Huyo msukuma sababu ana pesa ndio anasakiziwa au?
Juzi juzi alimrusha Mnamibia kuwa mimba yake wanategemea mtoto sasa imekuwa ya nani.
Maisha haya danadana tu
wema ana miaka 24.
Hio 24 toka lini wakati juzi kafanya bethdei....
Hio 24 toka lini wakati juzi kafanya bethdei....
Yani huyu Dada aliemroga kafa,inasikitisha...
atakuwa ni yule zuzu wa geita musukuma....hili jamaa ni lishamba sana na limbukeni wa wanawake
Huyo msukuma sababu ana pesa ndio anasakiziwa au?
Juzi juzi alimrusha Mnamibia kuwa mimba yake wanategemea mtoto sasa imekuwa ya nani.
Maisha haya danadana tu
musukuma hana hela yoyote ni kapuku chokoraa lowasa ndio alikuwa anamuweka mjini
Nadhani kila mmoja anaambiwa "ni wewe tuu baby!"Watu wana moyo jamaniii kupiga kavu kwa bongo muvi ni sawa na kujiweka kitanzi....
Juzi anaomba amani sijui alizani akiwa karibu na Aunt E atafika Ndani ya mjengo. Mara watu wamwache D na familia yake mara uwiii...sasa Mama Tee kuingia Dar krisimasi ikamzingua aaagh akaanza kurusha vijembe tena re kuponda kazi ya D. Yaani ni Maombi anahitaji.
Hahahaa watu walichonga sana jamaniii hii couple ya D na maana tee inasonga,Mungu awaongoze kwakweli,mama swiss najua haamini mpaka kesho kwamba dai harudiiiii
hata kabla hujamaliza kuandika libarua lako reeeeefu mwenzako kashaitoa hiyo mimbaMwandishi wetu:Global Publishers
MJINI bwana! Habari nyingi
huanzia kwenye mikeka, siku hizi
wenyewe wamezimebatiza jina
la ?Ubuyu? ambapo kwa sasa ishu
kubwa inayozagaa mitaani ni
mwigizaji Wema Sepetu ?Madam?
kupachikwa mimba na mbunge
maarufu wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) wa Bunge la 11
(jina kapuni kwa sasa), vyanzo
vinasema. Pitapita ya sikio la Gazeti la
Ijumaa katika Jiji la Dar es Salaam,
hivi karibuni ilikutana na Ubuyu
huo kuwa mwigizaji huyo
amenasa ujauzito wa
mwanasiasa huyo ambaye ni
kijana mwenye utajiri mkubwa
anayetajwa kwa sasa kumiliki
vilivyo penzi la Madam.
KUMBUKUMBU KABLA YA HABARI
Kwa muda mrefu, Wema amekuwa akihaha kusaka mtoto
baada ya kupitia kwenye uhusiano na wanaume tofauti
akiwemo Yusuph Jumbe, Steven Kanumba (marehemu),
Nasibu Abdul ?Diamond? na CK (yule kigogo). Akiwa kwenye uhusiano wa
kimapenzi na wanaume hao kwa
hesabu yake na nyakati tofauti,
mara kadhaa msanii huyo
maarufu amekuwa
akikebehemiwa na mahasimu
wake kuwa ni mgumba jambo
ambalo limekuwa
likimhuzunisha. HABARI KAMILI
Ijumaa baada ya kuzinasa habari
za ujauzito wa msanii huyo,
lilijongea kwenye vyanzo vyake
na kukutana na ushuhuda huu
kutoka kwa rafiki wa karibu wa
Wema ukisema: ?Suala la mimba
sijui lakini Wema na mheshimiwa
wana uhusiano. ?Ukaribu wao ulianza wakati wa
kampeni za uchaguzi mkuu
(Wema alikuwa akimnadi
mgombea urais wa CCM, John
Magufuli), mpaka leo
wanaendelea.? MIMBA KABAAH!
Baada ya chanzo cha karibu na
Wema kutoboa mfereji wa
uhusiano na kuliacha suala la
ujauzito kwenye sintofahamu,
wachapakazi wa Ijumaa
waligeuza masikio yao upande
wa mheshimiwa mbunge ili
kupata ubuyu mwingine ambapo
suala la mimba lilitajwa waziwazi. ?Sitaki kunukuliwa ila mimi
nimemsikia mheshimiwa
akidokeza kuwa Wema ni
mjamzito, kwangu mimi kama
rafiki yake naona ni jambo jema,
hiyo ndiyo kazi ya mwanaume
kaka?hahahahaha!? Mmoja kati
ya marafiki wa mbunge huyo
alisema na kumalizia kwa
kicheko. WEMA NA MBUNGE FULL KICHEKO
Inaelezwa na vyanzo vyetu kuwa
baada Wema na mbunge huyo
kuwa wazazi watarajiwa wote
kwa pamoja wamekuwa na
furaha ya aina yake huku kila
mmoja akimsisitiza mwenzake
kuwa makini ili upepo mbaya
usipite kati yao. Aidha, katika hali inayoashiria
kuwepo kwa kitu cha tofauti
kwa msanii huyo aliyepata kuwa
Miss Tanzania 2006, hivi karibuni
aliandika kwenye akaunti ya
Instagram kuwa anayo sapraizi
ya nguvu kwa mashabiki wake. Baadhi ya wadau wa masuala ya
burudani wamehusisha sapraizi
aliyoitangaza Wema na habari za
ujauzito wake unaotarajiwa
kumaliza kejeli juu yake kuwa
yeye ni sawa na mti usiozaa
kwamba hauna thamani. MBUNGE NI TAJIRI MKUBWA
Mbali na umaarufu wa mbunge
huyo timu ya Ijumaa ilijiridhisha
kuwa mwanasiasa huyo ni tajiri
anayemiliki migodi ya madini na
kufanya biashara mbalimbali
zikiwemo za usafirishaji mizigo
na abiria anazofanya kupitia
magari yake. Kutokana na utajiri huo, habari
zinadai kuwa mbunge huyo
ndiye anayempa jeuri ya fedha
Wema ambayo inamfanya aishi
maisha ya ?nyodo? kama
wasemavyo watoto wa mjini. WEMA, MBUNGE WATAFUTWA
Katika kukamilisha weledi wa
habari, gazeti hili lilimtafuta
mbunge huyo kwa njia ya simu ili
azungumzie ishu hiyo lakini
hakuweza kupatikana hewani
jambo ambalo limechangia kwa
kiasi kikubwa jina lake
kuhifadhiwa. Kwa upande wa Wema naye
hakuweza kupatikana kwa
namba zake za simu sambamba
na ile ambayo chanzo chetu
kilisema ni mpya jambo
linaloifanya habari hii kuwa na
mwendelezo baada ya
kujiridhisha kwa kupata kauli za
pande zote mbili. AUNT ANENA
Kama haitoshi gazeti hili
lilimtafuta shosti wake wa karibu
na Wema, Aunt Ezekiel ili naye
afunguke kidogo juu ya madai ya
ujazito wa rafiki yake ambapo
mahojiano yalikuwa hivi: Ijumaa: Mambo anti?ake?
Aunt: Safi cha umbea wangu,
nipe mpya.
Ijumaa: Naona shosti yako Wema
karudi ili umpe mafunzo ya kulea
mimba, mpe hongera zake,
kushika mimba ya mbunge si
jambo dogo. Aunt: Kwani kakuambia yeye
mwenyewe? Kwanza niko naye
hapa, anasema simu zako
amekuwa anaziona lakini hataki
kupokea.
Baada ya mazungumzo hayo
ilisikika sauti ya Wema ikisema:
?Tena mwambie ni ya miezi 6,
tatizo nini??
hahaaaa! Hapana chezea watu waliokua wakila dona gumuuu, maziwa, samaki, samli, manumbukwa mapigo ya kisukuma ataachaje kushika mimba kwa mfano.?
Sasa si atakua mtoto wa zinaa.aibu mpya.bora mondi kafunga ndoa kimyakimyaMwigizaji Wema Sepetu ‘Madam’.
Mwandishi wetu
MJINI bwana! Habari nyingi huanzia kwenye mikeka, siku hizi wenyewe wamezimebatiza jina la ‘Ubuyu’ ambapo kwa sasa ishu kubwa inayozagaa mitaani ni mwigizaji Wema Sepetu ‘Madam’ kupachikwa mimba na mbunge maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Bunge la 11 (jina kapuni kwa sasa), vyanzo vinasema.
Pitapita ya sikio la Gazeti la Ijumaa katika Jiji la Dar es Salaam, hivi karibuni ilikutana na Ubuyu huo kuwa mwigizaji huyo amenasa ujauzito wa mwanasiasa huyo ambaye ni kijana mwenye utajiri mkubwa anayetajwa kwa sasa kumiliki vilivyo penzi la Madam.
KUMBUKUMBU KABLA YA HABARI
Kwa muda mrefu, Wema amekuwa akihaha kusaka mtoto baada ya kupitia kwenye uhusiano na wanaume tofauti akiwemo Yusuph Jumbe, Steven Kanumba (marehemu), Nasibu Abdul ‘Diamond’ na CK (yule kigogo).
Akiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaume hao kwa hesabu yake na nyakati tofauti, mara kadhaa msanii huyo maarufu amekuwa akikebehemiwa na mahasimu wake kuwa ni mgumba jambo ambalo limekuwa likimhuzunisha.
HABARI KAMILI
Ijumaa baada ya kuzinasa habari za ujauzito wa msanii huyo, lilijongea kwenye vyanzo vyake na kukutana na ushuhuda huu kutoka kwa rafiki wa karibu wa Wema ukisema: “Suala la mimba sijui lakini Wema na mheshimiwa wana uhusiano.
“Ukaribu wao ulianza wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu (Wema alikuwa akimnadi mgombea urais wa CCM, John Magufuli), mpaka leo wanaendelea.”
MIMBA KABAAH!
Baada ya chanzo cha karibu na Wema kutoboa mfereji wa uhusiano na kuliacha suala la ujauzito kwenye sintofahamu, wachapakazi wa Ijumaa waligeuza masikio yao upande wa mheshimiwa mbunge ili kupata ubuyu mwingine ambapo suala la mimba lilitajwa waziwazi.
“Sitaki kunukuliwa ila mimi nimemsikia mheshimiwa akidokeza kuwa Wema ni mjamzito, kwangu mimi kama rafiki yake naona ni jambo jema, hiyo ndiyo kazi ya mwanaume kaka…hahahahaha!” Mmoja kati ya marafiki wa mbunge huyo alisema na kumalizia kwa kicheko.
WEMA NA MBUNGE FULL KICHEKO
Inaelezwa na vyanzo vyetu kuwa baada Wema na mbunge huyo kuwa wazazi watarajiwa wote kwa pamoja wamekuwa na furaha ya aina yake huku kila mmoja akimsisitiza mwenzake kuwa makini ili upepo mbaya usipite kati yao.
Aidha, katika hali inayoashiria kuwepo kwa kitu cha tofauti kwa msanii huyo aliyepata kuwa Miss Tanzania 2006, hivi karibuni aliandika kwenye akaunti ya Instagram kuwa anayo sapraizi ya nguvu kwa mashabiki wake.
Baadhi ya wadau wa masuala ya burudani wamehusisha sapraizi aliyoitangaza Wema na habari za ujauzito wake unaotarajiwa kumaliza kejeli juu yake kuwa yeye ni sawa na mti usiozaa kwamba hauna thamani.
MBUNGE NI TAJIRI MKUBWA
Mbali na umaarufu wa mbunge huyo timu ya Ijumaa ilijiridhisha kuwa mwanasiasa huyo ni tajiri anayemiliki migodi ya madini na kufanya biashara mbalimbali zikiwemo za usafirishaji mizigo na abiria anazofanya kupitia magari yake.
Kutokana na utajiri huo, habari zinadai kuwa mbunge huyo ndiye anayempa jeuri ya fedha Wema ambayo inamfanya aishi maisha ya ‘nyodo’ kama wasemavyo watoto wa mjini.
WEMA, MBUNGE WATAFUTWA
Katika kukamilisha weledi wa habari, gazeti hili lilimtafuta mbunge huyo kwa njia ya simu ili azungumzie ishu hiyo lakini hakuweza kupatikana hewani jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa jina lake kuhifadhiwa.
Kwa upande wa Wema naye hakuweza kupatikana kwa namba zake za simu sambamba na ile ambayo chanzo chetu kilisema ni mpya jambo linaloifanya habari hii kuwa na mwendelezo baada ya kujiridhisha kwa kupata kauli za pande zote mbili.
AUNT ANENA
Kama haitoshi gazeti hili lilimtafuta shosti wake wa karibu na Wema, Aunt Ezekiel ili naye afunguke kidogo juu ya madai ya ujazito wa rafiki yake ambapo mahojiano yalikuwa hivi:
Ijumaa: Mambo anti’ake?
Aunt: Safi cha umbea wangu, nipe mpya.
Ijumaa: Naona shosti yako Wema karudi ili umpe mafunzo ya kulea mimba, mpe hongera zake, kushika mimba ya mbunge si jambo dogo.
Aunt: Kwani kakuambia yeye mwenyewe? Kwanza niko naye hapa, anasema simu zako amekuwa anaziona lakini hataki kupokea.
Baada ya mazungumzo hayo ilisikika sauti ya Wema ikisema: “Tena mwambie ni ya miezi 6, tatizo nini?”
Chanzo: GPL
Hahahaa my dear,yani huko Insta nimekuta tag nyingi nikasema leo kuna moto huku,huyu madam si tunaambiwa ana mambo ya kizungu mbona kawa mswahili na vijembe anavyotoa sasa....Anarusha haya jana na leo sijui kawaje na Dee anamchoma roho hadi anabaki kumtafuta tafuta leo huko insta
View attachment 313373
View attachment 313375
Na hii kwa Eeeeeeh, kweli mk.u.ni wa Dee anauota hadi basi na picha ya nisi wa Dee juu leo na maneno kibao.
Krisimasi inayowasha ndio hii
View attachment 313376