Mbowe: Kukosa pesa za MCC Inachafua jina la nchi ktk medani za kimataifa

Mbowe: Kukosa pesa za MCC Inachafua jina la nchi ktk medani za kimataifa

Joined
Sep 28, 2014
Posts
78
Reaction score
113
Sasa imethibitika kuwa Bodi ya MCC iliyokaa tarehe 16 Dec 2015 imehairisha rasmi kuidhinisha msaada wa Millenium Challenge uliokuwa umekusudiwa kwa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2016.

Sababu kuu mbili zilizosababisha uamuzi huo ni:

1. Mkwamo wa Uchaguzi wa Rais na Wawakilishi Zanzibar na
2. Matumizi mabaya ya sheria ya makosa ya mtandao hususan kuhusiana na uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa 2015.

Kauli yangu juu ya jambo hili ni hii;

1. Ubabe wa baadhi ya viongozi wa CCM ni janga la Taifa. Kuchelewa kupatikana kwa fedha za MCC si tu kunachafua jina la nchi na hadhi yake katika medani za kimataifa, bali kutaathiri kwa kiasi kikubwa miradi yote iliyo chini ya ufadhili wa MCC.

2. Sheria ya makosa ya mtandao (Cyber Crime Act 2015) ni sheria mbaya sana inayokinzana na kukua kwa technologia ya habari na mawasiliano. Aidha, kwa makisudi kabisa inafifisha uhuru wa kupashana habari na ni dhahiri ilitungwa kwa nia mbaya ya kuthibiti kijinai uchaguzi mkuu.

Tuliipinga sheria hii Bungeni na ikapitishwa usiku wa manane kwa ubabe wa wabunge wa CCM na hata tulipomtaka rais Kikwete asiisaini aliisaini kibabe akijua anaandaa mazingira gani ya "kihalifu".

Sheria hii ilitumika kuvamia vituo vyetu vya kukusanya matokeo ya kura za rais na wabunge na mpaka Leo vijana wetu zaidi ya 161 wana kesi za "kubumba" mahakamani.

Aidha Sheria hii ilitumika kuficha dhana ovu kuvamia kituo cha Sheria na haki za binadamu (LHRC) waliokuwa wakikusanya matokeo ya kura za Rais .

Vile vile Sheria hii imetumika kuwakamata na kuwaweka ndani na hata kuwanyima dhamana vijana wetu ambao walituunga mkono katika uchaguzi mkuu.

Namtaka rais Magufuli achukue hatua za kiuongozi na kiutawala kwa kufanya yafuatayo:

1. Aumalize mgogoro wa kisiasa Zanzibar kwa kuhakikisha kuwa mshindi halali anatangazwa .

2. Achukue hatua ya kuifanyia marekebisho makubwa Sheria ya makosa ya mtandao katika bunge lijalo. Aidha wale wote waliobambikiwa kesi amuamuru DPP kuzifuta kesi hizo Mara moja.

Hatua hizo zitalinusuru taifa na hasara ya kupoteza mabilioni hayo ya MCC na zaidi kuepusha kuporomoka zaidi kwa biashara ya Utalii nchini Zanzibar.
 
Eti namtaka rais achukue hatua...kwa hiyo mbowe amemtambua magufuli?
 
Mabadiliko yanapoanza yana gharama zake, Magufuli alitangaza mabadiliko pia hivyo binafsi huu ndio mwanzo wenyewe wa mabadiliko! Si kila kitu kiwe namna kilivyokuwa mwanzo! Yote haya ndo mabadiliko maana ni lazima tukutane na changamoto mbalimbali ili kuja kufikia mahali tunapohitaji! Tumpe muda Magufuli kwani hata yeye hili kaliona na bila shaka atajitahidi kuweka mambo ya msingi mbele ili kukabiliana na changamoto zitakazoendelea kutokana na suala la Zanzibar!
 
Mbowe ni raia km walivyo raia wengne wa TANZANIA hvyo ana haki ya kueleza ama kushauri awezavyo ama kuzungumza ilmrad hapingan na katiba.
 
Kauli yangu juu ya jambo hili ni hii
Ubabe wa baadhi ya viongozi wa CCM ni janga la Taifa. Kuchelewa kupatikana kwa fedha za MCC si tu kunachafua jina la nchi na hadhi yake katika medani za kimataifa, bali kutaathiri kwa kiasi kikubwa miradi yote iliyo chini ya ufadhili wa MCC.

Nchi zote duniani huhitaji chama imara cha upinzani kinachoweza saidia serikali iliyopo madarakani kutawala vizuri.Vyama vya upinzani imara huwa ni jicho la pili la serikali kuishitua endapo kuna madudu ndani ya serikali ambayo Raisi au serikali yaweza kuwa hayana taarifa nayo.Pia wafadhili wan je hupenda kuwepo chama pinzani imara kinachoaminika katika nchi ili kuwa jicho lao (WATCH DOG) ya kuangalia kama misaada yao inatumika ipasavyo.
Madudu hayo yaweza kuwa kashfa mbali mbali za ufisadi nk.Chama pinzani chaweza yafichua kupitia wabunge wake kulipuka bungeni n.k


CHADEMA kwa miaka Zaidi ya 20 kilijipambanua kama chama pinzani imara chenye dhamira ya dhati ya kupambana na ufisadi.Kiasi kuwa kikaaminiwa na wananchi wakawa wako tayari hata kukipelekea hati za siri za watu kama Lowasa na wengineo ili wazifanyie kazi.Na wao wakawa waaminifu wakawa wakilipuka bungeni na mikutano ya hadhara hadi baraza la mawaziri likavunjwa mara kibao kwa sababu ya hoja za ufisadi za CHADEMA bungeni.
Wafadhili nao wakatokeaa kuwaamini sana tena sana CHADEMA wakijua kuwa ni chama hodari na kilichodhamiria kupambana na ufisadi kiasi kuwa ripoti za CHADEMA za ufisadi zilipowafikia wafadhili zikiwa na majina ya akina Lowassa nk, wafadhili waliwasikiliza wakazuia misaada ya mabilioni ya pesa zikiwemo za madawa mahospitalini na za kuboresha sekta ya afya na elimu wakitaka suala la ufisadi wa watu kama Lowasa limalizike kwanza ndipo pesa zitoke
Baada ya Tanzania kunyimwa pesa za wafadhili zikiwemo za sekta ya afya na elimu wagonjwa wengi wakaanza kuwa wanalala chini na dawa zikaanza kuwa hazipo mahospitalini,watoto wakawa wanasoma wamekaa chini na serikali kushindwa kuongeza ubora wa elimu sababu ya uwezo mdogo wa serikali.

Tatizo la huduma za afya na elimu zilipoanza kudorora CHADEMA wakaanza kampeni kusema serikali ndio inayosababisha yote hayo wakati ukweli ni CHADEMA ndiyo iliyosababisha wafadhili wasimamishe misaada kwa tuhuma za kusema akina Lowasa mafisadi wakubwa wanazibomoa pesa zao.

Kama kuna chama kilichowasaliti na kuwaumiza watanzania ni CHADEMA.Watu wameumia sana kwa huduma mbovu sekta ya afya na elimu kwa sababu ya CHADEMA .CHADEMA kinatakiwa kiwaombe radhi watanzania walioumia kwa huduma mbovu za afya na elimu zilizosabisha hadi vifo kwa wengine baada ya wafadhili kusimamisha misaada kwa umbeya uliopelekwa na CHADEMA kwa wafadhili uliopelekea misaada ya kibajeti kusimamishwa.Wasizunguke tu na Lowasa wawaombe radhi watanzania kwa hasara waliyowatia kimaendeleo ya afya na Elimu.

Ndio maana nahitimisha kwa kusema mgombea Lowasa wa Chadema ALISHINDWA KUPITA KWA Kuwa CHADEMA kimelaaniwa na wale walioathirika na huduma duni za elimu na afya zilizosababishwa na kukosa hela za wafadhili.Laana ya wagonjwa walalo chini,na wakosa dawa na wale watoto wakaao chini bila madawati na kusoma kwenye nyumba za nyasi,Na walimu wafanyao kazi mazingira magumu ziliwafanya CHADEMA washindwe sana safari hii kuanzia ubunge,udiwani hadi uraisi.

Hili la MCC CHADEMA wamechangia sana kuhujumu ili pesa za wafadhili zikosekane na huduma zishindwe kufanyika halafu wao ndio utakuta baadae wanapita kubwata ona Umeme hamna ni CCM hao!! Wakati wao wamehusika kuchonga MCC.

Hebu fikiria MCC inaweza shupalia kuwa haitioi hela sababu za wale vijana wa CHADEMA na Kituo cha haki za binadamu waliodakwa na kufunguliwa mashtaka.Kesi iko mahakamani hivi MCC hawajui utawala wa sheria hadi waamue tu wenyewe kutoa hukumu kuwa serikali imekosea? Si wangesubiri maamuzi ya mahakama.Hapa wazi kunaonyesha kuna mkono wa CHADEMA.Hivi au inawezekana hiyo software ya kuingilia Uchaguzi ya hao waliokamatwa ilinunuliwa na kufadhiliwa na MCC? Kwa nini MCC wasisubiri maamuzi ya mahakama?

Zanzibar pia kuna malalamiko kuwa kuna vituo vinaonyesha wapiga kura walikuwa wengi kuliko waliojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.Inaonyesha wazi kuwa kule pia vijana wa IT walichezea mtandao wa ZEC kwa kuungilia.MCC kuna kitu wanaficha lakini yawezekana mtandao ule wa kuingilia matokeo ulikuwa wao.Hatua wanazochukua unaziona kabisa ni za PRO-UKAWA na zinalenga kwenye IT zaidi.MCC nao wawe wakweli.Kuna kitu hawako wazi mahali.
 
mbowe anafurahia sisi tukiwa omba omba milele lakini yeye ana mapesa huko nje ya nchi. badala ya kushauri namna ya kuongeza pato la taifa ili kufidia hili gap anazidi kuunga mkono mabeberu wenzake.
 
Hizo fedha za MCC ndizo zilizofanya ndugu zenu waishio vijijini kupata umeme. Kama Magufuli ana dhamila ya dhati kusaidia Taifa hili hana budi kutatua mgogoro wa zanzibar haraka sana. Nashangaa kuona watu wanamshabikia Magufuli kama timu ya mpira. Sasa naanza kuamini tafiti zilizoonesha kuwa "BLACK PEOPLE ARE NOT AS SMART AS WHITE"
 
Hapa kazi tu..fedha za ndani zitapatikana. hao wamarekani kwani hawaoni kasi ya kupambana na rushwa kama ni kuleta utawala bora hadi watunyime hizo hela. vinginevyo wana lao jambo.
 
Ukiona mtu anashabikia wazungu muogope kama ukoma. Misaada unaiua uchumi.
 
Magu kusanya kodi vya kutosha....pato la ndani ndio muhimu misaada inakuja kikoloni koloni......
 
Mbowe mtu wa ajabu sana badala ya kushinikiza Serikali kukusanya zaidi kwa mapato Ya ndani anataka tanzanie iendelee kulilia msaada. Halafu bungeni anaanza lia lia oooh bajet inategemea wafadhili wa nje. Ni muda wa kujitegemea
 
Hizo fedha za MCC ndizo zilizofanya ndugu zenu waishio vijijini kupata umeme. Kama Magufuli ana dhamila ya dhati kusaidia Taifa hili hana budi kutatua mgogoro wa zanzibar haraka sana. Nashangaa kuona watu wanamshabikia Magufuli kama timu ya mpira. Sasa naanza kuamini tafiti zilizoonesha kuwa "BLACK PEOPLE ARE NOT AS SMART AS WHITE"

Kwa mawazo yangu nafikiri MCC inatakiwa itatue mgogoro wa IT wa ule mfumo wa komputa uliokuwa ukiingilia mtandao wa NEC na ZEC.Mgogoro wa uchaguzi unahusika hasa na ule mfumo wa kijangili uliokuwa ukiingilia matokeo ya NEC na ZEC na kuzalisha matokeo ya kugushi. Bila shaka MCC wanalijua hilo vizuri.

NEC waliwahi mapema na kuwadaka wahusika na wako mahakamani. ZEC wakachelewa ndio maana imependekezwa Uchaguzi urudiwe ili matokeo yakusanywe na Mtandao usioingiliwa. MCC kuingilia na kusema hawatoi hela kuna tatizo kwenye chaguzi mmmmmmmm!!!! Mhusika hasa wa hilo tatizo ni nani? Sio MCC wenyewe kweli? Sio wao waliofadhili?

Isije kuwa wanatengeneza tatizo halafu wanataka mtu mwingine atatue. Si watatue wenyewe?
 
Kwanza Mbowe hamtambui Magufuli sasa kwanini aambiwe Kama haumtambui? Pili, hatuwezi kuuza Uhuru wetu kwa sababu ya vijana wa CHADEMA waliotaka kusevu matakwa ya wachache na kuleta fujo katika nchi hii.

Kwa akili ya Mbowe Marekani akimwambie Tanzania iruhusu ushoga atabadili hata na sheria ya nchi. Kama aliweza kununuliwa na LOWASSA sababu ya pesa kwanini asibadili sheria ili apate fedha za Wamarekani?
 
Back
Top Bottom