Mbeya: Msanii wa Nyimbo za Injili, Sifa Bujune ashikiliwa kwa tuhuma za kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi

Mbeya: Msanii wa Nyimbo za Injili, Sifa Bujune ashikiliwa kwa tuhuma za kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi

wAAYu9E.jpg
 
Keyboard warrior washapaniki [emoji23][emoji23]endeleeni kufanya maigizo shida mtayopata sisi tutaijadili hapa jf na kukupa like za uzalendo mengine utajua wewe na familia yako [emoji23]
Hahaaaaa, naona umewapa za uso Keyboard warriors.
 
Wewe Shangazi i love you
 
CHAWA MKUBWA WEWE! Eti mlikumbushia kwa spika! Spika mwenyewe ni wale wale wahujumu wa uchumi, haki na maendeleo ya nchi hii!
😀😀😀😃😃. Heti mwenyewe ndio kaona kaongea point, nimemkumbushia spika. Unamkumbusha alieziba masikio kwa maneno.
 

Mwimbaji huyo Sifa Boniventure Bujune (25) ni Mkazi wa Isyesye anatuhumiwa kuimba wimbo unaojulikana kwa jina la “Tanzania Inaelekea Wapi?” wenye maudhui ya uchochezi na kisha kuurusha katika Mitandao ya Kijamii pamoja na YouTube.

Kamanda wa Polisi Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema Mtuhumiwa alikamatwa Septemba 13, 2023 huko Isyesye Jijini Mbeya baada ya kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuusambaza kupitia mitandao ya kijamii pamoja na mtandao wa kurusha maudhui wa YouTube.

Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa kwa hatua zaidi za kisheria.
View attachment 2750998
Huu ndo wimbo anatuhumiwa nao

Pia, soma:
- Mbeya: Mwimbaji wa Wimbo wa "Mnatuona Nyani" afikishwa Mahakamani, asomewa mashtaka
Vijana wanaimba, "...mnatuona nyani." Wanakamatwa na kuswekwa lupango.

Wanaokamata vijana- hata wale wanaowatuma wawakamate - hawawaambii wao wanawaonaje.

Waliohuru wanasema wanavyoona; hata wanavyoonwa na wengine. Wasiotaka kuonwa kama wanavyoonekana; au kusemwa kama walivyo, ndio maadui wa uhuru.

Kumbuka maadui wa uhuru hawako huru. Kama wehu, hujipora hata uhuru wao wenyewe; na hatimaye kuwa watumwa wastahilio ukombozi
 
Hao ni vijana wa Mbarikiwa Mwakipesile na huwa tunamshauri sana aache kushindana na dola na kama anainba kuisema serikali aimbe na kusema yeye kama yeye na asihusishe kanisa na Ukristo kwenye mambo yake. Yule ana shida kidogo kwa. Suala lake binafsi liniiuma sana kwani nilikuwa nampenda na kupenda zile tenzi wanazoimba.

Sasa amejiingiza kushambulia serikali bila sababu akisema wamemuulia mwanaye tena Mkurugenzi wa usalama wa Taifa ndio kafanya hivyo. Jamaa hashauriki, vijana wake hao waliokamatwa hawashauriki wao wanatokana na kujiona wajuaji kama genta alivyo. Kiburi, kutojinyenyekesha, ujuaji mara nyingi huenda kwenye anguko.

Sasa kumezuka wimbi kubwa la watumishi wanaosimama na kuoneshana umwamba na serikali. Hakuna duniani mtumishi wa Mungu aliwahi ishinde dola nasi wajibu wetu ni kushauri na kuiombea mamlaka na siyo kushindana nayo.

Mimi ni kiongozi wa Kanisa na ni miongoni mwa wajumbe CPCT Taifa, kama wapentecoste tulishauri na kutoa maoni yetu kwa Mamlaka kuhusu Bandari kwani nasi tunaaminiwa na watu hatuwezi mshutumu mfalme mbele za watu.


Tulikumbushia kwa Spika wakati wa mkutano wetu mkuu pale CBC Miuji Dodoma kuhusu maoni yetu na msimamo wetu ki sio kushindana wala kupinga hadharani.
Wewe ni mjinga na kibaraka! Mtumishi wa kweli atatetea haki!
 

Mwimbaji huyo Sifa Boniventure Bujune (25) ni Mkazi wa Isyesye anatuhumiwa kuimba wimbo unaojulikana kwa jina la “Tanzania Inaelekea Wapi?” wenye maudhui ya uchochezi na kisha kuurusha katika Mitandao ya Kijamii pamoja na YouTube.

Kamanda wa Polisi Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema Mtuhumiwa alikamatwa Septemba 13, 2023 huko Isyesye Jijini Mbeya baada ya kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuusambaza kupitia mitandao ya kijamii pamoja na mtandao wa kurusha maudhui wa YouTube.

Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa kwa hatua zaidi za kisheria.
View attachment 2750998
Huu ndo wimbo anatuhumiwa nao

Pia, soma:
- Mbeya: Mwimbaji wa Wimbo wa "Mnatuona Nyani" afikishwa Mahakamani, asomewa mashtaka
Huu wimbo hauna tatizo lolote. Wameuzuia kwa kuwa wanatuona NYANI tu!
 
Vijana wanaimba, "...mnatuona nyani." Wanakamatwa na kuswekwa lupango.

Wanaokamata vijana- hata wale wanaowatuma wawakamate - hawawaambii wao wanawaonaje.

Waliohuru wanasema wanavyoona; hata wanavyoonwa na wengine. Wasiotaka kuonwa kama wanavyoonekana; au kusemwa kama walivyo, ndio maadui wa uhuru.

Kumbuka maadui wa uhuru hawako huru. Kama wehu, hujipora hata uhuru wao wenyewe; na hatimaye kuwa watumwa wastahilio ukombozi
Wanatuona nyani tu!
 
Back
Top Bottom