Mbinu mpya wanayotumia matapeli wanaotuma meseji

Mbinu mpya wanayotumia matapeli wanaotuma meseji

mimi alinitumia ela 50000 halafu hapohapo akanipigia kwamba amekosea hivyo ananitumia namba ya dogo aliye skuli nimrushie...
nikampotezea maana janja ya nyani kwishajua!!
hadi mwisho ikaomba msamaha kwamba nirudishe haitarudia tena...
hapo mimi iko kwa mama muuza piga moja moto moja baridiiiii..
iko fikiri kila mtu ni MAKU MAK

Leo nikiwa naelekea City Centre hapa Jijini Mwanza tukiwa daldalani ilipofika maeneo ya Kona ya Nyegezi kaingia bibi mmoja analia anadai katapeliwa laki nne na nusu kwenye simu na mtu aliyejitambulisha kama Padre wa Kanisa Katoliki Parokia ya Butimba.
Konda hakumdai nauli na dereva kamshusha Kanisani hapo ili "akapambane" na aliyemtapeli.
Mh, isijekuwa huyo bibi ni tapeli nae na hapo aliapply mbinu yake namba 2 kati ya 200 alizonazo za kusafiri bure!!!!! Mungu anisamehe kwa kufikiria hv, ni matapeli hawa waliotufikisha katika hali hii.
 
ni cheusi chekundu alitaka kucheza,
nilikuwa na pesa kwenye simu laki420 alivyotuma hiyo elf50 ikawa 470..!

wakati ananipigia kunipush nimtumie katika ile namba ya dogo wake alieko shule huku nyuma alikuwa anataka awahi kunipiga pini,nikishatuma kwenye ile namba ya dogo palepale anapiga huduma ya wateja kisha wana reverse kwake ile hamsini!!
kumbuka hapo nilishatuma 50 yake kwa dogo ambaye ni yee
Dah! Kweli kua uyaone- siyo maghorofa... mkuu asante kwa kunitoa tongotongo katika hili nimekuelewa vilivyo kwamba anatuma hamsini ila kwenye kurudi irudi na (hamsini) mwenzake, kwahiyo ukaenda zako kutoa laki nne yako yote au ukakausha areverse kahela kake?
 
Back
Top Bottom