Mbowe kwa aliyopitia na aliyofanya, naumizwa na kejeli dhidi yake LAKINI ni Muhimu sana atumie Hekima

Mbowe kwa aliyopitia na aliyofanya, naumizwa na kejeli dhidi yake LAKINI ni Muhimu sana atumie Hekima

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Sidhani kama kuna mtu ambaye anaweza kusimama na kwa dhamira akazikataa jitihada za Mbowe katika kuijenga CHADEMA na katika kupigania haki na demokrasia nchini Tanzania.

Ni katika jitihada hizo, Mbowe aliwekwa mahabusu za polisi mara kadhaa, alifilisiwa kwa nguvu, alitumia muda wake, rasilimali zake, akili yake na kila jitihada kuhakikisha nchi inapiga hatua katika uhuru, haki na demokrasia, na zaidi kuifanya CHADEMA kuongoza katika jitihada hizi. Kama binadamu, Mbowe katika kuyatenda hayo, yawezekana alifanya makosa ya hapa na pale. Hiyo ni kawaida.

Lakini pamoja naye, wapo Watanzania wengi walioungana naye, nao walipambana na kupoteza mengi, wengine mpaka uhai wao (Mungu wa huruma awarehemu). Miongoni mwa walioumizwa sana katika mapambano haya ni Tundu Lisu, na wengi tuwajuao.

Mbowe na Lisu na hawa wengine wote walioumizwa kwa namna mbalimbali kwaajili ya kuipigania Tanzania na CHADEMA, walistahili kuheshimiwa na kukumbukwa daima katika historia yetu.

Kuna mahali Mbowe na Lisu, wanataka kukosea. Na makosa wanayoyafanya yanaweza kuwafanya wapoteze heshima kubwa ambayo wanastahili. Kwa yanayoendelea sasa, tumefikia hata watu wasio na mchango wowote wa maana katika nchi hii, watu kama Ntobi na Steve, wanawadhihaki na kuwakejeli miamba hii mikubwa ya siasa za upinzani.

Kabla muda haujaenda, Mbowe na Lisu, wafedhehesheni wapuuzi hawa. Haraka mnaweza kufanya yafuatayo:
1. Kwa uwazi kabisa, onesheni kuwa hakuna uhasama baina yenu maana mnachokioigania ni kimoja ingawa mnaweza kutofautiana katika mawazo na mbinu namna ya kutekeleza.
2. Mbowe muda uliokitumikia Chama ni mrefu sana, tangaza kujiondoa na kuwaunga mkono wote waliogombea kuchukua nafasi yako, na kutamka wazi kuwa utampa ushirikiano wa kutosha yeyote atakayechaguliwa.
3. Lisu jitahidi kuzuia kauli zinazoweza kutafsiriwa kama ni personal attack dhidi ya mwenyekiti wako, japo una haki ya kutofautiana naye kimbinu endapo utachaguliwa. Ni vema na ni sahihi kabisa kuweka bayana juu ya mambo utakayoyafanya tofauti na mtangulizi wako, endapo utachaguliwa.

4. Lisu endelea kuzipuuza kauli za kejeli dhidi yako kutoka kwa watu ambao hawana mchango wowote wa maana katika harakati hizi za kuitafuta haki na demokrasia.

5. Katibu Mkuu Mnyika, wakati wagombea wako wa nafasi ya umwenyekiti wakijizuia kupambana na watu binafsi, jukumu la kutunza nidhamu na maadili lipo mikononi mwako. Toa maelekezo kwa mamlaka zinazohusika kuchukua hatua dhidi ya wote wanaoonekana kutoa kauli zinazokiuka maadili ya chama, lakini kwa kufuata taratibu na katiba ya chama, bila ya kumwonea au kumpendelea mtu.

Mbowe usiipe nafasi CCM kukutumia wewe katika kuleta mfarakano ndani ya chama. Mbinu inayotumika sasa ya kuonesha kuwa wewe ni kipenzi cha CCM na Serikali ya CCM, ni silaha mbaya sana dhidi yako.
 
Sidhani kama kuna mtu ambaye anaweza kusimama na kwa dhamira akazikataa jitihada za Mbowe katika kuijenga CHADEMA na katika kupigania haki na demokrasia nchini Tanzania.

Ni katika jitihada hizo, Mbowe aliwekwa mahabusu za polisi mara kadhaa, alifilisiwa kwa nguvu, alitumia muda wake, rasilimali zake, akili yake na kila jitihada kuhakikisha nchi inapiga hatua katika uhuru, haki na demokrasia, na zaidi kuifanya CHADEMA kuongoza katika jitihada hizi. Kama binadamu, Mbowe katika kuyatenda hayo, yawezekana alifanya makosa ya hapa na pale. Hiyo ni kawaida.

Lakini pamoja naye, wapo Watanzania wengi walioungana naye, nao walipambana na kupoteza mengi, wengine mpaka uhai wao (Mungu wa huruma awarehemu). Miongoni mwa walioumizwa sana katika mapambano haya ni Tundu Lisu, na wengi tuwajuao.

Mbowe na Lisu na hawa wengine wote walioumizwa kwa namna mbalimbali kwaajili ya kuipigania Tanzania na CHADEMA, walistahili kuheshimiwa na kukumbukwa daima katika historia yetu.

Kuna mahali Mbowe na Lisu, wanataka kukosea. Na makosa wanayoyafanya yanaweza kuwafanya wapoteze heshima kubwa ambayo wanastahili. Kwa yanayoendelea sasa, tumefikia hata watu wasio na mchango wowote wa maana katika nchi hii, watu kama Ntobi na Steve, wanawadhihaki na kuwakejeli miamba hii mikubwa ya siasa za upinzani.

Kabla muda haujaenda, Mbowe na Lisu, wafedhehesheni wapuuzi hawa. Haraka mnaweza kufanya yafuatayo:
1. Kwa uwazi kabisa, onesheni kuwa hakuna uhasama baina yenu maana mnachokioigania ni kimoja ingawa mnaweza kutofautiana katika mawazo na mbinu namna ya kutekeleza.
2. Mbowe muda uliokitumikia Chama ni mrefu sana, tangaza kujiondoa na kuwaunga mkono wote waliogombea kuchukua nafasi yako, na kutamka wazi kuwa utampa ushirikiano wa kutosha yeyote atakayechaguliwa.
3. Lisu jitahidi kuzuia kauli zinazoweza kutafsiriwa kama ni personal attack dhidi ya mwenyekiti wako, japo una haki ya kutofautiana naye kimbinu endapo utachaguliwa. Ni vema na ni sahihi kabisa kuweka bayana juu ya mambo utakayoyafanya tofauti na mtangulizi wako, endapo utachaguliwa.

4. Lisu endelea kuzipuuza kauli za kejeli dhidi yako kutoka kwa watu ambao hawana mchango wowote wa maana katika harakati hizi za kuitafuta haki na demokrasia.

5. Katibu Mkuu Mnyika, wakati wagombea wako wa nafasi ya umwenyekiti wakijizuia kupambana na watu binafsi, jukumu la kutunza nidhamu na maadili lipo mikononi mwako. Toa maelekezo kwa mamlaka zinazohusika kuchukua hatua dhidi ya wote wanaoonekana kutoa kauli zinazokiuka maadili ya chama, lakini kwa kufuata taratibu na katiba ya chama, bila ya kumwonea au kumpendelea mtu.

Mbowe usiipe nafasi CCM kukutumia wewe katika kuleta mfarakano ndani ya chama. Mbinu inayotumika sasa ya kuonesha kuwa wewe ni kipenzi cha CCM na Serikali ya CCM, ni silaha mbaya sana dhidi yako.
Hivi unajua kwanini marais wengi wa Afrika ambao walipigania uhuru baada ya ya uhuru walikuwa hawataki kuachia madaraka? Ni kwa sababu akili zao na mawazo yao ni kama ya Mbowe na mnaomuunga mkono. Mnaona yuko entitled kuwa pale maisha, yani ni kama vile chama ni cha kwake.
Ndiyo maana hata wakina Mugabe walikuwa wanaona kuachia madaraka haiwezekani maana ni kama vile wanayaacha kwa watu wengine ambao ni wakuja wakati wao ndiyo waliopigania uhuru.
Ni jambo la busara na la maana knowing when to quit.
Ukifanya jambo jema, jua ni muda gani wa kuquit otherwise binadamu wana tabia ya kusahau mazuri yote ukianza kuwaboa.
 
Sidhani kama kuna mtu ambaye anaweza kusimama na kwa dhamira akazikataa jitihada za Mbowe katika kuijenga CHADEMA na katika kupigania haki na demokrasia nchini Tanzania.

Ni katika jitihada hizo, Mbowe aliwekwa mahabusu za polisi mara kadhaa, alifilisiwa kwa nguvu, alitumia muda wake, rasilimali zake, akili yake na kila jitihada kuhakikisha nchi inapiga hatua katika uhuru, haki na demokrasia, na zaidi kuifanya CHADEMA kuongoza katika jitihada hizi. Kama binadamu, Mbowe katika kuyatenda hayo, yawezekana alifanya makosa ya hapa na pale. Hiyo ni kawaida.

Lakini pamoja naye, wapo Watanzania wengi walioungana naye, nao walipambana na kupoteza mengi, wengine mpaka uhai wao (Mungu wa huruma awarehemu). Miongoni mwa walioumizwa sana katika mapambano haya ni Tundu Lisu, na wengi tuwajuao.

Mbowe na Lisu na hawa wengine wote walioumizwa kwa namna mbalimbali kwaajili ya kuipigania Tanzania na CHADEMA, walistahili kuheshimiwa na kukumbukwa daima katika historia yetu.

Kuna mahali Mbowe na Lisu, wanataka kukosea. Na makosa wanayoyafanya yanaweza kuwafanya wapoteze heshima kubwa ambayo wanastahili. Kwa yanayoendelea sasa, tumefikia hata watu wasio na mchango wowote wa maana katika nchi hii, watu kama Ntobi na Steve, wanawadhihaki na kuwakejeli miamba hii mikubwa ya siasa za upinzani.

Kabla muda haujaenda, Mbowe na Lisu, wafedhehesheni wapuuzi hawa. Haraka mnaweza kufanya yafuatayo:
1. Kwa uwazi kabisa, onesheni kuwa hakuna uhasama baina yenu maana mnachokioigania ni kimoja ingawa mnaweza kutofautiana katika mawazo na mbinu namna ya kutekeleza.
2. Mbowe muda uliokitumikia Chama ni mrefu sana, tangaza kujiondoa na kuwaunga mkono wote waliogombea kuchukua nafasi yako, na kutamka wazi kuwa utampa ushirikiano wa kutosha yeyote atakayechaguliwa.
3. Lisu jitahidi kuzuia kauli zinazoweza kutafsiriwa kama ni personal attack dhidi ya mwenyekiti wako, japo una haki ya kutofautiana naye kimbinu endapo utachaguliwa. Ni vema na ni sahihi kabisa kuweka bayana juu ya mambo utakayoyafanya tofauti na mtangulizi wako, endapo utachaguliwa.

4. Lisu endelea kuzipuuza kauli za kejeli dhidi yako kutoka kwa watu ambao hawana mchango wowote wa maana katika harakati hizi za kuitafuta haki na demokrasia.

5. Katibu Mkuu Mnyika, wakati wagombea wako wa nafasi ya umwenyekiti wakijizuia kupambana na watu binafsi, jukumu la kutunza nidhamu na maadili lipo mikononi mwako. Toa maelekezo kwa mamlaka zinazohusika kuchukua hatua dhidi ya wote wanaoonekana kutoa kauli zinazokiuka maadili ya chama, lakini kwa kufuata taratibu na katiba ya chama, bila ya kumwonea au kumpendelea mtu.

Mbowe usiipe nafasi CCM kukutumia wewe katika kuleta mfarakano ndani ya chama. Mbinu inayotumika sasa ya kuonesha kuwa wewe ni kipenzi cha CCM na Serikali ya CCM, ni silaha mbaya sana dhidi yako.
hekima na busara za wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema Taifa ni muhimu zaidi zikaelekezwa katika kuziba mdomo na makelele ya kibaraka wa mabwenyenye ya magharibi mwenye tamaa na uchu wa madarka na vyeo kupindukia.

Kwa umoja wao wajumbe watoe adabu ili iwe fundisho kwa wenye midomo wengine ndani ya chadema 🐒
 
Mbowe anatuona makamanda kama mandondocha yake maana hatuwezi kumshauri wala kumkosoa na kila kitu ni ndio hata kama haikupaswa kuwa ndio.
Imetosha sasa kufanywa mandondocha akae pembeni abaki kuwa mzee wa chama.
 
hekima na busara za wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema Taifa ni muhimu zaidi zikaelekezwa katika kuziba mdomo na makelele ya kibaraka wa mabwenyenye ya magharibi mwenye tamaa na uchu wa madarka na vyeo kupindukia.

Kwa umoja wao wajumbe watoe adabu ili iwe fundisho kwa wenye midomo wengine ndani ya chadema 🐒
Naona unasimama na muonga uongozi kwa mahawala zake na kuwa acha makamanda tukiwa wana harakati. Inatosha sasa.
 
Lissu hatoshi, Mbowe ana hekima.

Huu mahala wake wa mwisho aandae mrithi sasa.

Huwezi kuwaachia chama wenye siasa za ki ‘demagogue’ na hawajui mantiki ya give and in ‘negotiations’.

Japo Mbowe alikuwa a minority kwenye msimamo wa chama kuhusu maridhiano but he was right.

Negotiation lazima ujue who has the upper hand na uende nae vipi. Akili za hakina Lissu ni demands ambazo CCM isingeweza pokea kirahisi kama Lissu na matahaaira wenzake wa club house yalivyo kuwa yanamtia (upepo); msimamo wa Mbowe ulikuwa sahihi.

Lissu hana mikakati zaidi ya akili ya social disobedience tu, wakati he is not the demagogue he think he is.

Mbowe aongezewe muda, siasa azitaki pupa za Lissu.
 
Heshima unaijenga na kuibomoa mwenyewe. Unadhani "wanaokejeli" hawana sababu? Isitoshe wanaeleza sababu, hata hivyo ukweli mmekuwa mkiita kejeli
mf mimi sina personal interest na Kiasi na wala simjui zaidi ya kumuona kwenye TV na mitandao tu.

Lakini common sense inaniambia Mbowe anatakiwa kupumzika aachie wengine wenye maono zaidi yake
 
Dj Mbowe atasema tu; amekaliwa kooni haswaa. Watu wake wakaribu wamtafutie Dr wa BP na kisukari yasije kujitokeza mengine
 
Juu ya yote uliyoyasema, haya kayataka mwenyewe. Msiba wa kujitakia hauna kilio.

Hadi sasa siamini kama Mbowe amefikia hatua hii kwa maisha yake aliyoyatumia kupigania Demokrasia, amejidhalilisha sana kuendelea kung’ang’ania Uwenyekiti.
 
Lissu hatoshi, Mbowe ana hekima.

Huu mahala wake aandae mrithi sasa.

Huwezi kuwaachia chama wenye siasa za ‘demagogue’ na hawajui mantiki ya give and in ‘negotiations’.

Japo Mbowe alikuwa a minority kwenye msimamo wa chama kuhusu maridhiano but he was right.

Negotiation lazima ujue who has the upper hand na uende nae vipi; akili za hakina Lissu ni demands ambazo CCM isingeweza pokea kirahisi kama Lissu na matahaaira ya club ya yalivyo mjaza (upepo).

Lissu hana mikakati zaidi ya akili ya social disobedience tu, wakati he is not the demagogue he think he is.

Mbowe aongezewe muda, siasa azitaki pupa za Lissu.
Hekima kuacha vijana wako wanachezea rungu za ugoko halafu yeye anagonga glass na CCM? Wacha hiyo mineno wewe. Hapo hekima ipo wapi?
 
Lissu hatoshi, Mbowe ana hekima.

Huu mahala wake aandae mrithi sasa.

Huwezi kuwaachia chama wenye siasa za ‘demagogue’ na hawajui mantiki ya give and in ‘negotiations’.

Japo Mbowe alikuwa a minority kwenye msimamo wa chama kuhusu maridhiano but he was right.

Negotiation lazima ujue who has the upper hand na uende nae vipi; akili za hakina Lissu ni demands ambazo CCM isingeweza pokea kirahisi kama Lissu na matahaaira ya club ya yalivyo mjaza (upepo).

Lissu hana mikakati zaidi ya akili ya social disobedience tu, wakati he is not the demagogue he think he is.

Mbowe aongezewe muda, siasa azitaki pupa za Lissu.
How is that maridhiano working? Chadema wamepata faida yoyote?
 
Umeeleza vizuri sana. Jambo la muhimu kwa Mbowe ni kusoma alama za nyakati. Akishindana na wakati yale yote mazuri aliyofanya atayaharibu kwa mikono yake mwenyewe. Wanachadema wanataka mabadiliko,wanaona kwa sasa Mbowe hana uwezo tena kuwafikisha pale wanapotaka kufika,wamemchoka,awape kile wanachotaka,mabadiliko. Bado anayo nafasi ya kuendelea kukitumikia cha akiwa kama mjumbe wa kudumu wa CC. Muamar Ghadaf alifanya mengi kwa Walibya lakini kwa kung'ang'ania madarakani angalia alivyoumaliza mwendo kwa fedheha kubwa. Hao wapambe wanaomshauri aendelee wanafanya hivyo kwa manufaa ya matumbo yao. Hao wajumbe 1200 wanaweza kumchagua tena lakini jaaribu kusikiliza sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.
 
How is that maridhiano working? Chadema wamepata faida yoyote?
Lissu hataki maradhiano, yeye ana unyielding demands.

Huo sasa ni utoto kuendekezwa, maridhiano ni give and take (Mbowe kaelezea kwa kina).

Anachotaka Lissu at whim na ilo aliwezekani kwa CCM tu, bali popote kwengine duniani mambo sio rahisi hivyo.
 
Lissu hataki marafhiano ana unyielding demands.

Huo sasa ni utoto kuendekezwa, maridhiano ni give and take (Mbowe kaelezea kwa kina).

Anachotaka Lissu at whim sio CCM tu, popote kwengine duniani haiwezekani kirahisi hivyo.
Mbowe amekuwa aki komaa na hayo maridhiano for a while now, yes mamybe lissu is so aggresive but naangali outcomes za maridhiano, chadema wame achieve nini kutoka kwneye hayo maridhiano?
 
Hivi unajua kwanini marais wengi wa Afrika ambao walipigania uhuru baada ya ya uhuru walikuwa hawataki kuachia madaraka? Ni kwa sababu akili zao na mawazo yao ni kama ya Mbowe na mnaomuunga mkono. Mnaona yuko entitled kuwa pale maisha, yani ni kama vile chama ni cha kwake.
Ndiyo maana hata wakina Mugabe walikuwa wanaona kuachia madaraka haiwezekani maana ni kama vile wanayaacha kwa watu wengine ambao ni wakuja wakati wao ndiyo waliopigania uhuru.
Ni jambo la busara na la maana knowing when to quit.
Ukifanya jambo jema, jua ni muda gani wa kuquit otherwise binadamu wana tabia ya kusahau mazuri yote ukianza kuwaboa.
Utakuwa haujasoma hilo andiko uliloljibu
 
Mbowe amekuwa aki komaa na hayo maridhiano for a while now, yes mamybe lissu is so aggresive but naangali outcomes za maridhiano, chadema wame achieve nini kutoka kwneye hayo maridhiano?
Ukiangalia kilichofanyika kwenye uchafuzi wa serikali za mitaa eti CCM imepata ushindi wa 99% upuuzi mtupu,mnafanya maridhiano ya kishikaji na kuacha mambo muhimu sana ya kubadili mifumo ya uchaguzi, hivi unafikiri kitakachotokea October 2025 kitakuwa na tofauti na kilichofanyika October 2020 na November 2024 sasa kwa mazingira kama haya kuna haja gani ya kufanya siasa katika nchi hii? Ni upuuzi kuingia kwenye uchaguzi chini ya sheria na kanuni za kipumbavu kama hizi.
 
Mbowe amekuwa aki komaa na hayo maridhiano for a while now, yes mamybe lissu is so aggresive but naangali outcomes za maridhiano, chadema wame achieve nini kutoka kwneye hayo maridhiano?
Msikilize Lissu yale anayoita haki zao, kwa CCM ni maridhiano.

Anza na kesi ya Mbowe iliyompeleka gerezani.
 
Ukiangalia kilichofanyika kwenye uchafuzi wa serikali za mitaa eti CCM imepata ushindi wa 99% upuuzi mtupu,mnafanya maridhiano ya kishikaji na kuacha mambo muhimu sana ya kubadili mifumo ya uchaguzi, hivi unafikiri kitakachotokea October 2025 kitakuwa na tofauti na kilichofanyika October 2020 na November 2024 sasa kwa mazingira kama haya kuna haja gani ya kufanya siasa katika nchi hii? Ni upuuzi kuingia kwenye uchaguzi chini ya sheria na kanuni za kipumbavu kama hizi.
Is why sometimes naona maridhiano ni hoax, huwez ku make deal with devil halaf ukadhani ata play fair, haiwezekani
 
Back
Top Bottom