Mbona kelele zinazidi kuna shida gani!?

KILIO KIKUBWA NI WAPIGAJI KUINGIA KWENYE WIZARA NYETI NA KUANZA UPIGAJI WA WAZIWAZI MCHANA KWEUPE.
 
Ni wamachinga waliofukuzwa huko barabarani ndio wanapiga makelele humu JF.

Enzi za baba Yao tulikua tukipiga kelele humu wanasema acheni mzalendo achape kazi,sasa na Mimi nawaambia ANDAMANENI mle kipigo Cha Mbwa Koko.
Kwani wamachinga wanatUmia umeme wanapopanga biashara zao barabarani au wenye fremu!? Machinga ndiye anayelazimika kununua jenereta ili asikose wateja ofisini kwake!? Au machinga ndiye ana shida sana ya maji kwa kuwa anapigwa sana na jua!? Unao uwezo wa kuwapiga wote wanaoumizwa na janjajanja ya wapigaji walioshika madaraka sasa!? Hizo bangi unazopuliza hazikufai.
 
Malkia was Uingereza, angel markle ni wanaume??
Hao hawaendeshwi na yule aliyekataa kuuachia uwaziri wa mambo ya nje ingawa alikuwa Rais tayari. Yule mbembeaji kule Jamaica.
 
Hawa wanaoona mambo ni shwari ni TEAM SAMIA

Hawa wanaoona tumepotea ni TEAM MWENDAZAKE a.k a sukuma gang

Siasa chafu za jiwe zimeigawa CCM vipande 2.
Sentensi ya mwisho ndiyo inajibu swali la mtoa mada. Team Jiwe hawataki kubali kwamba uteuzi si cheo cha kudumu. Jiwe alitengua karibu teuzi zoooote za Team Msoga Ili aunde timu yake tena alitengua teuzi hizo kwa kashfa kedekede. Na wao wakaona haina shida na Timu Msoga ikakaa benchi bila kelele. Leo Timu Kizimkazi inaundwa, timu jiwe washasahu kama nao kuna timu ikitolewa ndio ikaingia timu yao. Timu Jiwe kubalini matokeo maisha yapo hivyo. Zamu itafika hata timu Kizimkazi itatolewa nayo.
Kikubwa nachokiona pia timu Kizimkazi haina kelele nyingi za kuwapumbaza watanzania kama timu Jiwe ilivyokuwa.
 
Malkia was Uingereza, angel markle ni wanaume??
Ujerumani na uingereza!? Taasisi imara baba hata ukiweka mtoto anatawala bila tabu,fikiria Trump angeitawala marekani yenye katiba na taasisi regelege Nini kingetokea? fanya Kama kuwaza tu!
 
Hizo nchi tayari zina mifumo imara zinahitaji usimamizi zaidi kuliko misuli..
Uliiona Marekani ya Trump? Alishaanza kutengeneza makundi hapa US kama alivyofanya dingi yenu. Thanks to true democratic process imemuondoa kabla hajaharibu sana. In short hata kama mkiwa na Katiba nzuri vipi, kiongozi mkuu ana nafasi kubwa pia ya kuharibu au kutengeneza. Dubai inaendeshwa na familia moja tu. Lakini kwa kuwa ni familia bora, leo Dubai inaenda. Tatizo la msingi la nchi zetu ni kutokuwa na familia bora.
 
Ujerumani na uingereza!? Taasisi imara baba hata ukiweka mtoto anatawala bila tabu,fikiria Trump angeitawala marekani yenye katiba na taasisi regelege Nini kingetokea? fanya Kama kuwaza tu!
Lakini je, Marekani umeona ilivyogawanyika katika kipindi chake? Katiba imara ni jambo bora lkn watu imara ni jambo bora zaidi. Tanzania haina mifumo ya kuzalisha watu imara maana mifumo ya kifamilia na kielimu haujaweka kuandaa watu kuwa imara.
 
Hizi bangi ninazopuliza hazinipi stimu tena,njoo nikupulize hayo matakoh.
 
Mambo tele hayaendi vizuri ni mazuzu tu wanaona hali ni shwari.

Nimekaa na kutafakari sana bila majibu, hasa kuhusiana na namna malalamiko yanazidi kuongezeka mitandaoni.
 
Sikh mia za mwanzo nilimuelewa sana na alikuwa anaeleweka bila utata.
Baada ya hapo nadhani alipata washauri nje ya wale Siku 100.
Wanamharibia kikwelikweli.
Sijui kwanini watu mnaukwepa ukweli na kuwavika lawama washauri hewa tusiowajua.

Siku zote kama wewe si mwizi huwezi ambiwa uibe na ukaiba kweli and vise versa is true, haihitajia hata mtu akushauri ndio utekeleze ubaya wako.

Tunachokiona kutoka kwa SSH ndio rangi yake hailisi. Na mbaya zaidi ameshafahamu kuwa watu mna mtetea kwa kutokuamini kama ni yeye anayafanya hayo, matokeo yake na yeye anatembelea humohumo kwenye hizo huruma zenu!
 
Kutokuridhika na yaliyopo kwa sababu tofauti
 
Ukweli sasa hivi hali ni ngumu Sana,sema sisi wengine ni Wazee wa kujikaza kiume huku tukingoja kudra za Mwenyezi MUNGU.
 
Malkia was Uingereza, angel markle ni wanaume??
Hao wanaongoza nchi zenye taasisi imara siyo sisi hapa na polisi wetu,takukuru yetu,uhamiaji yetu hizo ni baadhi ya taasisi zisizo imara kabisa.
 
Kwa nchi yetu ambayo haina mifumo imara..mwanamke hawezi na hafai kua kiongozi..ndioa mana hukuwii kumsikia ssh akilia masuala ya usawa wa kijinsia..namuomba ikifika 2025 apumzike tu..

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…