Pre GE2025 Mbowe ashauriwe kutogombea tena uenyekiti wa CHADEMA, siasa ni muonekano (perception) kwanza

Pre GE2025 Mbowe ashauriwe kutogombea tena uenyekiti wa CHADEMA, siasa ni muonekano (perception) kwanza

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Baada ya Tundu Lissu kujitosa kugombea uenyekiti wa CHADEMA ni wazi kutakuwa na mchuano mkali sana endapo Mbowe naye ataamua kugombea tena nafasi hiyo. Huo ushindani hautakuwa na afya kwa CHADEMA zaidi sana endapo Mbowe atashinda tena, kwa mantiki hiyo ni vyema basi Mbowe akaamua au akashauriwa kutogombea tena nafasi hiyo kwa sasa.

Hofu kubwa ya Wanachedema imekuwa kupatikana mtu atakayemrithi Mbowe ambaye hawezi kununulika au kutumika na chama tawala kuihujumu CHADEMA, katika eneo hilo Lissu anatosha na hakuna mtu anayeweza kumtilia mashaka.

Mambo ya faida kwa Mbowe kutokugombea tena uenyekiti ni pamoja na kumaliza kelele za ukanda, uchagadema, uchawa na kung'ang'ania madaraka ambazo Mbowe na CHADEMA wamekuwa wakirushiwa. Japo ni hoja zisizo na mashiko au uhalisia wowote wa maana kwa CHADEMA lakini hazikipi CHADEMA sura nzuri kwa sababu siasa wakati mwingi ni kuhusu muonekano (perception) kwanza ndipo mambo ya sera, uhalisia na ukweli yanafuata.
 
Baada ya Tundu lissu kuonesha nia ya kugombea uenyekiti ndani ya CHADEMA, ni Mbowe anakwenda kupata wakati hasa kama naye atagombea maana hakuna ataweza shinda kihalali .

Wana CHADEMA tunataka mabadiliko na tunaitaka dola tofauti na msimamo na mitizamo ya Mwenyekiti.

Busara kwa Mwenyekiti ni kujitoa na kubakia mlezi wa Chama
 
Ni kweli Mbowe kajichokea lakini sauti bado inasema Lissu is not a better replacement!! Tulisema kwa Magufuli tulidhihakiwa na sasa tunasema kwa Lissu!

Nampenda sana Lissu lakini kwa hiyo nafasi hayuko matured kusimamia wenzake.
 
Chadema impitishe Tundu Lissu kuwa mwenyekiti mpya na wamuandae kuwa mgombea uraisi pamoja na kumpata mgombea mwenza.

Mheshimiwa Mbowe awe mlezi na mshauri na awe mjumbe wa kudumu halmashauri kuu wa chama.

Pia Chadema iajiri strategist zaidi ya wannę ambao watakiandaa chama kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwakani 2025.

Sambamba na hilo aajiriwe meneja wa kampeni ambae ndie atashughulikia masuala yote ya rasilimali watu, usimamizi wa kampeni nchini kote.

Kwa kufanya hivyo kitaweza kurekebisha na kuboresha kitu chaitwa “ground game” ambayo ndo yaonekana kukididimiza chama.
 
Ni kweli Mbowe kajichokea lakini sauti bado inasema Lissu is not a better replacement!! Tulisema kwa Magufuli tulidhihakiwa na sasa tunasema kwa Lissu!

Nampenda sana Lissu lakini kwa hiyo nafasi hayuko matured kusimamia wenzake.
Kabla hajawa Rais Magufuli hakuwahi kuongea kuhusu katiba mpya , hakuwahi kuzungumza historia ya Tanzania kama Lissu, hakuwahi kuoneka mstari wa mbele akipambana na ufisadi bungeni, hakuwahi kuonekana akiwatetea wanyonge kama Lissu huko migodini na katika siasa. Lissu anayo mambo yote ya kumfanya kuwa mwenyekiti bora wa CHADEMA.
 
Kabla hajawa Rais Magufuli hakuwahi kuongea kuhusu katiba mpya , hakuwahi kuzungumza historia ya Tanzania kama Lissu, hakuwahi kuoneka mstari wa mbele akipambana na ufisadi bungeni, hakuwahi kuonekana akiwatetea wanyonge kama Lissu huko migodini na katika siasa. Lissu anayo mambo yote ya kumfanya kuwa mwenyekiti bora wa CHADEMA.
Kuzungumza na kutenda ni tofauti. Hulka ya mtu huwa kigezo kikubwa sana cha uongozi. Lissu hafai kuwa msimamizi wa wenzie. Muda ni hakimu wa yote.
 
Ni kweli Mbowe kajichokea lakini sauti bado inasema Lissu is not a better replacement!! Tulisema kwa Magufuli tulidhihakiwa na sasa tunasema kwa Lissu!

Nampenda sana Lissu lakini kwa hiyo nafasi hayuko matured kusimamia wenzake.

Anatakiwa malaika gabriel? Muache aunde taasisi keshasema na hayo mapungufu yake atakuwa na team ya kuyacover! Lakini umetumia kipimo gani kujua hatoshi boss?
 
Mr Mbowe should have known this saying: “A good dancer knows when to leave the stage,” Patrick Lumumba once said. Mr Mbowe, with all due respect, 20 years is enough time to mentor young leaders and let them move the party to even higher heights! Mr Mboye, please honourably rescind your candidature as party chairman.
 
Mbowe awe mweka hazina wa chama, ela ziendelee pitia kwake. Amwachie Lissu uenyekiti.
 
Baada ya Tundu Lissu kujitosa kugombea uenyekiti wa CHADEMA ni wazi kutakuwa na mchuano mkali sana endapo Mbowe naye ataamua kugombea tena nafasi hiyo. Huo ushindani hautakuwa na afya kwa CHADEMA zaidi sana endapo Mbowe atashinda tena, kwa mantiki hiyo ni vyema basi Mbowe akaamua au akashauriwa kutogombea tena nafasi hiyo kwa sasa.

Hofu kubwa ya Wanachedema imekuwa kupatikana mtu atakayemrithi Mbowe ambaye hawezi kununulika au kutumika na chama tawala kuihujumu CHADEMA, katika eneo hilo Lissu anatosha na hakuna mtu anayeweza kumtilia mashaka.

Mambo ya faida kwa Mbowe kutokugombea tena uenyekiti ni pamoja na kumaliza kelele za ukanda, uchagadema, uchawa na kung'ang'ania madaraka ambazo Mbowe na CHADEMA wamekuwa wakirushiwa. Japo ni hoja zisizo na mashiko au uhalisia wowote wa maana kwa CHADEMA lakini hazikipi CHADEMA sura nzuri kwa sababu siasa wakati mwingi ni kuhusu muonekano (perception) kwanza ndipo mambo ya sera, uhalisia na ukweli yanafuata.
Kwa sasa Mbowe bado anahitajika kuliko hata wakati uliopita.
 
Back
Top Bottom