Mazingaombwe ni ujuzi gani?

Ya kweli hayo Mkuu?
Bro alikua anapiga hizo mbanga kuweka makaratasi kwenye gazette lililokunjwa kisha inatokea misimbazi kadhaa kisha anairudisha ilipotoka michezo ya kucheza na kitambaa kisha linatokea ua (njiwa) lilikua sio jambo la hatari kwake na aliwahi kutuonyesha michezo ya kuleta ndizi, embe mpaka majani ya chai tena majani ya chai nakumbuka aliruhusu tupikie chai tunywe na tukafanya hivyo kutoka kusikojulikana ni ilikua jambo la kawaida kabisa, sasa alipomaliza shughuli zake town akarudi bush kule hawakumuelewa unajua siku zote nabii hakubaliwi nyumbani kwao na professional yake alikua ni Mwalimu wa Primary tu hadi anafariki ndio kazi alikua anaifanya kufundisha watoto kwa hio unafika muda humo humo class anapiga show ya bure anaingia bila chai kisha chaki inaletwa kutoka kusikojulikana, point ya kwanza walisema ni Mchawi point ya pili walisema vile vitu anavyoleta anaiba kwenye maduka yao yaan chuma ulete, kingine bro alikua hapendi kumfundisha mtu hizo mambo kabisa yaan hata ungemwambiaje akufundishe alikataa sababu yeye pekee ndio alikua anaijua hatari yake na hakuwahi kusema ni hatari kiasi gani kufanya vile
 
Hakuna uthibitisho wowote kwa kisicho kuwepo.

Hakuna dalili yeyote kwa kitu ambacho hakipo.

Kisichokuwepo hakipo kwa dalili yeyote ile wala kwa uthibitisho wowote ule.

Mungu hayupo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika yupo.

Alikuwa na balaa lake.
 
Wewe umeshindwa kuelewa ni namna gani huyo jamaa anaweza kumeza hiyo hela, Halafu unasema ni uchawi.

Umejuaje ni uchawi na si maarifa ambayo wewe huyaelewi?
Mi nimehitimisha kuwa ni uchawi..wew unaebisha ndio uniambie ni maarifa gani anatumia kuamisha ela kutoka mdomoni hadi mfukoni?
 
Toa codes kuhusu hiyo elimu.

Au kama ni mwiko kuweka hadharani njoo PM unipe tips kidogo.
 
Early 1990's ,wanamazingaombwe walikuja kijijini kwetu na makutano yalikuwa ndani ya Godowns ya mazao zike alizojenga Hayati Ally Hassan Mwinyi ambayo kwa wakati huo ilikuwa siyo msimu wa kahawa,Baba alipiga marufuku sisi watoto wake kwenda kwenye event ile, lakini kwa demo waliyotuonyesha shule ya msingi kwangu ilikuwa ngumu kuto kwenda.Wale jamaa walifanya mengi ila nikiwa nazubaa zubaa pale mbele nikiwa dogo sana,alikuja na kuonekana ametoa shilingi kwenye pua,ikawa story kubwa kijijini na Baba akapata taarifa,kipigo nilichopata sijawahi sahau
 
Wachungaji wengi tu mbona Ni wanamazingaumbwe si mkawaulize!
Na kuna mtu anafundisha hayo mambo yupo pale mkata njia panda ya kwenda kwa msisi tanga!
 
Kunq huyo mwamba wa kuitwa chriss angel, mmarekani huyu, kama ni mazingaombwe basi labda yalizaliwa kwao, huwa ananiacha mdomo wazi.
Yule hamna kitu pale.
Nimeshamfatilia sana ni muongo, na ni tricks tu anatumia.
Hana mazingaombwe yoyote
 
Sawa,.Lakini nauliza ni elimu gani Ile?

Kwanini mtu awe kama amepumbazwa?
Inaitwa white magic hata mitume na manabii wa miujiza wanafanya hizi mambo ukisoma ujuzi huo utafundishwa vyote ikiwemo mind control, magic trick,nk.
Hizi ni elimu chache kwa wanaziitaji.
Kuna elimu za ujuzi mbalimbali hata wwe ukitaka unasoma unajifunza mfano.
Kuuita mtu mkubwa kama mwembe ukufuate au ukimbie na watu wanashuhudia,kuna kupotea ghafla watu wasikuone hii kwa wanaofanya ninja wanasoma, kuna kupenya kwenye ukuta wowote ukaingia au kutoka ndani ya jengo bila kubomoa ukuta,kuna kuzuia nguvu ya risasi kisu isipenye mwilini,kuna kusoma mawazo ya mtu ukajua anawaza nini.nk hizi ni elimu kama zingine tu unajifunza
 
Hakuna uchawi hapo ni ujanja tu wa kuwazidi akili.
Ngoja nikuelezee wanachokifanya hapo,yule anayefanya huo mchezo anakuwa amevaa shati lenye mikono mirefu na ndani ya hiyo mikono ya shati anakuwa amezificha hizo noti kwa hiyo anavyokuwa anaingiza mikono yake kwenye bahasha huku akijifanya kuomba hapo anakuwa abazishusha hizo hela taratibu bila ya watazamaji kujua helazikishashuka ndio atajifanya kuita mtazamaji mmoja aje kuzitoa.
Siku ukikutana nao tena ukitanga kuwapa changamoto waambie wafanyie kwenye sahani iliyo wazi badala ya kutumia bahasha uone kama watafanya
 
Toa codes kuhusu hiyo elimu.

Au kama ni mwiko kuweka hadharani njoo PM unipe tips kidogo.
Mkuu; hakuna cha eti ni mwiko wowote au nini. Wala huko PM siji/siendi. Naweka hapa👇👇
1. Mazingaombwe ni ujanja wa kuficha na kufichua. Unaficha sirini na unafichua hadharani mbele za watazamaji.
Kwa mfano gari kushindwa kuondoka: Mwoneshaji anajitahidi sana tairi isikanyage chini walau hata kwa sm0.3. Hakuna tairi iliyogusa ardhi -Gari itaendaje? Ni muhimu sana dereva anayeendesha gari la maonesho awe ni sehemu ya maonesho hayo.
 
N

Ndo ubaya wa kumwelewesha mtu ambaye anaangalia Mazingaombwe youTube.

Hiyo ndizi ilishikwa na Mwanafunzi na ilikuwa nzima kabisa.

Kuna baadhi ya Mazingaombwe kweli ni tricks ila mengine yamevuka ukomo.
Mkuu usiwe mbishi mbinu zote za mazingaombwe huwa zinafanana na huwa zinasambaa duniani kote,ukienda America utazikuta,ukienda India utazikuta na ukija Africa utazikuta mbinu hizo hizo.
Hiyo ndizi kama alikuja nayo mwenyewe kuna namna inakuwa imechokonolewa kwa ndani,na nje pia inakuwa ishakatwa halafu inaunganishwa na gundi yenye rangi sawa na ndizi ili kukuzubaisha wewe usione kitu.
Ukitaka kujua hilo siku ukiwaona waambie unakuja na ndizi yako mpya kutoka gengeni waifanyie kazi kama watakubali
 
Kuna elimu au Ujuzi wa magic na unafundishwa ukitaka sema tukupeleke kwa mtaalam
 
Ni tricks ndio ushawah ona mtu anakatwa kichwa live kinatengwa na Anaongea?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…