Mbeya: Basi la Kampuni ya Shari lapata ajali Mbarali, Watu 9 wapoteza maisha, Polisi wamshikilia Dereva

Mbeya: Basi la Kampuni ya Shari lapata ajali Mbarali, Watu 9 wapoteza maisha, Polisi wamshikilia Dereva

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687

My Take
Kila siku hapa Tanzania Kuna ajari inatokea inayoua watu na chanzo mara zote ni uzembe wa madereva.

Swali,Je Serikali mumeshibdwa kuja na Sheria Kali za kuwadhibiti Hawa Madereva wanasababisha ajali Kwa uzembe?
---
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Dereva Alfredy Baharia maarufu kama Mwidunda (50) mkazi wa Ubaruku wilayani Mbarali aliyekuwa akiendesha Gari namba T.896 DHK aina ya Yutong basi la abiria mali ya kampuni ya Shari line lililokuwa likitokea Sumbawanga kuelekea Ubaruku Wilaya ya Mbarali.

Ni kwamba tarehe 03.09.2024 majira ya saa 1:10 jioni huko Kijiji cha Itamboleo, Kata na Tarafa ya Chimala, Wilaya ya Mbarali katika barabara kuu ya Mbeya - Njombe, Gari iliyokuwa ikiendeshwa na Mwidunda, mkazi wa ubaruku iliacha njia kisha kugonga gema, kuanguka na kusababisha vifo kwa watu tisa (09) kati yao wanaume 06 kati yao watoto 02, wanawake 03 ambao wote kwa sasa bado kutambulika.

Aidha, katika tukio hilo watu 18 walijeruhiwa kati yao wanaume 05, wanawake 13 na watoto 02 wa kiume na wa kike. chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa basi hilo kushindwa kulimudu gari hilo kwenye kona kali na kupelekea kuacha barabara, kutumbukia korongoni na kugonga gema. Dereva wa Basi hilo anaendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Misheni Chimala akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.

Miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya misheni Chimala na majeruhi wanapatiwa matibabu Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya na wengine Hospitali ya Misheni Chimala.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kwa madereva kuwa makini na kuzingatia sheria, alama na michoro ya usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

Imetolewa na:
Benjamin E. Kuzaga – SACP
Kamanda wa Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
Soma Pia: Polisi Mbeya wamshikilia Dereva wa Lori kwa kusababisha ajali


R.I.P ndugu 😭😭😭😭
 
WhatsApp Image 2024-09-04 at 16.35.46_bf6d976d.jpg

WhatsApp Image 2024-09-04 at 16.35.43_004937c1.jpg
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Dereva Alfredy Baharia maarufu kama Mwidunda (50) mkazi wa Ubaruku wilayani Mbarali aliyekuwa akiendesha Gari namba T.896 DHK aina ya Yutong basi la abiria mali ya kampuni ya Shari line lililokuwa likitokea Sumbawanga kuelekea Ubaruku Wilaya ya Mbarali.

Ni kwamba tarehe 03.09.2024 majira ya saa 1:10 jioni huko Kijiji cha Itamboleo, Kata na Tarafa ya Chimala, Wilaya ya Mbarali katika barabara kuu ya Mbeya - Njombe, Gari iliyokuwa ikiendeshwa na Mwidunda, mkazi wa ubaruku iliacha njia kisha kugonga gema, kuanguka na kusababisha vifo kwa watu tisa (09) kati yao wanaume 06 kati yao watoto 02, wanawake 03 ambao wote kwa sasa bado kutambulika.

Aidha, katika tukio hilo watu 18 walijeruhiwa kati yao wanaume 05, wanawake 13 na watoto 02 wa kiume na wa kike. chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa basi hilo kushindwa kulimudu gari hilo kwenye kona kali na kupelekea kuacha barabara, kutumbukia korongoni na kugonga gema. Dereva wa Basi hilo anaendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Misheni Chimala akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.

WhatsApp Image 2024-09-04 at 16.35.43_0af053a0.jpg

WhatsApp Image 2024-09-04 at 16.35.42_2196c8f4.jpg
Miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya misheni Chimala na majeruhi wanapatiwa matibabu Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya na wengine Hospitali ya Misheni Chimala.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kwa madereva kuwa makini na kuzingatia sheria, alama na michoro ya usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

Imetolewa na:
Benjamin E. Kuzaga – SACP
Kamanda wa Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Soma Pia: Polisi Mbeya wamshikilia Dereva wa Lori kwa kusababisha ajali
 
Miundombinu ni mibovu Tanzania na vyombo vingi vya Moto hasa mabus na malori ni majeneza yanayotembea.
Tanzania kila dereva anataka ligi na mwenzake kuanzia madereva wa magari makubwa Hadi madogo
Wapi waliposema miundombinu imesababisha ajali?
 
Ajali za barabarani ni tatizo kubwa linalohitaji umakini wa haraka, hasa katika maeneo kama Basi la Shari Line, ambapo ajali tisa zimeripotiwa katika kipindi kifupi.

Katika mkoa wa Mbeya, hususan Mbarali, hali hii inatia hofu kubwa kwa wasafiri na jamii kwa ujumla.

Serikali ina jukumu la msingi la kuhakikisha usalama wa raia wake, na ajali hizi zinaonyesha kasoro katika udhibiti wa usafiri wa barabarani.

Mpango wa serikali unapaswa kujumuisha hatua mbalimbali, kama vile kuimarisha ukaguzi wa magari, kutoa mafunzo kwa madereva, na kuanzisha kampeni za uhamasishaji kuhusu usalama barabarani.

Aidha, kuweka alama za barabarani na mfumo wa kamera za ufuatiliaji kwenye maeneo hatarishi kunaweza kusaidia kupunguza ajali.

Hata hivyo, ni wazi kwamba juhudi hizi hazitoshi kama hazitafanyika kwa ukamilifu na kwa wakati.

Kukaa kimya kwa serikali kunaweza kutafsiriwa kama kutokuwepo kwa uongozi thabiti katika kushughulikia matatizo haya.

Wakati mwingine, upungufu wa rasilimali na miundombinu duni vinaweza kuwa sababu za kutofanya mabadiliko yanayohitajika.

Vilevile, kuna uwezekano wa kupuuzilia mbali ripoti za ajali na kuacha kupiga hatua stahiki.

Ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua za haraka ili kuhakikisha usalama wa abiria na kuzuia ajali zaidi.

Hii inahitaji si tu sera bora, bali pia utekelezaji wa sheria na kanuni zinazohusiana na usafiri wa barabarani.

Juhudi hizi zinapohitajika, lazima zitolewe kipaumbele ili kuokoa maisha na kupunguza majeruhi.
 
Back
Top Bottom