Pre GE2025 Mbagala: RC Chalamila apokelewa kwa Wimbo "Bao 1 milioni 10 lakini barabara mbovu"

Pre GE2025 Mbagala: RC Chalamila apokelewa kwa Wimbo "Bao 1 milioni 10 lakini barabara mbovu"

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Wakazi wa Mbagala Mzinga Wamefunga barabara ya kutoka Dar kwenda Mikoa ya kusini kwa madai ya kuchoshwa na ajali kwenye eneo lao, jambo hilo limesababisha foleni kubwa ya Magari.

Jambo hilo limemtoa Mkuu wa Mkoa wa DSM ofisini na kumfikisha eneo la Tukio ili kuwaomba wananchi hao waruhusu barabara iendelee kutumika .

Hata hivyo Bwana Chalamila amepokelewa na wimbo mpya uliotungwa eneo la tukio unaoitwa "bao 1 milioni 10 lakini barabara mbovu" ambao haufahamiki maana yake

Screenshot_2024-05-17-10-54-12-1.png
=======
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewasili eneo la Mbagala Mzinga baada ya wananchi kufunga Barabara ya Kilwa inayounganisha Jiji la Dar es Salaam na mikoa ya kusini, kwa madai ya kuchoshwa na ajali zinazotokea kila siku.

Chalamila amewasili eneo hilo asubuhi ya leo Mei 17, 2024 na kupokelewa na wananchi hao wakiimba ...goli moja milioni 10 halafu barabara mbovu.

Wananchi hao wamefunga barabara hiyo kutokana na ajali iliyotokea usiku wa jana Alhamisi Mei 16,2024 na kusababisha vifo vya watu wanne.

Kutokana na kufungwa kwa barabara hiyo kuanzia asubuhi ya leo kumesababisha foleni kubwa ya vyombo vya moto na watumiaji wengine wa barabara hiyo.


 
Wakazi wa Mbagala Mzinga Wamefunga barabara ya kutoka Dar kwenda Mikoa ya kusini kwa madai ya kuchoshwa na ajali kwenye eneo lao, jambo hilo limesababisha foleni kubwa ya Magari.

Jambo hilo limemtoa Mkuu wa Mkoa wa DSM ofisini na kumfikisha eneo la Tukio ili kuwaomba wananchi hao waruhusu barabara iendelee kutumika .

Hata hivyo Bwana Chalamila amepokelewa na wimbo mpya uliotungwa eneo la tukio unaoitwa "bao 1 milioni 10 lakini barabara mbovu" ambao haufahamiki maana yake

View attachment 2992446
Huyu ndio raisi wa ajabu kuwahi kutokea
 
Soon Dar nzima itaamka.
Hatimaye nchi nzima itaamka maana kuna maeneo ya nchi hii hakuna barabara bali zimebakia njia. Pesa wanapewa wasanii, kulipia magoli, kuwalipa machawa, kusafirisha misiba ya watangazaji, kuwatibu wasanii wakati kundi kubwa la watanganyika linataabika kwa kuwa na huduma duni.
 
Waacheni waendelee na kumpamba "mama" yao maana siku hizi hadi wanasema kapunguza vifo vya wanaozaa, mara hata madaktari wakifanikisha upasuaji mgumu wanasifia eti "madaktari wa mama" waokoa mgonjwa na sifa zote.

Sasa wananchi watamuondoa huyo anayeshindwa kutengeneza barabara, kuboresha maisha, mishahara na pension bora, ajira za vijana nk kisha huyo anayepunguza vifo watambakiza ila adhibitishe kuwa ni yeye kweli
 
Back
Top Bottom