Mazingaombwe ni ujuzi gani?

Toa hiyo elimu kuhusu namna unavyoweza kusoma majina yaliyokunjwa kwenye karatasi au kama haupo willing kuiweka public nicheki PM. Mana nipo interested walau kujua baadhi ya tricks.

Napenda kujifunza vitu vipya kila siku.
Mkuu; wewe ni mdadisi sana. Kongole. Unataka uitumie kujipatia maokoto? Nimesema hapo juu PM siji naweka hapa-hapa hadharani ujinga/ujanja unaotumika:
1. Ni lazima/Sharti (Muhimu sana hii) awepo mmoja kati yenu msiyemjua/kumdhania ninafahamiana naye awe naye ameandika na ataandika kitu tutakachokuwa tumekubaliana kabla ya onesho. Huyu ni msiri wangu.
Mimi nitakapofika hapo mlipo na mkiwa tayari mmeshaandika mliyo yaandika na kuzikunja karatasi; nitachukua karatasi lolote miongoni mwa makaratasi yenu mliyokunja-kunja. Nitasoma kwa sauti kwa kuliweka kisogoni kwangu bila hata ya kulikunjua kile msiri wangu alichoandika. Naye atanyosha mkono kukubali kwamba ameandika yy. Then nitalifungua na kulisoma kiukweli. Tahadhari; Hakuna mtu kukaa nyuma yangu-manake siri itabumbuluka. Kuanzia hapo nitakuwa nasoma kile nilichokisoma kwenye karatasi la kwanzaalilokubali msiri wangu. Kamchezo hako ka kijinga kataendelea vivyo hivyo mpaka namaliza karatasi zote. Siri inabaki kati yangu mimi na Msiri wangu. Aaamen.
 
Ni tricks ndio ushawah ona mtu anakatwa kichwa live kinatengwa na Anaongea?
Ndio -tena sio mara moja. Jitahidi uhudhurie Maadhimisho ya kitaifa au kikanda(maonesho) e.g. Nane-Nane pale Uwanja wa Themi Arusha au Sabasaba pale Dodoma. (Hicho kichwa huwekwa kwenye beseni na kuzungushiwa pamba au kitambaa cheupe -ujiulize why ? si angekatwa kama kuku tu halafu aachwe hapo?? .Ukienda kwenye matamasha au maadhimisho ya Kitaifa Utaweza kubahatika kuona. Yapo pia maonesho ya Mtu anakatwa panga kichwani hadi linazama nusu ya kichwa au mtu anachomwa kisu ubavuni hadi kinatokeza upande wa pili na damu imevuja nyingi na bado anaendelea kuongea kwa mbwembwe zote na maonesho yake.
 
Kama mpaka hapo hajaelewa basi tena: Case dismissed. Cooooooourt.
 
Wachungaji wengi tu mbona Ni wanamazingaumbwe si mkawaulize!
Na kuna mtu anafundisha hayo mambo yupo pale mkata njia panda ya kwenda kwa msisi tanga!
Uko sahihi,pia hata wale waganga wa kienyeji wa mjini wengi wanatumia mbinu kama hizi za wanamazingaombwe kuwarubuni watu ila wengi wao hawana dawa yoyote na wala hawajui chochote kuhusu tiba.
Kwa mfano kuna mchezo mmoja hivi anaweza akachukua yai akalipasua kitundu kidogo kisha anatoa nje kile kiini na yale majimaji ya yai kwa kuvuta na bomba la sindano/syringe baada ya hapo wanaingiza damu ndani kwa kutumia hilo hilo bomba la sindano kisha wakishamaliza wanaziba hilo tundu kwa kutumia maranda ya mbao wanayanasisha na gundi kisha wanapiga msasa yai linakuwa kama jipya kwa nje.
Sasa mteja akienda atajifanya kupiga ramli kwa kutumia hilo yai kisha baadae analivunja linatoka damu kisha anakutafsiria kwamba ukiona yai linatoka damu ujue maisha yako yapo hatarini maana yake wabaya wako wako karibu kukumaliza kinachofuata hapo anakutoa mpunga ili akupe dawa ya kuzuia mashambulizi ya adui,hahahaha
 
Dogo hujawahi kuona Mazingaombwe kakojoe ulale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…