Mbeya: Watu wawili washikiliwa kwa kukutwa na bunduki aina ya Shotgun Pump Action bila kibali

Mbeya: Watu wawili washikiliwa kwa kukutwa na bunduki aina ya Shotgun Pump Action bila kibali

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-05-15 at 13.49.31_8d46a0a7.jpg
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili Nerbat Bwiga (33) mkazi wa Ifumbo na Isaya Zumba (38) mkazi wa Airport Songwe kwa tuhuma ya kupatikana na silaha bunduki moja aina ya Shotgun Pump Action bila kibali.

Akizungumza na waandishi wa habari Mei 15, 2024 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga amesema kuwa, awali mnamo Aprili 29, 2023 majira ya usiku huko maeneo ya Nzovwe Jijini Mbeya, watuhumiwa walivunja Jengo la Black Microfinance Bank na kuiba silaha hiyo.

Kamanda Kuzaga ameongeza kuwa, kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi kupitia kikosi maalum cha kuzuia na kupambana na uhalifu lilifanya ufuatiliaji na mnamo Mei 11, 2024 huko Kijiji cha Itete kilichopo Kata ya Isuto mkoani Mbeya lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa Nerbat Bwiga akiwa na silaha hiyo.

Aidha, Kamanda Kuzaga amesema kuwa mtuhumiwa amekiri kufanya matukio mbalimbali ya uhalifu kwa kushirikiana na mwenzake Isaya Zumba.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa jamii kutafuta kazi halali ya kufanya na kuachana na uhalifu kwani hauna nafasi. Pia linatoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
 
Ujambazi siku hizi mgumu sana. Watu hawatembei na keshi wala hawaweki ndani.
Ukitaka cash ya kijambazi nenda bank kabisa. Ukitaka cashflow jiunge na mtandao wa madawa ya kulevya

Ukitaka uzima wa milele dunduliza hela za kuuza kilo za mchele rejareja
 
Kwa kuwa wamekiri kuhudika na matukio, mgeshimiwa rpc andaa press nyingine kututaarifu kuwa mlipokuwa mnampeleka mahakanani chini ya ulinzi mkali mtuhumiwa Nerbat alijaribu kuruka kwenye karandinga bahati mbaya akaangukia kichwa na utoe wito tena wahalifu hawana nafasi.


Maoni yangu: uchunguzi ukikamilika Kwa majambazi na wakatia ramanu yote chapu wawahishwe Kwa almighty God
 
Ukitaka cash ya kijambazi nenda bank kabisa. Ukitaka cashflow jiunge na mtandao wa madawa ya kulevya

Ukitaka uzima wa milele dunduliza hela za kuuza kilo za mchele rejareja
Ambao tuko kwenye field ndiyo tunakuambia, kazi ni ngumu siku hizi
 
Ndio nimeijua leo hiyo bunduki naonaga kwa walinzi tu
 
Kwa kuwa wamekiri kuhudika na matukio, mgeshimiwa rpc andaa press nyingine kututaarifu kuwa mlipokuwa mnampeleka mahakanani chini ya ulinzi mkali mtuhumiwa Nerbat alijaribu kuruka kwenye karandinga bahati mbaya akaangukia kichwa na utoe wito tena wahalifu hawana nafasi.


Maoni yangu: uchunguzi ukikamilika Kwa majambazi na wakatia ramanu yote chapu wawahishwe Kwa almighty God
Ni jambazi sugu, kwa Nini anaruka na kichwa
 
Back
Top Bottom