Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
- Thread starter
- #21
Sasa hatukuwahi hata kuvuta pumzi uzuri mara jiwe lingine liliporomoshwa, na hilo lilianguka kwa mshindo mkuu katikati ya jahazi yetu, ikavunjika vipande vipande. Abiria na mabalharia wote waliokuwamo wakazama baharini pamoja na mimi mwenyewe; walakini nilipata bahati nzuri ya kuibuka tena bila ya kuumia mahali. Nikashika kipande cha ubao kilichokuwa kikielea nikapata kuogelea, na mara ile ile nikapigwa na wimbi kunipeleka kisiwani. Pwani zake zilikuwa zimechongoka sana tena zilikuwa na mawe mawe, lakini nikapanda hivyo hivyo kwa kutamba taratibu mpaka nikafika juu salama, nikajilaza penye majani mororo, nikapumzıka.
Nilipoondoka nikaanza kwenda huku nikikichungua kisiwa, hata mwisho nikajiona nimefika kwenye bustani nzuri kulikokuwa na miti iliyozaa matunda na maua kochokocho, na kijito cha maji safi meupe kama kioo yakipita chini ya vivuli vyao. Hata usiku ulipoingia nikachagua mahali pazuri nikalala; lakini nilikuwa nikigutuka mara kwa mara na kuangalia huku na huku kwa woga, na hasa nikikumbuka kuwa ni peke yangu katika nchi ya ugeni, nikatamani sana niweko kwetu. Lakini huo usingizi nilioupata ulikuwa mtamu tena wa raha. Sasa kulipokucha nikawa mwana mume kamili na uwoga wote ukanitoka nikaanza kuzungukazunguka katika miti mara ingine, lakini kila nikizunguka hivyo nafsi yangu ilikuwa kama nitakayeona kitu. Basi nikazidi kuendelea mbele ndani ya kile kisiwa hata mwisho nikaja nikamtokea mzee mmoja aliyejikunja, tena mnyonge sana amekaa ukingoni pa mto. Kwanza nilimdhania kuwa ni baharia aliyevunjikiwa jahazi kama mimi. Nikamwendea kumwamkia lakini hakunijibu neno ila aliinamisha kichwa chake kuniitikia. Kisha nikamwuliza anafanya nini hapo. Ndipo akanifanyia ishara kuwa anataka kuvuka ule mto aende akachume matunda, na katika kumwangalia kwangu nikaona kama aniambiaye nimbebe nimvushe. Basi nikahuhurumia uee na unyonge wake nikambeba mabegani kumvusha, hat a nilipofika naye ng’ambo ya pili nikainama kusadi ashuke kwa urahisi, nikamwambia, ‘Sasa shuka.’ Lakini badala ya kushuka na kusimama kwa miguu yake mwenyewe (nh'u, hata sasa nikikumbuka hucheka!) kiumbe yule niliyemwona kuwa mkongwe akazidi kuniganda mabegan1 mwangu, tena akanifunga na miguu yake shingoni mwangu ikanibana sana hata nilikuwa siwezi kutoa pumzi. Na hivyo nilishindwa nguvu kwa woga, nikaanguka chini
nikazimia.
Hata nilipopata fahamu nikaona adui yangu bado yuko pale pale mahali pake, ijapokuwa alinilegezea kidogo ili nipate pumzi. Basi alipoona kuwa naanza kufufuka, akanipiga mateke hata ikanilazimu kuondoka na kwenda naye chini ya miti huku aende akichuma matunda ayatakayo akila. Mambo hayo yalikuwa yakiendelea mchana kutwa, na usiku nikilala huwa kama mfu kwa kuchoka, na yeye alikuwa akilala karibu yangu huku amenibana barabara shingoni. Na asubuhi kukicha haachi kunipiga mateke mpaka niamke, nianze tena mwendo wangu kwa hasira na uchungu.
Siku moja nikatukia kupita chini ya mti ambao chini yake kulikuwa na mamumunye makavu, nikatwaa moja nikatoa mbegu zake nikafanya kibuyu. Halafu yake nikakichukua na kukikamulia maji ya zabibu zilizokuwa zikilewalewa vichakani. Hata kilipojaa nilikiacha nikakiegemeza katika panda ya mti, na baada ya siku chache nilimchukua yule mzee nikaenda naye njia ile ile, na nilipofika huko nilichukua kile kibuyu changu nikanywa kiasi, na hivyo nilipata kuusahau uzito wa mzigo wangu niliouchukia, nikaanza kuimba na kuchezacheza. Basi siku hiyo yule mzee aliyeniganda
allpoona kwamba nikinywa maji yale ya zabibu huchangamka tena huweza kumchukua kwa urahisi zaidi ya siku zote, akanyosha mikono yake iliyo ngozi tupu na kushika kibuyu. Kwanza akaonja kidogo kwa hadhati, lakini halafu yake akagugumia yote hata tone lisibaki.
Hicho kibuyu nacho kilikuwa kikubwa, na mvinyo nao uilikuwa mkali sana hata naye pia akaanza kuimba na kuchezacheaza na nikiwa furaha sana kuona zile kucha za chuma zilizo katika vidole vya miguu yake ya kijini zilianza kulegea. Na kwa nguvu zangu zote nikamtupa chini na kutwaa jiwe nikamwua. Nilifurahi mno kutokana na balaa la shetani huyo mzee, nikaenda Kutukaruka mpaka pwani, ambako kwa bahati kubwa, nikakutana mabaharia waliotia nanga kusudi waje kule kisiwani kwa kula matunda na kuteka maji.
Wakasikiliza habari zangu kwa kustaajabu sana, nao wakasema ‘Uliangukia mikononi mwa Mzee wa Bahari, naye alikuhurumia sana kwa kutokunyonga kama vile anavyomnyonga kila mtu anayemchukua mabegani mwake. Kisiwa hiki chajulikana sana kwa visa vyake viovu, wala hapana mfanyaji biashara au baharia ateremkaye pwani akawa mbali na mwenziwe. Basi tulipokwisha kusema wakanichukua kunipeleka jahazini mwao, na huyo nahodha wao alinipokea kwa uzuri, na mara tukang’oa nanga kusafiri Baada ya siku kadha wa kadha tukafika katika bandari ya mji mkubwa uliostawi sana, ambao majumba yake yalijengwa kwa mawe, tukatia nanga. Basi mmoja katika wale wafanyaji biashara, ambaye alikuwa rafiki yangu sana humo njiani, akanichukua pwani; akaenda kunionyesha nyumba za kupanga wafanyaji biashara wageni zilizojengwa kando ya mji. Halafu akanipa na gunia moja kubwa, na akanionyesha watu wengine waliokuwa na magunia yao sawasawa na mimi. Akaniambia, ‘Nenda pamoja nao, ukafanye kama hivyo watakavyofanya, ila tahadhari usiwapotee, kwani ukipotea maisha yako yatakuwa katika hatari.
Baada ya hivi akanipa na chakula cha njiani, akaniaga. Nami nikatoka nikaenda pamoja na wale wenzangu wapya hata tukafika mahali penye minazi mingi iliyoshikana. Sasa nikafahanmu maana ya safari ile kuwa tumekwenda kujaza nazi magunia yetu. Nikiitazama ile minazi jinsi ilivyo mirefu mno na katikati miembamba, kisha yateleza sana, sikujua kabisa la kufanya. Na tena juu ya vilele vya minazi yote mlikuwa na manyani na matumbiri, wakirukaruka upesi upesi kwa kufadhaika kutoka mnazi huu hata mnazi ule; wakituchukulia wageni tu kisha twawaudhi mno kwa sura zetu. Basi wale wenzangu kwa hekima yao wakaokota mawe kuwarushia, na wale nyani walisumbuliwa mno hata nao wakapenda kujilipiza, ndipo wakaanza kukata nazi wakitutupia kwa hasira na chuki, na kwa njia hiyo tukapata kujaza magunia yetu, na kama si hivyo hatungalizipata. Basi tulipokwisha, kupata kadiri tulizoweza kuchukua tukarudi mjini. Rafiki yangu akanunua zile nazi zangu na kunishauri nizidi kuendelea kufanya kazi hiyo, mpaka nipate fedha za kutosha kunipeleka kwetu. Nami nikafanya hivyo, na baada ya si siku nyingi nikapata fedha za kitita. Sasa nikasikia kuwa kuna jahazi ya biashara ilivo tayari kuondoka, nikamuaga rafiki yangu nikaenda kujipakia pamoja na magunia ya nazi nyingi nilizokuwa nazo. Kwanza tukapitia katika kisiwa kilichopandwa pilipili, kutoka hapo tukaenda kisiwa cha Komari kilichoko Bara Hindi, ambako hupatikana udi mzuri. Hapo nikabadilisha nazi zangu kwa pilipili na udi. Kisha nikaenda mahali panapozamiwa lulu nikaajiri wazamiaji lulu. Hao wazamiaji lulu wangu walikuwa na bahati sana, na kwa muda mchache nikapata lulu nyingi mno, tena kubwa kubwa na safi. Nikarudi kwa furaha Baghdadi pamoja na mali hizi zote, nikaziuza kwa fedha nyingi mno na sikusahau kamwe kutoa fungu la kumi kuwapa masikini. Na baada ya hivi nikakaa kupumzika na kujifurahisha kwa anasa zote nilizoweza kupata kwa utajiri wangu.
Sindbad alipokwisha kutoa hadithi yake, akaamuru kwamba Hindbad apewe reale mia za dhahabu, na halafu wale wageni wote wakaaga, wakatoka. Lakini siku ya pili yake baada ya kuliwa karamu, Sindbad akaanza kutoa habari za safari yake ya sita, kama hivi ifuatavyo.
Nilipoondoka nikaanza kwenda huku nikikichungua kisiwa, hata mwisho nikajiona nimefika kwenye bustani nzuri kulikokuwa na miti iliyozaa matunda na maua kochokocho, na kijito cha maji safi meupe kama kioo yakipita chini ya vivuli vyao. Hata usiku ulipoingia nikachagua mahali pazuri nikalala; lakini nilikuwa nikigutuka mara kwa mara na kuangalia huku na huku kwa woga, na hasa nikikumbuka kuwa ni peke yangu katika nchi ya ugeni, nikatamani sana niweko kwetu. Lakini huo usingizi nilioupata ulikuwa mtamu tena wa raha. Sasa kulipokucha nikawa mwana mume kamili na uwoga wote ukanitoka nikaanza kuzungukazunguka katika miti mara ingine, lakini kila nikizunguka hivyo nafsi yangu ilikuwa kama nitakayeona kitu. Basi nikazidi kuendelea mbele ndani ya kile kisiwa hata mwisho nikaja nikamtokea mzee mmoja aliyejikunja, tena mnyonge sana amekaa ukingoni pa mto. Kwanza nilimdhania kuwa ni baharia aliyevunjikiwa jahazi kama mimi. Nikamwendea kumwamkia lakini hakunijibu neno ila aliinamisha kichwa chake kuniitikia. Kisha nikamwuliza anafanya nini hapo. Ndipo akanifanyia ishara kuwa anataka kuvuka ule mto aende akachume matunda, na katika kumwangalia kwangu nikaona kama aniambiaye nimbebe nimvushe. Basi nikahuhurumia uee na unyonge wake nikambeba mabegani kumvusha, hat a nilipofika naye ng’ambo ya pili nikainama kusadi ashuke kwa urahisi, nikamwambia, ‘Sasa shuka.’ Lakini badala ya kushuka na kusimama kwa miguu yake mwenyewe (nh'u, hata sasa nikikumbuka hucheka!) kiumbe yule niliyemwona kuwa mkongwe akazidi kuniganda mabegan1 mwangu, tena akanifunga na miguu yake shingoni mwangu ikanibana sana hata nilikuwa siwezi kutoa pumzi. Na hivyo nilishindwa nguvu kwa woga, nikaanguka chini
nikazimia.
Hata nilipopata fahamu nikaona adui yangu bado yuko pale pale mahali pake, ijapokuwa alinilegezea kidogo ili nipate pumzi. Basi alipoona kuwa naanza kufufuka, akanipiga mateke hata ikanilazimu kuondoka na kwenda naye chini ya miti huku aende akichuma matunda ayatakayo akila. Mambo hayo yalikuwa yakiendelea mchana kutwa, na usiku nikilala huwa kama mfu kwa kuchoka, na yeye alikuwa akilala karibu yangu huku amenibana barabara shingoni. Na asubuhi kukicha haachi kunipiga mateke mpaka niamke, nianze tena mwendo wangu kwa hasira na uchungu.
Siku moja nikatukia kupita chini ya mti ambao chini yake kulikuwa na mamumunye makavu, nikatwaa moja nikatoa mbegu zake nikafanya kibuyu. Halafu yake nikakichukua na kukikamulia maji ya zabibu zilizokuwa zikilewalewa vichakani. Hata kilipojaa nilikiacha nikakiegemeza katika panda ya mti, na baada ya siku chache nilimchukua yule mzee nikaenda naye njia ile ile, na nilipofika huko nilichukua kile kibuyu changu nikanywa kiasi, na hivyo nilipata kuusahau uzito wa mzigo wangu niliouchukia, nikaanza kuimba na kuchezacheza. Basi siku hiyo yule mzee aliyeniganda
allpoona kwamba nikinywa maji yale ya zabibu huchangamka tena huweza kumchukua kwa urahisi zaidi ya siku zote, akanyosha mikono yake iliyo ngozi tupu na kushika kibuyu. Kwanza akaonja kidogo kwa hadhati, lakini halafu yake akagugumia yote hata tone lisibaki.
Hicho kibuyu nacho kilikuwa kikubwa, na mvinyo nao uilikuwa mkali sana hata naye pia akaanza kuimba na kuchezacheaza na nikiwa furaha sana kuona zile kucha za chuma zilizo katika vidole vya miguu yake ya kijini zilianza kulegea. Na kwa nguvu zangu zote nikamtupa chini na kutwaa jiwe nikamwua. Nilifurahi mno kutokana na balaa la shetani huyo mzee, nikaenda Kutukaruka mpaka pwani, ambako kwa bahati kubwa, nikakutana mabaharia waliotia nanga kusudi waje kule kisiwani kwa kula matunda na kuteka maji.
Wakasikiliza habari zangu kwa kustaajabu sana, nao wakasema ‘Uliangukia mikononi mwa Mzee wa Bahari, naye alikuhurumia sana kwa kutokunyonga kama vile anavyomnyonga kila mtu anayemchukua mabegani mwake. Kisiwa hiki chajulikana sana kwa visa vyake viovu, wala hapana mfanyaji biashara au baharia ateremkaye pwani akawa mbali na mwenziwe. Basi tulipokwisha kusema wakanichukua kunipeleka jahazini mwao, na huyo nahodha wao alinipokea kwa uzuri, na mara tukang’oa nanga kusafiri Baada ya siku kadha wa kadha tukafika katika bandari ya mji mkubwa uliostawi sana, ambao majumba yake yalijengwa kwa mawe, tukatia nanga. Basi mmoja katika wale wafanyaji biashara, ambaye alikuwa rafiki yangu sana humo njiani, akanichukua pwani; akaenda kunionyesha nyumba za kupanga wafanyaji biashara wageni zilizojengwa kando ya mji. Halafu akanipa na gunia moja kubwa, na akanionyesha watu wengine waliokuwa na magunia yao sawasawa na mimi. Akaniambia, ‘Nenda pamoja nao, ukafanye kama hivyo watakavyofanya, ila tahadhari usiwapotee, kwani ukipotea maisha yako yatakuwa katika hatari.
Baada ya hivi akanipa na chakula cha njiani, akaniaga. Nami nikatoka nikaenda pamoja na wale wenzangu wapya hata tukafika mahali penye minazi mingi iliyoshikana. Sasa nikafahanmu maana ya safari ile kuwa tumekwenda kujaza nazi magunia yetu. Nikiitazama ile minazi jinsi ilivyo mirefu mno na katikati miembamba, kisha yateleza sana, sikujua kabisa la kufanya. Na tena juu ya vilele vya minazi yote mlikuwa na manyani na matumbiri, wakirukaruka upesi upesi kwa kufadhaika kutoka mnazi huu hata mnazi ule; wakituchukulia wageni tu kisha twawaudhi mno kwa sura zetu. Basi wale wenzangu kwa hekima yao wakaokota mawe kuwarushia, na wale nyani walisumbuliwa mno hata nao wakapenda kujilipiza, ndipo wakaanza kukata nazi wakitutupia kwa hasira na chuki, na kwa njia hiyo tukapata kujaza magunia yetu, na kama si hivyo hatungalizipata. Basi tulipokwisha, kupata kadiri tulizoweza kuchukua tukarudi mjini. Rafiki yangu akanunua zile nazi zangu na kunishauri nizidi kuendelea kufanya kazi hiyo, mpaka nipate fedha za kutosha kunipeleka kwetu. Nami nikafanya hivyo, na baada ya si siku nyingi nikapata fedha za kitita. Sasa nikasikia kuwa kuna jahazi ya biashara ilivo tayari kuondoka, nikamuaga rafiki yangu nikaenda kujipakia pamoja na magunia ya nazi nyingi nilizokuwa nazo. Kwanza tukapitia katika kisiwa kilichopandwa pilipili, kutoka hapo tukaenda kisiwa cha Komari kilichoko Bara Hindi, ambako hupatikana udi mzuri. Hapo nikabadilisha nazi zangu kwa pilipili na udi. Kisha nikaenda mahali panapozamiwa lulu nikaajiri wazamiaji lulu. Hao wazamiaji lulu wangu walikuwa na bahati sana, na kwa muda mchache nikapata lulu nyingi mno, tena kubwa kubwa na safi. Nikarudi kwa furaha Baghdadi pamoja na mali hizi zote, nikaziuza kwa fedha nyingi mno na sikusahau kamwe kutoa fungu la kumi kuwapa masikini. Na baada ya hivi nikakaa kupumzika na kujifurahisha kwa anasa zote nilizoweza kupata kwa utajiri wangu.
Sindbad alipokwisha kutoa hadithi yake, akaamuru kwamba Hindbad apewe reale mia za dhahabu, na halafu wale wageni wote wakaaga, wakatoka. Lakini siku ya pili yake baada ya kuliwa karamu, Sindbad akaanza kutoa habari za safari yake ya sita, kama hivi ifuatavyo.