Mbinu zipi wamezitumia Wakinga kuwa wafalme Kariakoo?

Kama mzunguko ni mkubwa sio mbaya vocha bei ya jumla 950 kwa 475 kinacho angaliwa sio mtaji ulio tumia bali mzunguko wako wingi wa wateja
 
Kumbe hazifiki hata 2%, basi nimetaja za Wachaga tu kati ya hizo 98% zilizobaki kama unavyodai taja za Wakinga tu nyingine ziache. Taja hata nusu ya biashara za Wakinga na majina yao si umeanzisha uzi kwa akili timamu
Wakinga wanatamba njombe makete mbeya ruvuma iringa kuna asasi dar kariakoo wakinga bado wageni
 
Hatari
 
Miaka flani nikiwa kinda kitambo hiko. Nipo hotel flan na shangazi na anko na familia yao twanywa na kula siku hio hapo mwenge nikasikia ripoti inasomwa kua sijui Chama kwa mwaka huu kimekusanya bilioni moja na millioni kadhaa nazani, tulitaraji kukusanya billion tatu, tumetoa mikopo ya million mia saba pia tunampango wa kuongeza kiwango cha michango kwa wanachama ili tufikie lengo la billion tatu mwaka ujao na tutoe mikopo ya riba ndogo angalau kiasi cha billion mbili. Miaka mingi mbele nilikuja kugundua ni kina mangi walikua baada ya kumuona member mmoja kwene tv. Jamani hao watu walishapiga hatua kama miaka ile chama kilikua na billion na ushee ni miaka imepita wakuu.
 
Yule Vunjabei si mkinga yule anawawakilisha, ila nimevutiwa na huyo mangi kaoa mchina...teh.
Mkuu huyu vunja bei ametolewa na mchagga mmoja mwenye maduka ya frank knows mkuu kuna mchagga mwingine anaitwa Edward Shayo mwenye East African Brothers engineering Ltd yenye tender nchi za kuinstall na kufanya service na ana duka la kuuza vifaa vya ac na mifumo yote ya hewa nmb,crdb,nsssf,bot,akiba bank,tra nk na ndio agent wa elsweed Ltd ya misri yenye kiwanda kigamboni.
 
Aisee sio kwa huu mkeka. Umetisha Boss
Mkuu kuna wachagga kariakoo wanaitwa G 7 walianzisha chama cha kufa na kuzikana kikawa na hela nyingi sana baadaye wakibadilisha kikawa mpaka na mambo ya loans na uwekezaji sasa hivi kujiunga ni million 20tsh na ada kwa mwaka ni zaidi ya million 50tsh ndio wenye mwenge social hall na wedding halls za kutosha sinza na kimara wamejenga nyumba za kufanana bagamoyo ndio wanatakuamia,wana hospitali morogoro,coasters za special hire za kutosha,viwanja vingi hapa mjini hawa jamaa wengi ni wakibosho mkuu
 

Nimewahi kusikia hicho chama ila sikuwahi kujua kiundani. Sasa watu kama hawa ni ngumu kufilisika maana akianguka mmoja ni rahisi kupata back-up.
 
ni uchawi na ndagu. na hivyo hivyo unavyowaona hawana miaka mingi ya kuishi, wanaishi muda mchache ila kwa pesa ndefu.
 
Nimewahi kusikia hicho chama ila sikuwahi kujua kiundani. Sasa watu kama hawa ni ngumu kufilisika maana akianguka mmoja ni rahisi kupata back-up.
Na sio kimoja mkuu mfano kuna hichi cha watoto wa miaka ya 80s na 90s kinaongozwa na lampard electronics nacho ni hatari yuhu is just in his 30s lkn tiyari ana nyumba k/koo
 
Kwa sisi kwetu,walikuwa wanongoza kwa biashara ya nguo wachaga,Ila kunakipindi wakaingia wasukuma aixee wachaga walipata tabu Sana,maana wao wanauza Bei ya chini kwa faida ndogo,walikuwa wanapigwa Sana na tra, Ila bado wapi tu nilichokijua ni kwamba wao ikifika msim wanavuna mpunga wanauza,wengine wanauza ng'ombe wanakuja kujaza dukan,je unaweza kushindana nae? Hasa km wewe chanzo no kimoja? So unachotakiwa ni kuwa na pumzi msubiri mpaka afirisike maana biashara haijui huyo(sitataja mkoa husika)
 
Labda kama utakuwa unataka battle ila hao jamaa ni Wamachame wanatokea sehemu inaitwa Masama.

Na nimewahi kuwa nao karibu wanaongea Kimachame halisi siyo cha kujifunza.
Basi ntakuwa nimechanganya mafaili ila huyo mbunge wa kibaha mwenye ako catering nampigia saluti maana yupo geita analisha wafanyakazi wote wa ggm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…