Mbali na kuikosoa serikali kuhusu Makato; lakini kiukweli Watanzania kwenye kulipa Kodi tuwagumu sana

Sababu kuu ni kutokana walipa Kodi directly ni wachache, hivyo lazima wachache waumie mno.

Ila Kama Kila mtu angelipa Kodi kulingana na Uchumi wake, Kodi ingepungua
Ukiishie kwenye kusema watanzania ni wagumu kulipa kodi tu unakuwa kama hiyo hiyo serikali iliyoishiwa na kubaki kubabaisha. Serikali yoyote makini itatafuta sababu ni kwa nini watu hawalitaki kulipa kodi na itafuata njia za kitaalam kuwashawishi na kukusanya kodi. Serikali yetu imekuwa ''inatawala'' na siyo ''kuongoza''. Top-bottom approch ya uongozi siku zote haifanikiwi. Nenda kwa wenye maduka fanya utafiti. Kodi haziendani na hali halisi na utozaji wake unategemea mtuzaji amemkaje kama kipindi cha Magufuli maamuzi mengi ya nchi yalivyotegemea ameamkaje. Jingine: Hata kile kidogo kinachokusanywa kinaishia kutumbuliwa juu kwa juu kuanzia kwa wakusanyaji mpaka ngazi za juu. Uliwahi kujiuliza ni kwa nini viongozi wetu hawawezi kusafiri kwenye madaraja ya kawaida kwa mfano kwenye ndege? uliwahi kuona picha ya spika Ndugai ili-trend kipindi cha nyuma akiwa kwenye first class kwenye ndege akitokea Paris? Unajiuliza kwa nini wilaya moja iwe na viongozi luluki wasio na kazi yoyote zaidi ya kupiga soga tu? Unajiuliza magari ya gharama wanayotembelea nani ananunua na kwa nini wasinunue magari ya kawaida au hata pikipiki? Tanzania ukifanikiwa kuziba matumizi mabaya ya fedha kuanzia kwa rais mwenyewe mpaka wilayani tutapiga hatua kubwa sana.
 
Amna kuna maduka mengine hayahitaji kupunguzianana mfano maduka ya dawa/ famasi


Sasa huku vichochoroni hayo MADUKA ndio yamejaa

Alafu faida ya dawa unaweza pata mara kumi yake.

Wengi hawalipi Kodi.

Madawa yasiyoruhusiwa kuuzwa Kama yakutoa mimba ndio usiseme, bei zake sio haba.

Mengine sio yakusema
 
Hiyo hiyo kodi kidogo inatumika ipasavyo? Kama sio, una uhakika gani ikiwa nyingi itatumika ipasavyo na kukuletea maendeleo?
 
๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ

Bei moja utapewa na Risiti
Bei nyingine hupewi,

Chagua mwenyewe
Simpo, sasa hapo mtanzania risiti ya kazi gani. Nachagua pa bei rahisi....ninlazima tulazimishwe kulipa kodi kwa njia ambazo hasikwepeki kama hizi za miamala...
 


SERIKALI ya Tanzania inaongozwa na Watanzania wachache waliopata bahati ya kuwa Viongozi.

Imagine wewe unakimbia Kodi sasa hivi na sio kiongozi, Inategemea ukiwa kiongozi utatoa Kodi?
 
Hiyo hiyo kodi kidogo inatumika ipasavyo? Kama sio, una uhakika gani ikiwa nyingi itatumika ipasavyo na kukuletea maendeleo?

Uhakika upo Kwa sababu jamii ikiwa na uadilifu ya kulipa Kodi basi kuna uwezekano wa Kodi kutumika vizuri.

Lakini jamii ikiwa na hila na wakwepa Kodi wengi, hata Kodi ikitolewa haiwezi fanyia lolote
 
Sio kwamba watanzania ni wagumu kulipa Kodi hapana ugumu unakuja pale Kodi hizo zikitumiwa vibaya na viongozi kwa mfano leo hii haijulikan makao makuu ya nchi ni wapi dar au Dodoma rais na mawaziri wanapishana barabarani na angani Kama daladala (dar-dodoma),(dodoma-dar) gharama zote hizi zinakwenda kwa walala hoi ambao serikali imewapa jina la wanyonge.

Mtu anaye sisitiza ulipaji wa Kodi yeye halipi Kodi kuanzia rais,mawaziri , wabunge nk hivi unategemea nani atakuwa na moyo wa kulipa kwa hali hii mkuu?

Watu kuto wajibishwa Mara kadhaa ripoti ya CAG imekuwa ikiibua ufisadi na matumizi mabaya ya pesa za Umma mwisho mafisadi na wezi husimamishwa tu kazi au kubadilishwa kitengo mambo ya ukoo wa panya ndani ya CCM badala kupelekwa mahakamani kwa hali Nani atakuwa na moyo wa kulipa Kodi ambazo zinakwenda kwenye matumbo ya watu wachache.

Nani atakuwa na moyo wa kulipa Kodi ambazo zinakwenda kuwajengea watu nyumba za kifahari na kuwanunulia magari ya kifahari uku nchi ikiwa na matatizo kibao Kwenye maji,elimu,umeme,ajira nk.

Nani atakuwa na moyo wa kulipa Kodi ambazo zinakwenda kuhudumia mashirika yanayo jiendesha kwa hasara Kama ATCL.
 
Unalipa kodi halafu unasikia wabunge walopitisha ulipe kodi wao hawalipi, mara waziri wa fedha anayetuambia tulipe kodi tena kwa dharau yeye anakwepa kodi, hujakaa sawa unasikia wizara ya fedha wamejilipa mamilioni kipuuzi puuzi tu. Halafu mtu aniambie nidai risiti, nehiiii.
 
Mkuu nchi kama tanzania yenye kila aina ya madini kuanzia dhahabu, tanzinite, ruby, chuma, makaa ya mawe, chokaa, almasi, gas asilia bado hujaweka bahari, maziwa, bado bandari bado mbuga za wanyama na vivutio kedekede vya utalii hivi kweli serikali makini inahitaji kukamua wananchi ili kujenga uchumi na kupeleka barabara vijijini?
Hapa ni kwamba viongozi wameishiwa ubunifu na hawajui wafanye nini ili kuendeleza uchumi.
Kuna nchi zina aina moja tu ya madini lakini zimejenga nchi, vijana wanasma ellimu ya juu bure kabisa. Hii nchi ina tatizo siyo bure
 
Kulipa Kodi si tatizo, tatizo ni je zinatumikaje? mtu unalipa Kodi serikali inaenda nunua magari ya anasa kibao,hapo hapo zinatumika holela na wanajigawia miposho minono na mishahara mikubwa,
Mtu anabeba mamilion ya hela na halipi Kodi ,hali hiyo ndio inafanya watu wakwepe kulipa Kodi
 
Kama mpaka leo hujui makao makuu ya nchi ni wapi hapo tatizo ni lako. Marekani kuna new york na washington, nigeria kuna abuja na lagos, india kuna delhi na mumbay, sauzi kuna joeburg na pretoria tz kuna dom na dar...
 
Kama mpaka leo hujui makao makuu ya nchi ni wapi hapo tatizo ni lako. Marekani kuna new york na washington, nigeria kuna abuja na lagos, india kuna delhi na mumbay, sauzi kuna joeburg na pretoria tz kuna dom na dar...
Aliyekuambia makao makuu ya nchi ni dar ni Nani? Thibitisha ithibati yako sio blabla
 
Utapataje nguvu za kulipa kodi,wakat huduma za kijamii zko hovyo,shule za sekondar hazna walimu wa sayansi,hospital hazna madawa,mabarabara ya vijijin hayapitik.

Nasema TRA hamtaniona
 
Nchi itaendelea kwa fedha za kigeni kama hatuingiz pesa za kutosha za kigeni,tusitegemee kodi zitajenga nchi.
Kodi zitaishia kulipa mishahara tu
 
Wewe kwa kuwa unaishi kwa shemeji yako hujui ukubwa na wingi wa kodi tunazolipa.
 
Tanzania tunakosa nini hadi tuanze kukamuana hiki ambacho hata hakikidhi Mahitaji? Kuendesha Serikali inamaana Utalii,Madini,Gas na Mengineyo alotujaalia ALLAH haviwezi kugeuka hela kwa Serikali?Kama Serikalini ni Wavivu wa kufanya kazi na kuvigeuza hivyo kuwa hela ya kununua Mafuta ya V8 huku nani boya sasaa.
 
Hivi nikuulize, hapo Ruaha ulipo, kuna nyumba ngapi za kupangisha? Dar zipo ngapi? Hivi kwa nini mpaka sasa hakuna kodi ya wenye nyumba? Na ninaamini kama wangewekewa kodi, hakuna ambaye angelalamika. Ni kodi itatozwa kwenye mapato yao. Siyo hii ya miamala ambayo inatozwa kwenye huduma, siyo mapato.

Zipo kodi zinazoumiza. Na hii ya miamala ni mfano. Tayari kuna tozo, tunatozwa tozo juu ya tozo. Huku wanaacha fursa tele za kutoza kodi ambazo zisingeumiza watanzania. Hiyo ndiyo hoja. Kusema tu kwamba watanzania hawapendi kulipa kodi, hujawatendea haki. Hizo ni kauli za kibwanyenye.
 
Ni vyema ila wao wawe mfano pia, sio kupuyanga tu kisha wanataka sie ndio tulipishwe mikodi kandamizi๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Wao wagongwe spana pia maana wana maisha ya kifahari sana! Wao wakishalipa kodi itatupa moyo na sisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ