Mazingaombwe yako aina nyingi inategemea yako vipi ya kumbi maalumu zilizoandaliwa kabisa kwa ajili ya mchezo huo,au ni yale ya tukusanyike kokote kule na tushuhudie mfano,barabarani,mashuleni n.k, neno mazinga likiwa na maana kadhaa za kibantu kama kizuizi,mafumbo,mipaka,maficho na n.k hutumika kama utambulisho wa mchezo huo ama sanaa hiyo lakini neno ombwe likiwa na maana ya wana kadamnasi,wapokeaji,maafikiano n.k hufanya maneno hayo mawili kuwa na ukamilifu katika uwasilishwaji wake.
Kwanini nimesema inategemea na maeneo ya mchezo huo unatendeka wap na utakuwa ni wa aina ipi kwa wakati huo,sababu hii michezo tukianza kwa miaka ya zamani huko kutizama michezo hio ilikuwaga ikifanyika katika sherehe za machifu,watemi lakini baadae ikaja katika sherehe za mavuno na baadae maeneo ya biashara kama magurio na mwisho zilipoanza shule sasa maonyesho hayo ya mazingaombwe yakafikia mashuleni..
Ukweli halisi wa uo mchezo ni wa dawa za viini macho zina tafutwa zinatengenezwa sehemu na fayari kwa kwenda kufanyiwa mchezo huo kwa mitindo tofauti tofauti,kwa namna nyingine unaweza kuita uganga maana mtu wa mazingaombwe yeye pale anapokuwa mchezoni anacheza na dawa lakini pia anakuwa na watumwa ambao watumwa hawa wanakuwa na bidhaa kede kede mahusi kwa mtindo wa michezo wanaouhitaji watumwa hawa wanakuwa misukule ambao nao wanakuwa katika formula ya dawa huwezi kuwaona kwa macho ya kawaida...
Labda kuwaona kwako ww uende na hiyo dawa na wakikubaini wanakutoa sababu wale misukule wanapokuwa mizungukoni kushughulika ww utawabaini na kuharibu mchezo mfano labda nitolee umemkabidhi mcheza mazingaombwe simu simu yako ww ataipokea atampatia msukule kuipeleka mahali fulani ambapo kwa baadae ndipo atadai iko kule huku atachobaki nacho mkononi ni mzizi tu wa dawa wakat huo ww utabakia kuiona kama simu yeye ataifanyia chochote kwa uharibifu eidha kuipasua au kivyovyote vile na utahakiki imeharibiwa lakin baadae ifafuatwa ile simu sasa asili iliyopelekwa kule na msukule kisha kuletwa...
Kwenye upasuaji na uchinjaji hutumia wanyama na dawa za viini macho anaweza pasuliwa mbwa mtu akawekwa pembeni nyie mkaona kama mtu anaweza chinjwa kuku mtu akawekwa pembeni nyie mkaona kama mtu akichinjwa,
Ni marufuku na ni hatari kwenda katika mazingaombwe ukiwa na kipande kuni kilichoingia jikoni na kubaki kipisi kwa mbele kule kama mkaa,ni marufuku kuigiza maneno ya mwana mazingaombwe anayotamka kwa kumfatilisha nyuma kila atoapa hatua ya neno,ni marufuku kugeuzia nguo ya ndani katika mkusanyiko wa mazingaombwe,pia ni marufuku kuingia kinyumenyume katika ukumbi wa mazingaombwe au mkusanyiko...
Sijajua kwa sasa kama bado mazingaombwe yanafanywa maana ile michezo ilikuwa inafanywa sana na vijana waliokuwa wanajifua katika kuzinoa na majaribu ya dawa kwenye makundi tofauti ya uganga na uchawi wengi wao ndio maana hutawakuta wakiwa na mabadiliko ya kimaisha japo walikuwa wanafanya maonyesho sana maana zilikuwa ni majaribio sana sanaa ya dawa na wengi tuu walikuwa wanafeli na kuwaletea madhara watu..
Nihitimishe kwa kusema mazingaombwe ni majaribio ya dawa za kiganguzi(uchawi) japo yapo mazingaombwe ya ujanja ujanja ila kiasili ni uchawi...asanteni sana.