KERO Mbeya: Kabwe hapafai kuwa Soko Jioni, ni pachafu kupindukia, tunakaribisha Kipindupindu

KERO Mbeya: Kabwe hapafai kuwa Soko Jioni, ni pachafu kupindukia, tunakaribisha Kipindupindu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
Hivi ni nani alitoa wazo la kupafanya Stendi ya Daladala ya Kabwe kila ikifika jioni kupageuza Soko?

Moja hili eneo ni chafu kupita maelezo na Wafanyabiashara wamejianzishia Dampo hapohapo.

Yaani huku taka zimejaa lakini pembeni yake unaona mama anaendelea na kuuza Samaki, Matunda, Mboga Mboga n.k.

Maafisa wa Afya wale 'Mabwana Afya' mmetulia kimya kana kwamba hamuoni kinachoendelea maeneo hayo au mpaka Watu waugue kipindupindu ndiyo mtapazuia.

Ukiachana na uchafu pia ikifika jioni Daladala zinapata shida sababu stendi inakuwa imebanwa na Wafanyabiashara, hivyo kusababisha kero isiyokuwa na msingi.

Nao vibaka hawako nyuma kila ikifika jioni wanaingia kazini ukizubaa tu imekula kwako.

DSC_0377.JPG
DSC_0373.JPG
DSC_0376.JPG
 
Masoko mengi Tanzania ni machafu, wanachojua ni kukusanya ushuru tu.
Mara ya mwisho nilikwenda soko la Ilala mwaka jana, nimeapa sikanyangi tena. Soko hata choo kina afadhali.
 
HILO SIYO SOKO WALA SIYO STENDI,hata sisi serikali hatujui wananchi wametoa wapi kibali cha kuanzisha soko hilo!!wiki zijazo ntamwaga migambo hapo wakafanye kazi yao.

By the way tunasubiri upanuzi wa barabara njia nne uje uliue hili soko NATURAL DEATH.
 
Mleta mada umeutendea haki uzi huu kwa kuambatanisha ushahidi. Wahusika walifanyie kazi hili. Maana kuwanyima furusa Maafisa usafirishaji wa hiyo Stendi ya Kabwe mida hiyo ya Jioni si haki!!!
 
Hivi ni nani alitoa wazo la kupafanya Stendi ya Daladala ya Kabwe kila ikifika jioni kupageuza Soko?

Moja hili eneo ni chafu kupita maelezo na Wafanyabiashara wamejianzishia Dampo hapohapo.

Yaani huku taka zimejaa lakini pembeni yake unaona mama anaendelea na kuuza Samaki, Matunda, Mboga Mboga n.k.

Maafisa wa Afya wale 'Mabwana Afya' mmetulia kimya kana kwamba hamuoni kinachoendelea maeneo hayo au mpaka Watu waugue kipindupindu ndiyo mtapazuia.

Ukiachana na uchafu pia ikifika jioni Daladala zinapata shida sababu stendi inakuwa imebanwa na Wafanyabiashara, hivyo kusababisha kero isiyokuwa na msingi.

Nao vibaka hawako nyuma kila ikifika jioni wanaingia kazini ukizubaa tu imekula kwako.

Mchana na asubuhi ni pasafi sana ila ikifika jioni kunageuka na kuwa soko na palipo soko hapakosi uchafu
 
Hivi ni nani alitoa wazo la kupafanya Stendi ya Daladala ya Kabwe kila ikifika jioni kupageuza Soko?

Moja hili eneo ni chafu kupita maelezo na Wafanyabiashara wamejianzishia Dampo hapohapo.

Yaani huku taka zimejaa lakini pembeni yake unaona mama anaendelea na kuuza Samaki, Matunda, Mboga Mboga n.k.

Maafisa wa Afya wale 'Mabwana Afya' mmetulia kimya kana kwamba hamuoni kinachoendelea maeneo hayo au mpaka Watu waugue kipindupindu ndiyo mtapazuia.

Ukiachana na uchafu pia ikifika jioni Daladala zinapata shida sababu stendi inakuwa imebanwa na Wafanyabiashara, hivyo kusababisha kero isiyokuwa na msingi.

Nao vibaka hawako nyuma kila ikifika jioni wanaingia kazini ukizubaa tu imekula kwako.

On the same token hapo vinauzwa vyakula OG original. Hata embe likidondokea topeni ww osha kula hudhuriki
 
Back
Top Bottom