Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema kilichofanyika kwa wabunge 19 waliopelekwa bungeni bila idhini ya chama ilikuwa ni uhuni, na ni kuvunja Katiba.
Amesema wabunge hao walikuwa ni viongozi wao, hata hivyo mchakato wa kuwapeleka bungeni haukuwa mchakato wenye baraka za chama. Wale walikuwa sehemu yetu, lakini waliowasaidia kuingia bungeni ni wenzako (Rais Samia).
Baadhi ya vyombo vya habari vilipotosha kusema kuwa CHADEMA iliridhia kuwapeleka wabunge wale bungeni. Wale wabunge hawakilishi mtu wanawakilisha familia zao, bunge na spika wameamua kuwalinda.
Wewe Rais ndio unayeidhinisha mishahara yao, liangalie hili uepushe matumizi mabaya ya kodi za wananchi kwa wabunge wale wasiomuwakilisha mtu.
Mbowe ameyasema hayo akiongea na wanawake wa CHADEMA katika Siku ya Wanawake Duniani, ambayo Mgeni Rasmi alikuwa Rais Samia.
Amesema wabunge hao walikuwa ni viongozi wao, hata hivyo mchakato wa kuwapeleka bungeni haukuwa mchakato wenye baraka za chama. Wale walikuwa sehemu yetu, lakini waliowasaidia kuingia bungeni ni wenzako (Rais Samia).
Baadhi ya vyombo vya habari vilipotosha kusema kuwa CHADEMA iliridhia kuwapeleka wabunge wale bungeni. Wale wabunge hawakilishi mtu wanawakilisha familia zao, bunge na spika wameamua kuwalinda.
Wewe Rais ndio unayeidhinisha mishahara yao, liangalie hili uepushe matumizi mabaya ya kodi za wananchi kwa wabunge wale wasiomuwakilisha mtu.
Mbowe ameyasema hayo akiongea na wanawake wa CHADEMA katika Siku ya Wanawake Duniani, ambayo Mgeni Rasmi alikuwa Rais Samia.