Mbowe: Watanzania ni Wavivu na Waoga. Wanataka kila kitu afanye Tundu Lissu au Mbowe, hatutafika kwa utaratibu huu!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mwenyekiti wa Chadema mh Mbowe amesema Watanzania ni Wavivu wanategemea kila kitu afanye Tundu Lisu na Mbowe

Kwa utaratibu huu hata Katiba mpya itakuwa ngumu kuupata, amesema

Wananchi ni lazima mtumie WINGI wenu kuibana Serikali itekeleze matarajio yenu vinginevyo mtaendelea Kuwa Walalamikaji wa kudumu, amesisitiza Mbowe katika mkutano wa hadhara Temeke
 

Tofauti na chama cha mambuzi huku kwingine uchawa ni machukizo.

https://www.jamiiforums.com/threads...f-mtikila-julius-malema-au-kina-tutu.2013213/

Wengi tunatofautiana na hoja hiyo ya Mwenyekiti Mbowe.

Ikumbukwe kutofautiana si dhambi maana hata watoto mapacha hutokea mahali wakashindwa kuelewana.

https://www.jamiiforums.com/threads/tathmini-yakinifu-uzinduzi-wa-mikutano-ya-siasa-mwanza.2058702/

Kutofautiana ni jambo la afya tu.

Ninakazia:

"Harakati huongozwa, haziwezi kuja (spontaneously) kama mvua.

Kadamnasi lisililokuwa na viongozi thabiti ni sawa na kundi la kondoo bila Mchungaji."
 
Amehisi asali ya lissu ilifika ubeligiji ikiwa ya baridi hakulamba vizuri yeye ni kutema cheche. Anahofu yeye na hotuba yake ya kule mwanza ilikua hovyo hovyo
 
Wewe humuamini Tundu Lisu
 
Huo uoga ulijengwa kwa mda mrefu, kuanzia enzi za Nyerere, siasa za ujamaa zilileta hofu sanaa kwa wana nchi, na elimu duni hi inapotoshwa sanaa wa tanzania pamoja na umasikini, huo uoga ndo mtaji mkubwa wa CCM, bila huo uoga CCM haiwezi kurudi madarakani .
 
Wewe humuamini Tundu Lisu

Wapi nimesema simuamini Tundu Lissu? Vipi huyo ndiyo anawapeleka puta? Umeona wapi Lissu anasema watanzania ni waoga?

Zingatia aliyesema hayo ni Mwenyekiti Mbowe Wala si Lissu nami nimesema:

https://www.jamiiforums.com/threads...f-mtikila-julius-malema-au-kina-tutu.2013213/

"Harakati huongozwa, haziwezi kuja (spontaneously) kama mvua."

"Kadamnasi lisililokuwa na viongozi thabiti ni sawa na kundi la kondoo bila Mchungaji."

Hayo si leo wala jana
 
Huyu huyu Tundu Lisu ambaye akiona polisi anakimbilia Ubalozi wa Ujerumani?
 
Ukitegemea mabadiliko ya haraka ya siasa kutoka kwa wa Tanzania hapo utakua umebugi, Mbowe alifungwa miezi 9 jela ila watanzania waliendelea na maisha yao ya kawaida bila hata mgomo wa aina yoyote, kwahiyo watanzania wamesha mfanya akate tamaa kabisa hawezi kuwapigania tena. Na umri wake umeenda, kubali au kataa mbowe kabla ya kuenda Jela sio yule Mbowe wa baada ya Jela kajifunza mengi sana amekua na mtazamo mpya.
 
Huyu huyu Tundu Lisu ambaye akiona polisi anakimbilia Ubalozi wa Ujerumani?
Inaonesha mlipokosa kumwua kwa mara nyingine alivyokimbilia ubalozi wa ujerumani baada ya dodoma mngali na lenu jambo. Beberu anawaona.

Kwetu Lissu ni aina za akina Tutu, Nyerere, Mandela, Malema, Maalimu Seif nk (tuliowakosa sana) kama walivyoangaziwa hapa:

https://www.jamiiforums.com/threads...f-mtikila-julius-malema-au-kina-tutu.2013213/

Peleka habari - Lissu akituita hata leo, tunamwagika barabarani.

Habari ndiyo hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…