Mbowe: Nilifuatwa na Maaskofu Watatu na Mufti Gerezani, wakaniambia Serikali inataka kufuta KESI Yako Rais ameomba aonane na Wewe. Mimi ningekataaje?

Kama ikitokea Mbowe akashinda naomba kwenye maskio yangu nisiskie swala la ccm kuiba kura na mambo ya vyama nitakua sitaki tena kwenye maisha yangu yaliobakia hapa kwenye sayari ya Dunia.
Ndio kinasubiriwa kife
 
Lissu hajawahi kuishi gerezani hata nusu saa.
Kwa hiyo, hajui machungu ya gerezani.
Leo Slaa kadakwa usiku,Lissu ,kakimbia hajulikani aliko,sebuse gerezani?
Kwani kuishi gerezani ni sifa au lazima? Huyo Lissu unayesema kakimbia na hajulikani alipo mbona alikuwepo kwenye kikao cha kamati kuu? Inaonyesha unapenda sana kujitekenya na usipocheka unaomba wenzako wakutekenye!
 
Utetezi wa kijeuli huo, Rais hawezi kumuomba Mbowe waonane, Mbowe alikua na uwezo wa kuleta athari gani kwa Rais mpaka amuombe waongee?
 
Utetezi wa kijeuli huo, Rais hawezi kumuomba Mbowe waonane, Mbowe alikua na uwezo wa kuleta athari gani kwa Rais mpaka amuombe waongee?
Kwa nini mtuhumiwa aliyekuwa gerezani aibukie ikulu kwa rais badala ya mahakamani aanze kujitetea?
 
Maaskofu wana ushawishi mkubwa sana kila mahali duniani na isitoshe Mbowe ni Mkristo safi.
Hakuna alie kataa ila mmoja anatosha hakuna haja ya kuchukua kundi kubwa wakati wote ni wafuasi wa Yesu pamoja na Mbowe
 
Kwa nini mtuhumiwa aliyekuwa gerezani aibukie ikulu kwa rais badala ya mahakamani aanze kujitetea?
Naamini yeye ndiye aliomba kuonana na Rais, ndio maana kuna yale tunaambiwa sasa ilifika wakati akaanza kuambia wenzake si lazima wajue kila kitu anachoongea na Rais
 
Naamini yeye ndiye aliomba kuonana na Rais, ndio maana kuna yale tunaambiwa sasa ilifika wakati akaanza kuambia wenzake si lazima wajue kila kitu anachoongea na Rais
Ruhusu akili yako ifanye kazi kidogo, mtuhumiwa wa ugaidi, tena ametangazwa hadi na BBC kwenye mahojiano ya rais. Alikuwa anatakiwa asubuhi hiyo akaanze kujitetea, badala yake anaibukia ikulu.

Gaidi anamuomba rais aliyemtangaza BBC kuwa gaidi. Kisha rais anakubali kukutana na gaidi ikulu baada ya kuombwa na mtuhumiwa wa ugaidi. Does it makes sense to you? Kama hutaki kutumia kichwa kufikiria shauri yako tuache sisi tutumie, tunakubali mtuhumiwa wa ugaidi kaomba kuonana na rais
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…