MBOWE na ZITTO kwanini wameamua kuziacha hoja za wananchi mikutano ya hadhara

MBOWE na ZITTO kwanini wameamua kuziacha hoja za wananchi mikutano ya hadhara

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
MBOWE NA ZITTO KWANINI WAMEAMUA KUZIACHA HOJA ZA WANANCHI MIKUTANO YA HADHARA

Nimefuatilia mikutano ya hadhara ya Chadema na ACT Wazalendo sijawasikia Mbowe wala Zitto wakizungumzia au wakipaza sauti zao juu ya mambo makubwa yanayolalamikiwa na wananchi.

Mfano suala ulinzi wa rasilimali za Taifa, utoroshaji wa Madini na mambo ya Makinikia, suala la kushamiri kwa Ujangili wa wanyama pori, kushamiri kwa Uvuvi Haramu mpaka ndege zilizokuaa zinatua Mwanza na kupeleka samaki Ulaya haziji tena kwa kukosa samaki.

suala la ubadhirifu wa mali za umma na ufisadi, kushuka nidhamu kazini kwa watumishi wa umma, sintofahamu wanazokumbana nazo machinga, mama ntilie, wachimbaji wadogo wa Madini, Wavuvi, mauaji ya wakulima na wafugaji, Mifugo kupigwa risasi.

utoaji hafifu wa huduma za afya na malalamiko ya wananchi kukosa dawa baadhi ya hospitalini.

Umeme kukatika hovyo watu kupoteza ajira zinazotegemea umeme, mikataba yenye mashaka inayopigiwa kelele ya SGR Tabora Kigoma, gharama za ukarabati wa Kivuko cha MV Magogoni Bilioni 7.5.

Tanzania kuagiza mchele kutoka nje ikiwa tunayo Ardhi ya kutosha ya kulima mpunga, mgogoro wa ruzuku ya mbolea, usimamizi duni wa miradi ya madarasa na vituo vya afya maeneo mbalimbali nchini ambayo imetumia fedha nyingi za umma na maeneo mbalimbali.

Lakini jambo la kusikitisha maeneo yote ambayo Wananchi ndio wanalalamikia sana wao Mbowe na Zitto wameyaacha kabisa kuyazungumzia wala kutoa ushauri kwa Serikali.

Badala yake mikutano yao imebeba maudhui makubwa ya kuwaeleza watanzania juu ya ubaya wa Serikali ya awamu ya tano.

Nini kimesababisha Mbowe na Zitto wameyaacha mambo yanayolalamikiwa na wananchi kwa sasa na kujikita kutuelezea ubaya wa Serikali ya Magufuli ambayo wote tulikuwepo tangu anaapishwa Novemba 2015 hadi anafariki dunia Machi 17, 2021.
 
nimejiuliza sana mimi hilo swali nimekosa jibu... au hoja za wananchi sio ajenda tena za vyama vya upinzani
 
MBOWE NA ZITTO KWANINI WAMEAMUA KUZIACHA HOJA ZA WANANCHI MIKUTANO YA HADHARA

Nimefuatilia mikutano ya hadhara ya Chadema na ACT Wazalendo sijawasikia Mbowe wala Zitto wakizungumzia au wakipaza sauti zao juu ya mambo makubwa yanayolalamikiwa na wananchi.

Mfano suala ulinzi wa rasilimali za Taifa, utoroshaji wa Madini na mambo ya Makinikia, suala la kushamiri kwa Ujangili wa wanyama pori, kushamiri kwa Uvuvi Haramu mpaka ndege zilizokuaa zinatua Mwanza na kupeleka samaki Ulaya haziji tena kwa kukosa samaki.

suala la ubadhirifu wa mali za umma na ufisadi, kushuka nidhamu kazini kwa watumishi wa umma, sintofahamu wanazokumbana nazo machinga, mama ntilie, wachimbaji wadogo wa Madini, Wavuvi, mauaji ya wakulima na wafugaji, Mifugo kupigwa risasi.

utoaji hafifu wa huduma za afya na malalamiko ya wananchi kukosa dawa baadhi ya hospitalini.

Umeme kukatika hovyo watu kupoteza ajira zinazotegemea umeme, mikataba yenye mashaka inayopigiwa kelele ya SGR Tabora Kigoma, gharama za ukarabati wa Kivuko cha MV Magogoni Bilioni 7.5.

Tanzania kuagiza mchele kutoka nje ikiwa tunayo Ardhi ya kutosha ya kulima mpunga, mgogoro wa ruzuku ya mbolea, usimamizi duni wa miradi ya madarasa na vituo vya afya maeneo mbalimbali nchini ambayo imetumia fedha nyingi za umma na maeneo mbalimbali.

Lakini jambo la kusikitisha maeneo yote ambayo Wananchi ndio wanalalamikia sana wao Mbowe na Zitto wameyaacha kabisa kuyazungumzia wala kutoa ushauri kwa Serikali.

Badala yake mikutano yao imebeba maudhui makubwa ya kuwaeleza watanzania juu ya ubaya wa Serikali ya awamu ya tano.

Nini kimesababisha Mbowe na Zitto wameyaacha mambo yanayolalamikiwa na wananchi kwa sasa na kujikita kutuelezea ubaya wa Serikali ya Magufuli ambayo wote tulikuwepo tangu anaapishwa Novemba 2015 hadi anafariki dunia Machi 17, 2021.
Zito ni kijana wa mbowe na ameandaliwa na mbowe so mbowe ndio akili ya zito wote wanapigania matumbo yao wote wapo kimaslahi

USSR
 
Zito ni kijana wa mbowe na ameandaliwa na mbowe so mbowe ndio akili ya zito wote wanapigania matumbo yao wote wapo kimaslahi

USSR
Wananchi wameshawafungashia virago hawawahitaji tena mikutano yao yote imefeli pakubwa sana kwa sababu ya undumilakuwili
 
Mboe na Zitto mliwanyima ubunge!
Hawawajibiki 'kisheria' kuzungumzia matatizo ya wananchi.
Wadhifa wao unawaruhusu kuzungumzia siasa.
Kuna wabunge takriban 400 wanapaswa kuzungumzia hizo hoja/ matatizo uliyo yaibua.
Hiyo sio kazi ya Zitto wala Mboe wala yeyote ambaye hajachaguliwa.
Wakifanya hivyo, wanafanya kwa kujitolea ila sio wajibu wao.
 
Uhuru wao una vishinikizi.

Ni nani anayefaidika na
mikutano yao imebeba maudhui makubwa ya kuwaeleza watanzania juu ya ubaya wa Serikali ya awamu ya tano.
Tusubiri wakisamehewa, Tusubiri wakiweza kuchagiza na Kupata Katiba.

Ndio tutajua hatujui

Kuna chaka kubwa, tutaona mazingaombwe ambayo kiuhalisia, hayaonekani lakini yanaonekana.
 
Yaani imefikia hatua ni kana kwamba wamepewa fedha ili waanze kampeni mapema, kuipigia kampeni serikali iliyoko madarakani na kumchafua JPM. Lakini naona wananchi walio wengi na wanaojitambua, bado wanakumbuka mazuri aliyoyafanya. Ndiyo maana kila akisimangwa, wengi huingiwa na simanzi!
 
Back
Top Bottom