Mbulu: Wanusurika kuuawa na gari lao kuteketezwa baada ya kudhaniwa ni watekaji wa watoto

Mbulu: Wanusurika kuuawa na gari lao kuteketezwa baada ya kudhaniwa ni watekaji wa watoto


Watu wanne wamenusurika kifo baada ya kupigwa na kukatwa mapanga pamoja na gari waliyokuwa wakiitumia aina ya Raum kuchomwa moto katika Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara kwa kudhaniwa kuwa ni wezi wa kuiba Watoto baada ya kumpa pipi Mtoto aliyekuwa akipita pembeni ya gari yao waliyokuwa wanaitumia.

Neema Kilai ambaye alikuwa kwenye gari hiyo amesema kuwa walikuwa wakitoka kwenye harusi katika kijiji cha Kidarafa katika shughuli ya kupika ambapo gari yao ilipata pancha ghafla waliona gari yao ikiwa imezungukwa na walipofika pale waliambiwa kuwa wao ndio wanahusika kuwakata Watoto viungo.

Amesema kuwa Wananchi hao wakiongozwa na baadhi ya Viongozi walianza kuwashambulia kwa mapanga na mawe na kisha baadaye kuanza kuichoma gari hiyo.

“Kwenye gari tulikuwa tumebeba mahindi, jogoo wawili tumepewa, kuna njiwa, kuna begi zetu na nyama, pipi zilikuwa za kwetu tulikuwa tumenunua tunatafuna, Mtoto alivyopita akatuona tunakula yule rasta akampa kidogo Mama yake akatokea akawa anamchapa yule Mtoto yule wifi wangu akauliza mbona unamchapa Mtoto hivyo?akamuambia haikuhusu wakaanza kuongezeka, walituambia tuvue nguo zote ila Kaka yangu akasema kuliko nivue bora mniue”—— Neema

Watu wawili kati ya wanne wametibiwa katika Hospitali ya Meru lakini wengine wawili ambao ni Mke na Mume wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC kutokana na hali zao kuwa mbaya.

Chanzo: Millard Ayo

Pia soma
Somo kwa the so called wasiojulikana. Hivyo ndivyo wanavyotakiwa kufanyiwa
 
Pole yao lakini hao jamaa wajinga sana. Unaanzaje kumpa mtoto wa mtu pipi huku humjui wala hakujui? Wacha wapigwe tu.
Mimi hapa hata lifti tu kwenye baiskeli yangu ya swala hupati kama sikujui japo nitakuhurumia tu kwa kutembea.
 
Wao ni watu wa catering hao njiwa kuku na mahindi wakiokuwa kwenye gari wa kazi gani?

Polisi iwachunguze hao majeruhi kuna ukakasi hapo
Mi sijaelewa, kuku na mahindi kwenye gari wa kazi gani?

Kwenye gari ilitakiwa wakutwe na nini? Kondom?
 
Serikali isipokua serious kutoa elimu kwa wananchi wetu tutaendelea kuwa na raia bogus milele
 
Sometimes kujichukulia sheria mkononi ni ushamba
Yees; But Sometimes ni ujasiri pia. Kama anayetakiwa kuilinda Sheria iliyopo anazembea, basi huna budi wewe ujichukulie hiyo Sheria mkononi mwako. Mazungumzo ni baadaye.
 
Sure mimi napendekeze wananchi wawe makini na watu wa design kama hao maana moyo wa mtu ni kichaka ,kihalisia haiwezekani umpe mtoto pipi ambaye hata haumjui.

Maisha yamebadilika hata kama mtu unamdai pesa jitahidi umpigie simu na si kumfuata kwake au sehemu na kuanza kumdai maana akiita tu mwizi umekwisha.

Kwa vijana kwenda kwenye maghetto au hostel kwa madada bila appointment nayo ni hatari sana ,ukimfuma na sponsor lazima akuitie mwizi.
Kumpa mtoto pipi isn't a big deal.
Mbona mie kuna muda nakula chakula na watoto siwajui??
Muda mwingine kujichukulia sheria mkononi ni ushamba.
Je uchunguzi ukifanyika na ikagundulika hao watu hawana makosa??
Mtawafidia kwa namna gani??
Je mmoja wapo angepoteza maisha??
Mngemfidiaje??
Kama wao wangekua wana shauku wangewakamata na kuwafikisha mikono ya sheria na taratibu zingine zinafuata.
Yani mimi ndio niwe muhanga ndugu yangu kaumizwa na hana hatia kisa eti umachale wa wanakijiji!!😂😂😂😂
Nitaanza na mwenyekiti aliyewaongoza kuyaondoa maisha yake pasi na kupepesa jicho.
 
Sio ushamba , jaribu kufikiria watoto wanatekwa Kila Leo na polisi analeta masihara kwann usiingie field mwenyewe.
Je kama waliodhurika hawana hatia?
Utawafidiaje?
Sio tu ushamba ni usenge kabisa.
Kama wao walikua na mashaka nao kwanini wasingewakamata na kuwafikisha kituoni kwa uchunguzi zaidi!??
 

Watu wanne wamenusurika kifo baada ya kupigwa na kukatwa mapanga pamoja na gari waliyokuwa wakiitumia aina ya Raum kuchomwa moto katika Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara kwa kudhaniwa kuwa ni wezi wa kuiba Watoto baada ya kumpa pipi Mtoto aliyekuwa akipita pembeni ya gari yao waliyokuwa wanaitumia.

Neema Kilai ambaye alikuwa kwenye gari hiyo amesema kuwa walikuwa wakitoka kwenye harusi katika kijiji cha Kidarafa katika shughuli ya kupika ambapo gari yao ilipata pancha ghafla waliona gari yao ikiwa imezungukwa na walipofika pale waliambiwa kuwa wao ndio wanahusika kuwakata Watoto viungo.

Amesema kuwa Wananchi hao wakiongozwa na baadhi ya Viongozi walianza kuwashambulia kwa mapanga na mawe na kisha baadaye kuanza kuichoma gari hiyo.

“Kwenye gari tulikuwa tumebeba mahindi, jogoo wawili tumepewa, kuna njiwa, kuna begi zetu na nyama, pipi zilikuwa za kwetu tulikuwa tumenunua tunatafuna, Mtoto alivyopita akatuona tunakula yule rasta akampa kidogo Mama yake akatokea akawa anamchapa yule Mtoto yule wifi wangu akauliza mbona unamchapa Mtoto hivyo?akamuambia haikuhusu wakaanza kuongezeka, walituambia tuvue nguo zote ila Kaka yangu akasema kuliko nivue bora mniue”—— Neema

Watu wawili kati ya wanne wametibiwa katika Hospitali ya Meru lakini wengine wawili ambao ni Mke na Mume wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC kutokana na hali zao kuwa mbaya.

Chanzo: Millard Ayo

Pia soma

Kwa kudhaniwa..

Aina za kina Stroke uhalisia wao umejengwa kwenye kudhania.

Hao ndiyo wanaotuletea hii medali adhimu!

IMG_20240824_065438.jpg
 
Wao ni watu wa catering hao njiwa kuku na mahindi wakiokuwa kwenye gari wa kazi gani?

Polisi iwachunguze hao majeruhi kuna ukakasi hapo
Kipondo na mapanga wamechezea hao watu wa catering,chupuchupu watolewe uhai uwatoke

Ova
 
Tuwe na utaratibu wa kuhoji watu. Wawekeni chini wahojini wametoka wapi kwa nanni na wametoka kufanya nini,wanakwenda wapi wana nini kwenye gari na mnakagua kama ni watu waovu mtawajua tu.

Usiende sehemu ukakuta watu wanapiga nawewe ukapiga tu tue na tabia ya kudadisi vitu kwanza. Tubadilike WATANZANIA!!!
 
Kumpa mtoto pipi isn't a big deal.
Mbona mie kuna muda nakula chakula na watoto siwajui??
Muda mwingine kujichukulia sheria mkononi ni ushamba.
Je uchunguzi ukifanyika na ikagundulika hao watu hawana makosa??
Mtawafidia kwa namna gani??
Je mmoja wapo angepoteza maisha??
Mngemfidiaje??
Kama wao wangekua wana shauku wangewakamata na kuwafikisha mikono ya sheria na taratibu zingine zinafuata.
Yani mimi ndio niwe muhanga ndugu yangu kaumizwa na hana hatia kisa eti umachale wa wanakijiji!!😂😂😂😂
Nitaanza na mwenyekiti aliyewaongoza kuyaondoa maisha yake pasi na kupepesa jicho.
Wameshindwa kufanya uchunguzi kugundua watekwaji walipo sembuse wachunguze hilo?
Dhamana ya kulinda familia zetu sahivi iko mikononi mwetu.

Nawasapoti hao wananchi
 
Pole yao lakini hao jamaa wajinga sana. Unaanzaje kumpa mtoto wa mtu pipi huku humjui wala hakujui? Wacha wapigwe tu.
Mimi hapa hata lifti tu kwenye baiskeli yangu ya swala hupati kama sikujui japo nitakuhurumia tu kwa kutembea.
Kwakua hakukua na ndugu yako sio. Kuwapa watoto vijizawadi umekua utamaduni wa kiungwana wa Watanzania bila kujali ni mwanao ama lah unaweza kua na biskuti pipi bigijii na ukaona watoto wanacheza ukawapa kwa upendo tu isiwe sababu ya mtu kupigwa. Tue na tabia za kuhoji watu kama unaona kua humuamini mhoji very simple.
 
Back
Top Bottom