Mbunge adai SGR itajengwa kwa miaka 81

Mbunge adai SGR itajengwa kwa miaka 81

Hii serikali ya huyu mama sidhani kama itakamilisha hii miradi kama pasipokuwepo na juhudi za dhati, wanatakiwa wajue wapi watapata pesa za kukamilisha, labda wachina waingilie kati wakamilishe then wauendeshe huo mradi kwa miaka kadhaa, kinyume na hapo kazi ipo, hii SGR itatukamua haswa, it's a challenge they must face, no way back, ikibidi marupurupu ya wabunge yafyekelewe mbali na mishahara yao ipunguzwe pesa iende huko.
Staili hii si JPM aliikataa kwenye bandari ya bagamoyo?
 
Plan ya Funding ya huu mradi JK aliishaiweka sawa kabla ya kustaafu, mambo yalikuwa yanaenda vizuri. Kaja huyu JPM kaleta ujuaji wake sasa tunahangaika kutafuta hela, na safari hii kwa sababu project tumeshaianza na Wahisani wanajua kuwa tunashida kwa sababu hatuwezi kuacha tena watatupiga mariba makubwakubwa

Huu mradi mpaka unaisha tutajikuta tunatumia hata 50% more kuliko makadirio ya awali, na hii ni disaster
 
Mmesahau habari za contolnumber JPM atabaki kuwa Rais Bora kwangu Leo hii nalipia baadhi ya huduma nikiwa na imani kuwa nachangia taifa langu sio kile kipindi cha vijesenti watu wanabeba Hela kwenye sandarus na Hakuna maendeleo yoyote taliyofanywa twiga kukwea pipa Mzee nitakukumbuka Sana
Na wewe uwe unajifunza na kufuatilia mambo kwanza, kabla ya kuandika.
Suala la kuwepo malipo ya serikali kimtandao (govenment e-payment) ambayo ndio imezaa hiyo Control number ni mfumo uliofanyiwa utafiti na kupitishwa kutumika kipindi cha Kikwete japokuwa ulianza rasmi kutumika kipindi cha Magufuli. Majaribio yake yote yamefanyika kipindi cha Kikwete.

Ni kama ilivyo mradi wa SGR ulipitishwa kipindi cha Kikwete, hakupatikana mtu wa kuweza kuufadhili kipindi kile, Magufuli akaanza kuujenga na kama utakuja kukamilika kipindi cha mama Samia Suluhu basi haitamaanisha ni mradi wa Mama Samia.

Yote kwa yote, bado wataalamu wanasema bado kuna upotevu mkubwa wa malipo ya serikali kwa njia hiyo ya mtandao, mfumo wake wa kiusalama kimtandao ni hafifu, wajanja wa IT wanaweza kuingilia kirahisi na kupiga pesa. Hivyo unahitaji maboresho ya kimsingi.
 
Mbunge wa Handeni Mjini CCM, Reuben Kwagilwa, ameishauri Wizara ya Fedha na Mipango, waangalie namna ya kufadhili miradi mikubwa kwa mfumo wa dhamana ya miundombinu ‘infrastructure bond’ ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma za wananchi kila siku.

Amesema isipofanya hivyo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa wa SGR utachukua miaka 81 kukamilika kwakuwa mpaka sasa hata kilometa 300 bado hazijakamilika.

Kwagilwa ametoa ushauri huo Ijumaa Aprili 9, 2021 bungeni wakati akichangia mjadala wa mpango wa tatu wa maendeleo wa kitaifa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021/22 - 2025/26,

“Standard Gage Railway tunayoijenga ukijumlisha zile njia tunazotakiwa kujenga ni kilomita 4886 hapo naongelea zile njia tu, siongelei mahala ambapo reli huwa zinapishana. mpaka sasa tumeshajenga kipande kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kilometa 300 na tunaendelea kipande cha Morogoro Makutupora kilometa 422 lakini tuko upande mwingine wa Isaka na Mwanza kilometa kilometa 249

Kwa namna tunavyohudumia mradi huo kama tukiendelea kwa mfumo huo tutajenga kwa miaka 81 kwa nchi nzima ikiwa miaka mitano tumejenga kwa kilameta 300 na kilometa zilizosalia tutazijenga kwa miaka 81 hii katika nchi ambayo inapambana kujenga uchumi kasi hiyo haikubaliki na imegharimu Sh11 trilioni ambazo ni ‘hido investiment’ kwa sababu hatutaanza kutumia leo.,”amesema

Ameongeza “Serikali inatakiwa kujifunza na kuondokana na mfumo wa kizamani wa kufadhili miradi mikubwa kwa sababu inajipa pressure kubwa halafu inashindwa kupeleka huduma za kila siku kwa wananchi wake” amesema

Pole pole mawazo ya.kuturudisha nyuma yanaanza kupenyezwa.Okay,tusubiri,lakini Watanzania wana akili na wanaona.
 
Huo mradi hata ukikamilika hautakaa ulipe boss .. na ndio maana Ndungai alipendekeza PPP waingie ubia na kampuni binafsi kwenye uendeshaji
HEP ni Hydro Electric power
Ooh..I get it. Itafutwe namna be it PPP or any other modality tupate kupona...maana tukichanganya miradi yote iliyoanzishwa halafu iishie hewani jamani...hela yote ambayo imeshazama hapo...?!
 
Mbunge wa Handeni Mjini CCM, Reuben Kwagilwa, ameishauri Wizara ya Fedha na Mipango, waangalie namna ya kufadhili miradi mikubwa kwa mfumo wa dhamana ya miundombinu ‘infrastructure bond’ ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma za wananchi kila siku.

Amesema isipofanya hivyo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa wa SGR utachukua miaka 81 kukamilika kwakuwa mpaka sasa hata kilometa 300 bado hazijakamilika.

Kwagilwa ametoa ushauri huo Ijumaa Aprili 9, 2021 bungeni wakati akichangia mjadala wa mpango wa tatu wa maendeleo wa kitaifa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021/22 - 2025/26,

“Standard Gage Railway tunayoijenga ukijumlisha zile njia tunazotakiwa kujenga ni kilomita 4886 hapo naongelea zile njia tu, siongelei mahala ambapo reli huwa zinapishana. mpaka sasa tumeshajenga kipande kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kilometa 300 na tunaendelea kipande cha Morogoro Makutupora kilometa 422 lakini tuko upande mwingine wa Isaka na Mwanza kilometa kilometa 249

Kwa namna tunavyohudumia mradi huo kama tukiendelea kwa mfumo huo tutajenga kwa miaka 81 kwa nchi nzima ikiwa miaka mitano tumejenga kwa kilameta 300 na kilometa zilizosalia tutazijenga kwa miaka 81 hii katika nchi ambayo inapambana kujenga uchumi kasi hiyo haikubaliki na imegharimu Sh11 trilioni ambazo ni ‘hido investiment’ kwa sababu hatutaanza kutumia leo.,”amesema

Ameongeza “Serikali inatakiwa kujifunza na kuondokana na mfumo wa kizamani wa kufadhili miradi mikubwa kwa sababu inajipa pressure kubwa halafu inashindwa kupeleka huduma za kila siku kwa wananchi wake” amesema.

Chanzo: Mwananchi.
Huyu Mbunge alikuwa wapi wakati Rais Magufuli alipokuwa hai hakumweleza. Wamwache Mrithi wake Mhe. Samia Suluhu Hasani akamiliche miradi aliyoachiwa na Mtanguluzi wake. Acha hofu, hofu ni mbaya sana.
 
Mbunge wa Handeni Mjini CCM, Reuben Kwagilwa, ameishauri Wizara ya Fedha na Mipango, waangalie namna ya kufadhili miradi mikubwa kwa mfumo wa dhamana ya miundombinu ‘infrastructure bond’ ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma za wananchi kila siku.

Amesema isipofanya hivyo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa wa SGR utachukua miaka 81 kukamilika kwakuwa mpaka sasa hata kilometa 300 bado hazijakamilika.

Kwagilwa ametoa ushauri huo Ijumaa Aprili 9, 2021 bungeni wakati akichangia mjadala wa mpango wa tatu wa maendeleo wa kitaifa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021/22 - 2025/26,

“Standard Gage Railway tunayoijenga ukijumlisha zile njia tunazotakiwa kujenga ni kilomita 4886 hapo naongelea zile njia tu, siongelei mahala ambapo reli huwa zinapishana. mpaka sasa tumeshajenga kipande kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kilometa 300 na tunaendelea kipande cha Morogoro Makutupora kilometa 422 lakini tuko upande mwingine wa Isaka na Mwanza kilometa kilometa 249

Kwa namna tunavyohudumia mradi huo kama tukiendelea kwa mfumo huo tutajenga kwa miaka 81 kwa nchi nzima ikiwa miaka mitano tumejenga kwa kilameta 300 na kilometa zilizosalia tutazijenga kwa miaka 81 hii katika nchi ambayo inapambana kujenga uchumi kasi hiyo haikubaliki na imegharimu Sh11 trilioni ambazo ni ‘hido investiment’ kwa sababu hatutaanza kutumia leo.,”amesema

Ameongeza “Serikali inatakiwa kujifunza na kuondokana na mfumo wa kizamani wa kufadhili miradi mikubwa kwa sababu inajipa pressure kubwa halafu inashindwa kupeleka huduma za kila siku kwa wananchi wake” amesema.

Chanzo: Mwananchi.
Itafika sababu mpaka sasa hiyo phase 1 haijakamilika na ni miaka minne sasa tunaelekea wa tano.
 
Back
Top Bottom