Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Hamis Taletale ametimiza ahadi yake kwa Wananchi wa kata ya Ngerengare baada ya kufanikisha kupatiwa huduma ya maji baridi ambapo jumla ya matanki matatu yametolewa na Serikali kusambaza maji katika Vijiji viwili vya Mgude na Ngerengere.
Kwanzia sasa Vijiji hivyo vinapokea huduma ya maji baridi kutoka katika chanzo cha Wami Ruvu kupitia Mamlaka ya Majisafi na usafi wa mazingira Dar Es Salaam, DAWASA kwa kushirikiana na Wakala wa Majisafi na usafi wa mazingira vijijini, RUWASA.
“Awali tulikua tunapata shida sana, maji ya chumvi, nguo zinachakaa, Maharagwe hayawivi, Chai mbaya lakini kwa sasa hivi tunajisikia raha tu, Chai tamu sana, Maharagwe yanakwiva na tunakunywa tunastarehe.” amesema mmoja wa Wananchi walionufaika na mradi huo.
Miongoni mwa wabunge mabunju huyu jamaa sijui ilikuaje yani hata ile misimamo ya kisiasa hana ,huyu jamaa akiongea unaweza kutamani kuziba masikio kama haitoshi mwananchi wake kafurahi nae eti maharage yataiva🤣🤣🤣