Mbinu za kuwa msiri

Mbinu za kuwa msiri

Sio kucontrol tuu pia wanapenda kuonana mtu Hana kitu anateseka
Wapuuze watu wa hivyo hata ukifanikiwa hawatopenda, kuna aina ya watu wanapenda waone unateseka ili wapate cha kukusimangia.

Maisha yawe magumu sana au yawe mazuri sana ni yako mkuu, epuka sana kuwashirikisha watu mipango yako, wengi sio wema.
 
Habari zenu Wana jukwaa
Kama kichwa Cha Uzi kinavyosema naombeni mnisaidie mbinu za kua msiri
Baadae ya kua mtu mzima Kuna namna ninawaona ndugu na watu wa karibu kama watu wenye choyo na wengi hawapendi mtu afanikiwe iwe ni ndoa kazi au biashara
Sasa ninaomba mnipe mbinu gani nitumie ili maisha yangu yawe ya Siri nimeshahangaika sana Kuna vitu nisipowashirikisha Ina kua ni ugomvi hivyo inanilazimu niwaeleze mipango yangu yote hiki kitu sikipendi na hata nikiwama hawana msaada wowote ule
Nifanyaje wasijue maisha yangu na ukizingatia ni watu wangu wa karibu
Natanguliza shukran
Maisha yako ni yako,kaa kimya katika mipango yako na waone yametimia tu,hakuna lawama yenye madhara katika hilo hata waongee vipi
 
Sasa ni watu ninaoishi nao hata nikipata dili la kazi wanataka nijue ni wapi nafanyia hiyo kazi mpaka mshahara Mimi sipendi na siku nisipokua na ishu wanakaa mbali na Mimi hata mia yao siioni
Dah😭
Wanakuona bado ni mali au investment yao. Inawezekana wasikupe pesa ila huwa unakula na kujiweka sawa kupitia pesa zao hivyo, wanaona wana haki ya kujua kila kitu kinachoendelea kwenye maisha yako.

Second assumption, pengine ni mtoto wa mwisho mwisho hivyo wanakuona bado mtoto ndio maana wanakuwa overprotrotective. So, usiri wako utaanzia kwenye kujiondoa kwenye utegemezi wa aina yoyote na kujionesha kama mtu mzima. Pia fuatilia mishe nyingi nyingi ila ile kubwa usiwaambie hadi itiki na ikishatiki uondoke
 
Wanakuona bado ni mali au investment yao. Inawezekana wasikupe pesa ila huwa unakula na kujiweka sawa kupitia pesa zao hivyo, wanaona wana haki ya kujua kila kitu kinachoendelea kwenye maisha yako.

Second assumption, pengine ni mtoto wa mwisho mwisho hivyo wanakuona bado mtoto ndio maana wanakuwa overprotrotective. So, usiri wako utaanzia kwenye kujiondoa kwenye utegemezi wa aina yoyote na kujionesha kama mtu mzima. Pia fuatilia mishe nyingi nyingi ila ile kubwa usiwaambie hadi itiki na ikishatiki uondoke
Asante sana mkuu Kuna mishe niliipata mkoani nilishindwa kwenda mjomba anataka niende nae akapaone 😄😄 nikaacha kwenda nikaona ni uswahili
 
Pia hautofanikiwa kimaisha usipoamua na wewe kuwa sehemu ya kusaidia wengine wengine

Ukiona hauleti chakula jua wewe ndo hicho chakula

Sipiritual usipojiweka mkao wa kuwa msaada jua utabaki kuwa mtu wa kawaida Sana at your age unabidi kujitafakari Sana kwa hilo.
Sijakuelewa m
Pia hautofanikiwa kimaisha usipoamua na wewe kuwa sehemu ya kusaidia wengine wengine

Ukiona hauleti chakula jua wewe ndo hicho chakula

Sipiritual usipojiweka mkao wa kuwa msaada jua utabaki kuwa mtu wa kawaida Sana at your age unabidi kujitafakari Sana kwa hilo.
Sijakuelewa mkuu
 
Hakuna dawa ya kumfanya mtu awe msiri. Wengi wanadhani kuwa msiri ni kitu unachoweza kufundishwa, la hasha!.

Kuwa msiri inachochewa na maamuzi thabiti ya mtu binafsi ndani ya moyo wake. Na hii inatokana na nyakati tofauti tofauti anazopiti, ambazo humsukuma na kufanya mustakabali mpya wa mwenendo wa maisha yake.

Otherwise tuseme kuwa kuna vitu huchochea hali ya kuwa msiri, kama vile:

Elewa Thamani ya Siri
Jifunze Kusema Hapana
Sikiliza Zaidi, Zungumza Kidogo
Chagua Unayoshiriki
Epuka Kutangaza Mambo binafsi kwenye Mitandao ya Kijamii
Heshimu Siri za Wengine

Walakin yote haya huchochewa na msukumo binafsi. Na kama utaamua basi unapaswa kuwa na msimamo thabiti kwani mpaka kuwa msiri itachukua muda.
 
Kuna mambo hayapo sawa katika maisha yako .

Tafuta mentor mzuri akujenge unaishi mediocre life usipokuwa makini utajikuta umri umeenda with zero progress .
Mkuu ungeanza wewe kunisaidia ndo maana nimekuja huku jf
 
Asante sana mkuu Kuna mishe niliipata mkoani nilishindwa kwenda mjomba anataka niende nae akapaone 😄😄 nikaacha kwenda nikaona ni uswahili
Sorry mkuu lakini hapo hata wewe umeonesha upungufu flani katika kufanya maamuzi. Maana kama ulikuwa unaenda mkoani, ungemruhusu kwenda nae akapaona then wewe ungejua jinsi gani unapanga maisha yako huko mkoani pasipo wao kujua unaishije.

Sasa umeacha kazi kwa ajili ya kuogopa kuchungwa halafu unarudi home kuchungwa nao 24/7 😁😁

Nahisi pengine maamuzi yako yanawatia mashaka kama umefikia level ya kujiamulia mambo yako perfectly
 
Sorry mkuu lakini hapo hata wewe umeonesha upungufu flani katika kufanya maamuzi. Maana kama ulikuwa unaenda mkoani, ungemruhusu kwenda nae akapaona then wewe ungejua jinsi gani unapanga maisha yako huko mkoani pasipo wao kujua unaishije.

Sasa umeacha kazi kwa ajili ya kuogopa kuchungwa halafu unarudi home kuchungwa nao 24/7 😁😁

Nahisi pengine maamuzi yako yanawatia mashaka kama umefikia level ya kujiamulia mambo yako perfectly
Mkuu Mimi na utu uzima wangu kweli nifanyiwe hivyo kama mtoto? Unaona ni sawa
 
Mkuu Mimi na utu uzima wangu kweli nifanyiwe hivyo kama mtoto? Unaona ni sawa
Maisha ni kitu kikubwa sana mkuu na si kwamba nakuhukumu au naona ni sawa ila najaribu kukusaidia kupata solution.

Walichokifanya si sahihi lakini ulichokifanya si sahihi. Imagine hiyo kazi ungeichukua na kwenda mkoani. Je, Leo hii ungefungua hii thread ?..

Nina imani huyo mjomba angepaona then akarudi kwake na kukuacha wewe uendelee na maisha yako. Hiyo ndio ilikuwa gharama ya uhuru wako ila wewe ulitumia hisia zaidi ndio maana ulifanya kitu kitakachokufanya ujihisi sawa kwa muda, ila ungewekeza akili zaidi pengine ungejitoa kwenye hiyo situation uliyonayo kwa sasa.

Experience is the best teacher, napokuambia hivi jua nimepitia hizo situations mara nyingi. Niamini mkuu, uhuru una gharama zake na kama hutaki kuwa uncomfortable kwa muda, utaishi hivyo hivyo kwa muda mrefu zaidi. Maamuzi yapo mikononi mwako 🙏🏽
 
Maisha ni kitu kikubwa sana mkuu na si kwamba nakuhukumu au naona ni sawa ila najaribu kukusaidia kupata solution.

Walichokifanya si sahihi lakini ulichokifanya si sahihi. Imagine hiyo kazi ungeichukua na kwenda mkoani. Je, Leo hii ungefungua hii thread ?..

Nina imani huyo mjomba angepaona then akarudi kwake na kukuacha wewe uendelee na maisha yako. Hiyo ndio ilikuwa gharama ya uhuru wako ila wewe ulitumia hisia zaidi ndio maana ulifanya kitu kitakachokufanya ujihisi sawa kwa muda, ila ungewekeza akili zaidi pengine ungejitoa kwenye hiyo situation uliyonayo kwa sasa.

Experience is the best teacher, napokuambia hivi jua nimepitia hizo situations mara nyingi. Niamini mkuu, uhuru una gharama zake na kama hutaki kuwa uncomfortable kwa muda, utaishi hivyo hivyo kwa muda mrefu zaidi. Maamuzi yapo mikononi mwako 🙏🏽
Sawa mkuu shukran nafanyia kazi
 
Back
Top Bottom