Mbaroni kwa kumsababishia kifo mtoto wake

Mbaroni kwa kumsababishia kifo mtoto wake

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Polisi mkoa Njombe wanamshikilia Israel Msigwa Almaarufu kama "Mtoa Roho"(39)makazi wa Makambako kwa kumsababishia kifo mtoto Haskad Msigwa (7) kwa kumuadhidu kwa nyaya za umeme na fimbo kwa sababu amekojoa kitandani.

RPC wa Njombe Hamis Issah amesema "Huyu amemuadhibu mtoto wake kwa kumuadhibu kwa nyaya za umeme pamoja na fimbo matokeo yake amemsababishia kifo mtoto wake halafu akakimbilia Kilosa Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

"Mzazi huyu alitoweka na alipotoweka tumemkamata jana eneo la Kilosa Mufindi Mjini Mafinga na sasa tunamshikilia lakini mtoto amepoteza maisha, tukikamilisha upelelezi sheria zitafuata mkondo wake. Amesema RPC Issah

1643978174765.png
 
Polisi mkoa Njombe wanamshikilia Israel Msigwa Almaarufu kama "Mtoa Roho"(39)makazi wa Makambako kwa kumsababishia kifo mtoto Haskad Msigwa (7) kwa kumuadhidu kwa nyaya za umeme na fimbo kwa sababu amekojoa kitandani.

RPC wa Njombe Hamis Issah amesema "Huyu amemuadhibu mtoto wake kwa kumuadhibu kwa nyaya za umeme pamoja na fimbo matokeo yake amemsababishia kifo mtoto wake halafu akakimbilia Kilosa Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

"Mzazi huyu alitoweka na alipotoweka tumemkamata jana eneo la Kilosa Mufindi Mjini Mafinga na sasa tunamshikilia lakini mtoto amepoteza maisha, tukikamilisha upelelezi sheria zitafuata mkondo wake. Amesema RPC Issah


Kichwa cha Habari cha kijinga, kamuua mwanaye Huyu mpumbavu, he is the murderer
 
Wazazi tuangalie namna tunavyowaadhibu watoto njia tunazotumia ni sahihi?
 
Duh!

Enzi tukiwa wadogo ushagoo huko, ukikojoa kitandani basi utatishiwa kufungiwa chura kwenye kiuno ili ang'ate kidudu kila unapokojoa...
 
baada ya kumsaidia mwanawe kupata dawa ya kuacha kukojoa wewe unapiga fimbo, Primitive society, hapa ndio naona ile maana ya kuacha kuadhibu kwa viboko...
 
Duh!

Enzi tukiwa wadogo ushagoo huko, ukikojoa kitandani basi utatishiwa kufungiwa chura kwenye kiuno ili ang'ate kidudu kila unapokojoa...
Umenikumbusha mbali, walikamataga lichura likubwaa wakalifungia, wakawa wananitishia nikikojoa wataniwekea Kwa Bibi, niliacha kukojoa😂
 
Tuangalie sana majina haya tunayopewa mmmmmh! Yanatisha na yanasadifu yaliyomo
 
Back
Top Bottom