mchangiaji hapo juu alivyosema kuwa Kigoma wanauza 1.5 kg kwa 2500 sawa na 1,000/kg wakati DSM (ambapo Ni jiji la larger consumers wa mazao) Ni 2,000/kg.

Kwa sababu ya mtu mmoja mmoja kuzalisha kidogo kidogo gharama za kusafirisha kuunganisha mzigo zinakuwa juu sana. Ukumbuke pia wakulima hawasafishi vizuri Wala kuweka katika grades. Ukianza pia na kugrade ndipo usishangae kukuta grade 1 Ni 20% ya mzigo mzima, 60% Ni grade II. Hapa Sasa utakuta mazao ya Tanzania Yana Bei juu mno, Kama ilivyo kwenye mahindi. Mahindi ya Zambia Ni mazuri mno na Bei chini kidogo kuliko ya Tanzania. Soya ndio balaa lake bila angalau 1,200/kg mkulima anaona Bora atupe.

Suluhisho Ni Ushirika/Co-operatives societies. Kupitia ushirikani ndipo uhamasishaji wa kilimo unafanya, mazao yanaweza kukusanywa kwa Pamoja, kusafishwa inavyotakikana, kutafuta soko.
Tatizo jingine Ni wanasiasa na Serikali kuingilia kazi za Co-operative society mfano la mkuu wa wilaya ya Songwe.
Ushirika uliopo Sasa hivi umejaa wazee wasio na ubunifu, hawana soft marketing skills na hawajui hasa kazi ya Ushirika.

Now najifunza canning process, inshallah mwenyezi Mungu akijaalia in 5 years niwe nafunga njugu mawe.
Anayetaka njugu mawe kutoka Bukoba zipo karibu kukomaa, tutafutane.View attachment 1755251
Kwa ardhi tuliyonayo sekta ya kilimo ingetogen ajira nyingi sana. Chakula ni biashara yenye faida zikuzote kwani kila siku inahitajika. Bakhresa ame tajiri la kwa biashara ya chakula.

Vyama vya ushirika vikiwa na mitano mikubwa vinaweza kuajiri vijana wa purchasing and marketing ambao wanaweza kwenda nje ya nchi kutafuta masoko.

Wakulima waelimishwe kuwa lengo liwe ni kuzalisha grade 1 na kwa grade hii bei ni 1$ kwa kilo. Itasaidia kuongeza jitihada. Ni kama mtihani kila mtu anasoma apate A ikitokea umepata C unashukuru bora umefaulu.
 
Back
Top Bottom