Tangu nilipogundua umuhimu wa mazoezi kwenye mwendo wa kawaida wa maisha, nimejaribu hili na lile, kuona linalonifaa zaidi. Katika jaribujaribu mara kwa mara nimeongeza vikolezo mbalimbali kwenye mazoezi yangu na kuyaboresha kidogo. Nimeongeza vikolezo hivyo kwa malengo ambayo binafsi nayaona ni ya muhimu kwenye zoezi langu.
Kwa mtazamo wangu lazima nijue kiasi cha mazoezi niliyofanya. Hivyo natafuta namna ya kupima mazoezi yangu. Basi hapo nimejaribu kutumia fitness bands, na apps kama vile Endomondo pia Google fit kwa kutembea na kukimbia nk. Napenda pia kujiburudisha ndani ya zoezi. Napenda kutumia muziki ambao sio tu unaniburudisha wakati wa zoezi, lakini pia mwendo wa muziki unanipa msukumo wa pekee na wakati mwingine rhythm ya kwenda na zoezi langu. Napenda kuwa na zana sahihi, vitu ambavyo havitaleta usumbufu kwenye zoezi. Napenda kufanya zoezi ndani ya muda sahihi niliochagua, na mara nyingi nakwepa usumbufu wakati wa zoezi. Kuna suala la usalama ambalo pia linaniondolea wasiwasi wakati wa zoezi.
Pamoja na hayo yote nimegundua pia kuwa mambo mengine mengi yanaweza kuathiri mazoezi yangu. Kwa mfano, kuwa kwenye mood mbaya, ninapokua nimezongwa na mawazo, nashindwa kabisa kufanya mazoezi, sijui kwa nini. Hali ya hewa wakati mwingine umenikwamisha. Pengine mvua, kuna madimbwi, joto kali nk. Pia nahitaji kuwa katika hali njema kimwili. Kwa mfano wakati mwingine nimeshiba, au nina kinywaji tumboni, mwili unawasha, naumwa na kichwa, goti nk
Baada ya kujaribu mazoezi ya aina nyingi kama vile jogging kutembea kunyanyua mawe nk, hatimaye nikagundua kuwa zoezi la kuruka kamba linazingatia vigezo vyangu. Hivyo nikajaribu kwa namna mbalimbali kuliboresha zaidi, kwa kuyapunguza yanayoweza kuliathiri, na kuyaongeza yale yanayoboresha zoezi, nikatokea na mtindo huu.
Baada ya hapo nafanya mazoezi mengine madogomadogo kama vile push-ups, squats stretch mbalimbali na kucheza muziki. Kisha naoga maji ya moto.
Natamani sana kupata maneno ya kukuelezea ninavyojisikia baada ya hapo.
Mtindo huu wa mazoezi ni mzuri sana, maana unakuzuia kutokatoka hasa wakati huu wa Covid 19
Hapa nimeona wadau wengine wanaoelezana kuhusu zoezi hilo.
Kwa mtazamo wangu lazima nijue kiasi cha mazoezi niliyofanya. Hivyo natafuta namna ya kupima mazoezi yangu. Basi hapo nimejaribu kutumia fitness bands, na apps kama vile Endomondo pia Google fit kwa kutembea na kukimbia nk. Napenda pia kujiburudisha ndani ya zoezi. Napenda kutumia muziki ambao sio tu unaniburudisha wakati wa zoezi, lakini pia mwendo wa muziki unanipa msukumo wa pekee na wakati mwingine rhythm ya kwenda na zoezi langu. Napenda kuwa na zana sahihi, vitu ambavyo havitaleta usumbufu kwenye zoezi. Napenda kufanya zoezi ndani ya muda sahihi niliochagua, na mara nyingi nakwepa usumbufu wakati wa zoezi. Kuna suala la usalama ambalo pia linaniondolea wasiwasi wakati wa zoezi.
Pamoja na hayo yote nimegundua pia kuwa mambo mengine mengi yanaweza kuathiri mazoezi yangu. Kwa mfano, kuwa kwenye mood mbaya, ninapokua nimezongwa na mawazo, nashindwa kabisa kufanya mazoezi, sijui kwa nini. Hali ya hewa wakati mwingine umenikwamisha. Pengine mvua, kuna madimbwi, joto kali nk. Pia nahitaji kuwa katika hali njema kimwili. Kwa mfano wakati mwingine nimeshiba, au nina kinywaji tumboni, mwili unawasha, naumwa na kichwa, goti nk
Baada ya kujaribu mazoezi ya aina nyingi kama vile jogging kutembea kunyanyua mawe nk, hatimaye nikagundua kuwa zoezi la kuruka kamba linazingatia vigezo vyangu. Hivyo nikajaribu kwa namna mbalimbali kuliboresha zaidi, kwa kuyapunguza yanayoweza kuliathiri, na kuyaongeza yale yanayoboresha zoezi, nikatokea na mtindo huu.
- KAMBA: ya kawaida kabisa. Mwanzoni nilikua natumia kamba fulani ambayo ina counter, yaani inahesabu yenyewe wakati kamba inapozunguka. Niliipenda sana hiyo, lakini baadae nikagundua kuwa ina mapungufu. Mara nyingi inakua na ubovu, na inaruka namba, inahesabu vibaya na wakati mwingine haiesabu kabisa. Kamba hizo zenye counter zinakua nyembamba sana na hazina uzito ninaohitaji kwenye zoezi. Hivyo nilipogeukia kamba nyingine za kawaida, nikaona lazima nitafute namna nyingine ya kuhesabu kamba zangu.
- SIMU: yangu ya Tecno nimekua nikiitumia kwa mazoezi mengine kama kukimbia na kutembea. Nilipoanza zoezi la kuruka kamba, nikaanza kujaribu kutafuta apps mbalimbali ambazo zinaweza kuhesabu kuruka kwangu Mwaanzo nilitumia app inajulikana kama skeepjumping, ambayo baadae niliona ina mapungufu, wakati mwingine katikati ya shughuli inaacha kuhesabu, au inaanza mwazo. Baadae nikawa natumia nnyinggine inayojulikana kama Jumpro na hii ndio ninayoitumia wakati huu. Hii ni nzuri, isipokua wakati wa kuanza kuitumia lazima ufanye calibration kulingana na mtikisiko wa mwili wako unaporuka. Inaweza ikawa inahesabu mara mbili kwa mruko mmoja au isihesabu kabisa, inategemea umeifanyia calibration namna gani.
- ARMBAND: yangu ya kiyeboyebo, lakini inayonisaidia. Haka kamkoba nachomeka simu ndani yake, kisha nafungia kwenye mkono, ili ninaporuka, mruko uweze kuregister kwenye simu. Pengine hapa unaweza kuona inavyo valiwa Awali nilikua natumia kwa jogging, lakini sasa natumia kwa kuruka kamba.
- HEADPHONES: za bluetooth, nilinunua sabasaba. Awali nilikua natumia headphones zenye waya, zinafaa, lakini niliona kama vile waya unasumbua kidogo. Sipendi kabisa viheadphone vya kuchomeka masikioni havinipi raha, napenda hizi za kufunika masikio. Baada ya kuzi-pair na simu yangu, naweza kuisikia vizuri “Jumpro” inavyohesabu, kwahiyo najua nipo wapi katika round yangu ya kuruka, na pia nasikia muziki. Kwenye simu nimeinstall pia App ya kuchezesha muziki inayoitwa Musicolet hii ni app nzuri ya kuorganise miziki kwenye simu na kuichezesha. Unaweza kutengeneza playlists na queues ambapo kwa haraka unaweza kuchagua aina ya miziki unayotaka kusikia.
- BLUETOOTH KEYBOARD: Hii nilinunua kwa malengo mengine, lakini kwasababu inaunganisha vizuri sana na simu, naitumia moja kwa moja ku-control muziki wangu wakati wa zoezi. Inaniwezesha kuongeza sauti au kupunguza kwa miziki yenye namna tofauti za volume. Pia inaniwezesha kuskip forward au backward, ku-pause na kuendelea. Ku-mute nk. Hivyo nikisha ifungia simu kwenye Armband sihitaji kuitafuta kwaajili ya kurekebisha mambo, natumia keyboard hii.
- SOKSI: pamoja nanguo nyingine ndogo ambayo kimaadili si vizuri kuiweka hapa. Zoezi langu nafanyia chumbani. Nafunga mlango kisha nang’oa nguo zote nabaki na hizo ndogo za aina mbili. Hii inanipunguzia mambo ya kufua nguo zenye majasho ya mazoezi. Jasho kwa kweli linatoka sana, linaenda sakafuni na soksi hizi zinazuia kuteleza nk.
Natamani sana kupata maneno ya kukuelezea ninavyojisikia baada ya hapo.
Mtindo huu wa mazoezi ni mzuri sana, maana unakuzuia kutokatoka hasa wakati huu wa Covid 19
Hapa nimeona wadau wengine wanaoelezana kuhusu zoezi hilo.