Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,067
- 10,938
Watu wawili wanashikiliwa na jeshi la Polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za mauaji wa mwanafunzi wa shule ya msingi Mtumba, Farida Makuya (16) aliyeuawa usiku akiwa nyumbani kwao Oktoba 4, 2022.
Marehemu enzi za uhai wake
Binti alitakiwa kuwa miongoni kwa watahiniwa wa mitihani wa darasa la saba inayotamatika leo nchi nzima. Inadaiwa alipigwa na kitu kizito kichwani wakati wa tukio hilo la mauaji.
Huzuni ilitawala wakati wa maziko yake hapo jana.
” Tukio la kifo chake ni baya kuelezeka,” amesema Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma Martin Otieno.
“Kwa sasa tumewakamata watu wawili kwa mahojiano na ikithibitika watafikishwa mahakamani,” amesema.
Inasemekana binti huyo alishambuliwa wakati mama yake alipoondoka nyumbani kwenda kuuza pombe za kienyeji na aliporudi akiwa amelewa alikutana na michirizi ya damu kuanzia mlangoni baada ya kuwasha tochi ya simu yake.
Baada ya shambulio hilo, binti huyo alipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu kabla ya kufikwa na umauti.
----
Marehemu enzi za uhai wake
Binti alitakiwa kuwa miongoni kwa watahiniwa wa mitihani wa darasa la saba inayotamatika leo nchi nzima. Inadaiwa alipigwa na kitu kizito kichwani wakati wa tukio hilo la mauaji.
Huzuni ilitawala wakati wa maziko yake hapo jana.
” Tukio la kifo chake ni baya kuelezeka,” amesema Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma Martin Otieno.
“Kwa sasa tumewakamata watu wawili kwa mahojiano na ikithibitika watafikishwa mahakamani,” amesema.
Inasemekana binti huyo alishambuliwa wakati mama yake alipoondoka nyumbani kwenda kuuza pombe za kienyeji na aliporudi akiwa amelewa alikutana na michirizi ya damu kuanzia mlangoni baada ya kuwasha tochi ya simu yake.
Baada ya shambulio hilo, binti huyo alipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu kabla ya kufikwa na umauti.
----
Ni Jumatatu Tarehe 3/10/2022 Farida anajiandaa na kwenda zake Shule akiwa ni Binti wa Darasa la Saba.
Farida anaenda Shule huku akiwa amejiandaa vyema kwa Mtihani wake wa Kumaliza Elimu ya Msingi.
Farida ana wadogo zake wawili ambao wanamuona Dada yao kama mfano kwao.
Alasiri Farida anarudi Nyumbani, anakutana na wadogo zake na Mama yake.
Jioni Mama Farida anaondoka kwenda kwenye Mihangaiko na kuwaacha Watoto wake Nyumbani huku akiamini atawakuta salama salimini.
Lahaula.... Majira ya Giza linapoanza kumea Wahuni wanaingia Ndani kwa Mama Farida, Wanawakuta watoto wake Watatu (Farida na Wadogo zake 2) huku Mama akiwa kaenda kuwatafutia Mkate wanawe.
Wahuni wanamkamata Farida, WANAMBAKA na baada ya hapo wanamuangushia kipigo, wanamtoa nje wanamuacha huku Damu zikiwa zinavuja.
Masikini... wadogo zake Farida, wanashuhudia unyama anaofanyiwa Dada yao lakini hawana cha Kufanya.
Mama anarudi kutoka kwenye kutafuta Mkate wa watoto wake, anakutana na Watoto wake wawili wakiwa katika hofu kubwa na Damu ikiwa imemwagika Nyumbani kwake.
Mama anauliza Dada yenu yupo wapi watoto kwa hofu wanamuangalia Mama Yao huku Machozi yakiwatoka anafuatilia Damu anakutana na Binti yake akiwa anahema kwa mba...li Sana.
Kilio kinamtoka, Majirani wanakuja na kumsaidia kumpeleka Farida hospitali.
Njiani Farida anakata Roho na Mauti yanamfika.
FARIDA MAKUYA
Ni nani?
Ni Binti aliyekuwa akisoma Darasa la Saba (2022) na alitarajiwa Kufanya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi Tarehe 5-6/10/2022.
Anaishi wapi?
Mtumba
Anasoma wapi?
Mtumba Shule ya Msingi.
Mkoa Gani?
Dodoma
Ninashindwa kuendelea kuandika, Roho inauma Sana. Unyama aliotendewa unaumiza Sana.
Pumzika kwa Amani FARIDA MAKUYA.