Mbona hamueleweki Watz, hii gesi mnayotaka kutuuzia Wakenya ina maana sio yenu?

Mbona hamueleweki Watz, hii gesi mnayotaka kutuuzia Wakenya ina maana sio yenu?

Ni ujinga kufikiria gesi ni kwa ajili ya umeme tu! Huyo polepole hana upeo juu ya matumizi ya gesi kimapana yake!
 
Ni ujinga kufikiria gesi ni kwa ajili ya umeme tu! Huyo polepole hana upeo juu ya matumizi ya gesi kimapana yake!
Ni kweli gesi lina matumizi mengi ila Kenya inapanga kutumia gesi lenu kugenerate electricity. Kwa hivyo yupo sahihi anaposema kwamba Kenya itatumia gesi hilo kugenerate electricity.
 
Watu kama pole pole wanalipoteza Taifa..Gas kuna onshore na offshore na kuna mikataba ya uchimbwaji sio umiliki..anyways tutajua na miaka inavyoenda ukweli ni upi
 
Watu kama pole pole wanalipoteza Taifa..Gas kuna onshore na offshore na kuna mikataba ya uchimbwaji sio umiliki..anyways tutajua na miaka inavyoenda ukweli ni upi
Kuna kitu kinaitwa kitalu cha uchimbaji, vyote vilinunuliwa na Wazungu. Tangawizi na Periperi ni vitalu vya Statoil, Kuna vitalu vinamilikiwa na BG British Gas, na vingine vinamilikiwa na Orphir na makampuni mengine, TPDC wanamiliki porojo na manguo ya kijani yenye jembe na nyundo.

Tukisema CCM ni adui namba moja wa taifa hili muwe mnaelewa
 
Kha! Hizi ni chokochoko bana, kwani gesi ya nani? Ha ha ha!!!
Acheni tununue....


Huyu Jamaa anajichanganya Sana, ni sawa na kusema mafuta ya Uganda sio Yao kwasababu yanachimbwa na Total, au Mafuta huko Turkana sio ya Kenya, au umeme wa Geotherm hapo Kenya sio wa Kenya kwasababu unachimbwa na kampuni binafsi.
 
Ni ujinga kufikiria gesi ni kwa ajili ya umeme tu! Huyo polepole hana upeo juu ya matumizi ya gesi kimapana yake!

Giza ulale!

Polepole unaogeya lugha ya chama cha mazezeta au chama cha madudu [CCM].

Your mind needs a oxygen senser polepole.
 
Kuna kitu kinaitwa kitalu cha uchimbaji, vyote vilinunuliwa na Wazungu. Tangawizi na Periperi ni vitalu vya Statoil, Kuna vitalu vinamilikiwa na BG British Gas, na vingine vinamilikiwa na Orphir na makampuni mengine, TPDC wanamiliki porojo na manguo ya kijani yenye jembe na nyundo.

Tukisema CCM ni adui namba moja wa taifa hili muwe mnaelewa
Kaka jifunze vizuri neno uwekezaji katika sector ya gesi na mafuta kabla ya kuzungumza lolote, hivyo vitalu bado vipo vingi Sana hadi Leo ukitaka utapewa, hakuna hata mtanzania mmoja mwenye uwezo huo wa kumiliki na kutafuta mafuta au gesi kutokana na gharama kubwa.

Kumbuka uwezekano wa kugundua mafuta au gesi katika hivi vitalu ni chini ya 10% baada ya kutumia zaidi ya $300M bila mafanikio.

Hata hivyo serikali kwa kutumia wataalamu wake wanatafuta mafuta katika ziwa Eyasi ktk bonde la Ufa na matumaini yanaonekana.
 
Ni kweli gesi lina matumizi mengi ila Kenya inapanga kutumia gesi lenu kugenerate electricity. Kwa hivyo yupo sahihi anaposema kwamba Kenya itatumia gesi hilo kugenerate electricity.
Sasa Kama sisi wenyewe tunapunguza umeme unaotokana na gesi kwasababu ni ghali ukilinganisha na umeme wa maji, bado Kenya ikitumia gesi yetu kuzalisha umeme hairoweza kushindana na umeme wetu.

Sasa Kama gesi tunayo nyingi ya kuuza nchi za nje, vipi tukatae kuuza kwasababu tu Kenya hawatonunua umeme wetu?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kaka jifunze vizuri neno uwekezaji katika sector ya gesi na mafuta kabla ya kuzungumza lolote, hivyo vitalu bado vipo vingi Sana hadi Leo ukitaka utapewa, hakuna hata mtanzania mmoja mwenye uwezo huo wa kumiliki na kutafuta mafuta au gesi kutokana na gharama kubwa.

Kumbuka uwezekano wa kugundua mafuta au gesi katika hivi vitalu ni chini ya 10% baada ya kutumia zaidi ya $300M bila mafanikio.

Hata hivyo serikali kwa kutumia wataalamu wake wanatafuta mafuta katika ziwa Eyasi ktk bonde la Ufa na matumaini yanaonekana.
Sasa nijifunze nini? TPDC wana kisima gani?
 
Sasa nijifunze nini? TPDC wana kisima gani?
Ndio sababu nikakuambia jifunze uwekezaji katika hivyo vitalu, Sasa unauliza kabla ya kujifunza?, nimekuambia gharama ya utafutaji wa mafuta sio chini ya $300M na failure rate ni over 90%, wait TPDC itapata hiyo pesa?, Hakuna Bank Wala taasisi yoyote ya pesa duniani inayokubali kukopesha utafutaji wa mafuta na gesi kutokana na "failure rate kubwa"
 
Huyu Jamaa anajichanganya Sana, ni sawa na kusema mafuta ya Uganda sio Yao kwasababu yanachimbwa na Total, au Mafuta huko Turkana sio ya Kenya, au umeme wa Geotherm hapo Kenya sio wa Kenya kwasababu unachimbwa na kampuni binafsi.
Kwahiyo wewe unataka kusemaje?
 
Kwa hili nakataa. Gesi si Mali ya Tz, gesi ni mali ya makampuni yaliyowekeza tena bahati mbaya zaidi bei ya kutuuzia wanapanga wao
Hata dhahabu, almasi na madini yote sio Mali ya Tanzania sio?. Tofautisha Kati ya Mali ya serikali na Mali ya nchi. Kwahiyo mafuta ya Uganda, au South Sudan, Nigeria au Angola sio Mali za hizo nchi?, hakuna nchi hata Moja Kati ya hizo ambazo serikali zake zinachimba mafuta.
 
Back
Top Bottom