Mbeya kutamu bwana, usisikie habari za mtandaoni

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Mbeya ni mkoa mzuri sana kijografia, ukiwa umezungukwa na milima na vilima. Mito na vijito, hali nzuri ya hewa, udongo mzuri wenye rutuba na mambo mengi mazuri.

Watu wa Mbeya ni wakarimu sana, watoaji na wenye upendo, ila ukiwazingua wanakuzingua mara milioni sita zaidi.

Mbeya kuna mandhari ya kuvutia. Kuna vivutio kibao vya utalii, kama kona ya taifa, hii ni bonge ya kona, iko kwenye barabara ya lami itokayo Cape Town Afrika ya Kusini kwenda Cairo Misri kupitia Chunya kwa Masache Kasaka a.k.a Man Kasa mbunge wa Lupa Chunya.

Hii ni picha ya kona ya Taifa, iliyopigwa na Fadhy, Fadhili Mtanga, mpishi anaye andika na kupiga picha.



Kivutio kingine ni ziwa Masoko.

Hili ni ziwa lililoko mlimani, crater lake. Ziwa hili limekaa mithili ya lulu ipatikanayo kwenye samaki aina ya chaza (Oysters). Lulu hiyo kwa Kinyakyusa huitwa pearl.

Mbeya imejaaliwa bwana, pia juna ziwa Kisiba, ziwa la msituni. Ziwa hili liko kwenye msitu asilia, ile misitu inayojulikana kwa jina la rain forest. Hutojuta kabisa kufika mahali hapa.

Kwa wanaopenda kuoanda milima, Mbeya ni mahali sahihi kabisa kwa burudani hiyo. Kuna mlima Loleza, huu ni mlima mzuri sana na rahisi kupanda na wala hauko mbali na mji.

Shule ya sekondari ya wasichana ya Loleza ilipewa jina hili kwababu iko chini ya Mlima Loleza.
Picha hii ilipigwa na Fadhy, Fadhili Mtanga ikionyesha mlima Loleza unavyoonekana ukiwa Mwanjelwa, pale mahali ambapo soko liliungua. Nimepamiss sana home.


Mlima Rungwe, mlima huu una urefu wa meta 2,981. Mlima huu uko wilayani Rungwe. Unakaribishwa sana kutembelea mkoa huu, wenye neema nyingi za kutosha.

Picha mbili zikionesha mandhari tofauti za mlima Rungwe.




Mashamba ya Chai Katumba

Haya ni mashamba yaliyopo Katumba, Tukuyu. Mashamba haya yana muonekano mzuri sana, na jali ya hewa ni nzuri sana. Hakika ukifika Katumba, utabakiwa na kumbukumbu isiyofutika kamwe
 

Attachments

  • images (19).jpeg
    32.1 KB · Views: 22
Siasa zilianza kuiathiri Mbeya tangu enzi za Nyerere. Nyerere hakuipenda kabisa Mbeya.
Hata uwanja wa Sokoine ulitakiwa ujengwe na Wachina, Nyerere akakataa, akaamuru ujengwe na wafungwa. Ukaitwa jina uwanja wa Mapinduzi.

Serikali ilikuwa haijihangaishi na kupanga mji kwa mpangilio. Uzunguni, Uhindini, Soko Matola, 🇬🇭 Ghana, Majengo na Mbata ilipangwa na wazungu na sio CCM.

Serikali ya CCM ilipanga mitaa ya Soweto a.k.a Block Q, Ilimba, Sae, na Block T.
Zaidi ya hapo hamna ilichokifanya, labda ianze kuupanga na kuupima mji kisasa hivi leo
Tatizo la Mbeya ni ujenzi wa nyumba za ajabu ajabu na holela...
 
Picha ya kwanza dereva akiwa na wenge anapitiliza na harudi tena barabarani. Ukijani wake umenivutia sana.Mbeya kuzuri. Tanzania yetu ni nzuri sana ila inaharibiwa na watu wachache.
 
Hivi Nyerere alikuwa ana nini na watu wanaokula ndizi? Mbona karibu kila sehemu za hao wenyeji kuna kitu aliwatenga?
 

Yale matumizi ya tofali za udongo, imeufanya mji uonekane kijiji kilichochangamka...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…