Mazao yangu mwaka huu nitauza bei ghali sana

Mazao yangu mwaka huu nitauza bei ghali sana

SOEN

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2023
Posts
407
Reaction score
183
Ni msimu wa kilimo hasa kwa zao la mpunga kwa hapa nilipo. Nipo kijijini.

Kuna furaha kubwa sana kwa sisi wakulima mazao yakipanda bei sokoni! Thamani yetu na hali ya maisha inapanda sana.

Kundi ambalo lilisahaulika na kuwa kundi kwaajili ya kulisha watu mijini huku tukiumia mpaka tunaitwa wazee! Haha lakini kwa miaka hii miwili thamani yetu imeanza kuonekana mpaka tunapigiwa simu na jamaa zetu wa mjini waliulizia mvua kama zinanyesha.

Inachekesha sana mtu unaulizia mvua kuhofia mkulima kukosa mavuno hapana ni kwa yeye mtu wa Dar kuhofia bei ya mazao! Hivi hamjui kuwa mwaka jana kulikuwa na mvua kubwa sana jiulize bei ya mpunga wangu itakuwaje kwa hizi mvua za kwenye kikombe.

Issue sio mvua ila ni mkulima naye kaona thamani yake lakini pia standard ya maisha yake imepanda hii imekaa vyema sana.

Ndugu zangu wa mjini rudini kijijini mlime, leta mtaji wa hicho ukifanyacho uwekeze kwenye kilimo nenda hata Mkuranga tu hapo kalime mihogo, nazi, maembe, matunda kwa ujumla utapata kipato na chakula!

Hatutakuwa watumwa wenu wa kila siku mkae vijiweni mpige story mkirudi kijijini mtuletee mikate mtegemee kuondoka na debe la mchele thubutu.

Mwaka huu mpunga wangu tegemea kilo 5000 hutaki kausha, mpunga hauozi msisahau tunafuga bata, kuku ng’ombe nk hizo ni hela tegemea bei kuwa kubwa lakini kwa afanyaye kazi yake inayomwingizia kipato hatalalamika kuhusu chakula kupanda bei. Habari za asubuhi
 
😁😁😁😁 Hiyo hela utaipeleka wapi? Maana kama ni Bati na Sisi tunapandisha bei, kama cement tunapandisha bei, mafuta ya Kula hivyo hivyo, mwisho wa siku hela yote unatupatia.
 
Ni msimu wa kilimo hasa kwa zao la mpunga kwa hapa nilipo .. Nipo kijijini !

Kuna furaha kubwa sana kwa sisi wakulima mazao yakipanda bei sokoni ! Thamani yetu na hali ya maisha inapanda sana !
ni kwa afanyaye kazi yake inayomwingizia kipato hatalalamika kuhusu chakula kupanda bei ! Habari za asubuhi
Wewe sio mkulima ni chawa...subiri tu posho yako baada ya kuanzisha uzi huu kutoka kwa Bashe.
 
Ee TANZANIA sikia,

Mungu amekusudia mabaya JUU ya Dunia, inakuja njaa na ukame mkali ambao haijawahi tokea.

Mvua kidogo zilizonuesha juu ya nchi ni neema Kwa TANZANIA Ili kutunza chakula.

Tunzeni chakula sababu mvua haitonyesha Kwa kipindi kirefu,

Tuendelee na Maombi ya TOBA na REHEMA juu ya nchi yetu nzuri TANZANIA.

Amen
 
😁😁😁😁 hyo hela utaipeleka wapi? Mana kama ni Bati na Sisi tunapandisha bei, kama cement tunapandisha bei, mafuta ya Kula hvyo hvyo, mwisho wa sku hela yote unatupatia
Mkulima ndiyo kila kitu, basi jalibu kula hizo cement na bati
 
Tulime hiki kipindi mvua zinanyesha hatuna utaalamu wa kilimo cha umwagiliaji japo kwa wenye mitaji inawezekana
 
Na hayo ndiyo maisha mliyozea watu wa mjini Ulisikia wapi kijijini kuna chawa sisi jembe tu kaka badilikeni
 
Basi ujue kuwa Chakula kinahitajika nchini kaka Na huko Vietnam kuna wakulima pia
 
Debe moja la mahindi wauzieni kwa ng'ombe watatu-Magufuli.
 
Hahaha mwamba alijua hayo ingawa akabadili gear angani mahindi mjini walinunua bei mbovu sana
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] hyo hela utaipeleka wapi? Mana kama ni Bati na Sisi tunapandisha bei, kama cement tunapandisha bei, mafuta ya Kula hvyo hvyo, mwisho wa sku hela yote unatupatia
Mwenye mpunga atakoboa apike Haina haja ya mafuta, Kuna samaki huku niliko unapika bila mafuta Sasa wewe utakula bati, utakula cement?
 
Uza bei ghali tu mzee ata sisi wafanya biashara tunampango wa kupandisha vitu bei , tutakutana tu sokoni.
 
Mwambie aisee acha wale hela zao
 
Uza bei ghali tu mzee ata sisi wafanya biashara tunampango wa kupandisha vitu bei , tutakutana tu sokoni.
Hivyo vitu mtawapandishia wa mjini. Mnaumizana wenyewe. Wakulima chai ni anasa. Mabati na siment hayana mfumuko wa bei kama vyakuka.
Soda,juidi mikate huwatia kichefuchefu wakulima.
Thanks bashe kuwa na msimamo dhidi ya wanyontaji wa mjini.
 
Back
Top Bottom