Mbunge Jaguar kujipeleka polisi - hivi mbona Watanzania ndio wamecharuka sana japo wengine walitajwa

Mbunge Jaguar kujipeleka polisi - hivi mbona Watanzania ndio wamecharuka sana japo wengine walitajwa

na w

Na wewe sijui umeishakula mirungi? kinachoongelewa hapa ni raia walioingia nchi jirani with permit. Hawa ndio unaweza kuwatetea, lakini wanaoingia nchi jirani bila permit, hawa linalowakuta ni wao watajijua.

Watanzania wasiokua na vibali wakianza kukusanywa huku watajaza mkoa mzima, tunaishi kwa kuvumiliana.....
Msumbiji walikua wanachana vibali vya Watanzania, fuatilia taarifa zote vizuri.
 
Watanzania wasiokua na vibali wakianza kukusanywa huku watajaza mkoa mzima, tunaishi kwa kuvumiliana.....
Msumbiji walikua wanachana vibali vya Watanzania, fuatilia taarifa zote vizuri.
Huku pia wakenya msio na vibali mmejazana sana tu na hatuwagusi hata
 
Kukemea ubaguzi ni hulka ya binadamu yeyote mwenye akili timamu hata kama hauthiriki nao,Makaburu walipingwa hata na Wazungu wenzao wenye akili,Watanzania wana historia ya kukemea ukandamizaji unlike Kenyans na ndio maana wapigania Uhuru wengi walilelewa Tanzania na hata Raila alipewa passport ya Kitanzania kwa mantiki hiyo hiyo
 
Hao Msumbiji mko nao kwenye SADC ambayo huwa mnasema ndio ndugu wenu zaidi, ila huwa hawawataki huko, sisi huku tumeruhusu hadi omba omba wenu wamejaa pembeni mwa barabara zetu na hakuna anayeulizwa kitu. Tazama hii video

Haiingii akilini kuona mtu mwenye akili timamu anatetea ubaguzi na chuki katika jamii eti kwasababu majirani wengine nao walifanya hivyo

binafsi naingia na kutoka kenya kila mara nina marafiki wakenya wanaofanya biashara Tanzania kwa muda mrefu hakuna anayewasumbua hapa Tz na wanatupongeza kwa ukarimu wetu kwao.

Inashangaza kuona kauli za kibaguzi vitisho zinatolewa na kiongozi halafu serikali imekaa kimya maana yake kauli hiyo ina baraka za serikali.
 
Edit: Habari za hivi punde, mbunge Jaguar amekamatwa na polisi https://www.kenyans.co.ke/news/41074-jaguar-arrested-outside-parliament-buildings
-----------------
Muda wowote mbunge Jaguar atajipeleka kwenye kituo cha polisi baada ya uchunguzi kuanza kufanywa ili kubaini sheria ipi alivunja alipotoa matamko ya kuwatishia wageni. Kwa kweli alichokifanya ni mbaya zaidi na anafaa achukuliwe hatua za kisheria, ila nauliza tu, mbona humo alitaja raia wa kutokea mataifa mengine wakiwemo Waganda, lakini wote hao wapo kimya ila kwa Tanzania jana bunge halikua linakalika, mpaka hata waziri mkuu alilazimika kutoa tamko.

Siku zote nilijua Watanzania hawana haja ya kuja Kenya, na kwamba wao husema kwao huko ni nchi ya asali na maziwa. Iweje siku Watanzania walichinjwa Afrika Kusini walipiga kimya, Watanzania mamia wamefurushwa na kuteswa Msumbij hapo jirani wao, pia kimyaaa.... lakini hapa mbunge kwa kunywa gongo/chang'aa yake akabwatuka na kutaja taja wageni wa mataifa tofauti, lakini imeongelewa Bongo yote wamelia sana.

Hii iwe funzo kwa jirani zetu mnaopenda kiburi, sote ni ndugu, tunategemeana kwa njia moja au nyingine, mna desturi ya kuonyesha chuki dhidi ya Wakenya huko kwenu mkijiona kama kwamba nyie ndio kila kitu, lakini mwenye akili kati yenu akaombe takwimu za uhamiaji aone Watanzania wangapi wanakesha wakija huku Kenya.
-------------------------

Developing: Starehe MP Jaguar to present himself at parliament police station over xenophobic remarks. More details to follow on #TheDailyBrief.
D9-NZffX4AAlG5Q.png



Umeshakula mirungi tayar sio bure
 
Kenya hamna lolote la kututisha sisi na mnatutegemea zaidi kuliko tunavyowategemea wanafiki wakubwa ninyi na dhulumati wa mali zetu za EAC
 
jiwe alfurahia kupiga mnada ngombe kule namanga pamoja vifaranga! nasema wachagga wa gikomba walambwe tu nao waliskie joto la jiwe..

View attachment 1138921View attachment 1138922View attachment 1138923
kwa hiyo kama jiwe alipiga mnada ng'ombe zenu mumeona adhabu pekee ni kuwafurusha watz kenya?. akili za kijinga sana hizo.

ila nimefurahi kuona serikali ya kenya ikisema kauli ya jaguar siyo kauli ya serikali ya kenya, ni kauli yake binafsi. wamemuacha afe na zigo lake. [emoji16][emoji16]
 
Haiingii akilini kuona mtu mwenye akili timamu anatetea ubaguzi na chuki katika jamii eti kwasababu majirani wengine nao walifanya hivyo

binafsi naingia na kutoka kenya kila mara nina marafiki wakenya wanaofanya biashara Tanzania kwa muda mrefu hakuna anayewasumbua hapa Tz na wanatupongeza kwa ukarimu wetu kwao.

Inashangaza kuona kauli za kibaguzi vitisho zinatolewa na kiongozi halafu serikali imekaa kimya maana yake kauli hiyo ina baraka za serikali.

Wewe nawe umekurupuka baada ya kuvimbiwa ubwabwa, serikali gani imekaa kimyaa, tangu jana serikali imetoa tamko na kumkana mbunge huyu, pia amekamatwa leo na kuwekwa lock up https://www.kenyans.co.ke/news/41074-jaguar-arrested-outside-parliament-buildings
 
Wewe nawe umekurupuka baada ya kuvimbiwa ubwabwa, serikali gani imekaa kimyaa, tangu jana serikali imetoa tamko na kumkana mbunge huyu, pia amekamatwa leo na kuwekwa lock up https://www.kenyans.co.ke/news/41074-jaguar-arrested-outside-parliament-buildings
Matusi sio suluhisho mkuu, sikulaumu kwasababu nimeshaelewa kiwango cha ustaarabu na uelewa wako.
Naelewa vizuri kinachoendelea

Nilichomaanisha ni kwamba kudelay kwa serikali ya Kenya kuchukua hatua ndio chanzo cha jambo hilo kupewa uzito mkubwa.
 
Hao Msumbiji mko nao kwenye SADC ambayo huwa mnasema ndio ndugu wenu zaidi, ila huwa hawawataki huko, sisi huku tumeruhusu hadi omba omba wenu wamejaa pembeni mwa barabara zetu na hakuna anayeulizwa kitu. Tazama hii video

kuhusu ombaomba huo ni mradi wa wakenya.

wapo wakenya miongoni mwenu wanaofaidika na hao ombaomba.

ndio maana mpaka leo hamjachukua hatua yoyote madhubuti ya kuwakamata na kuwarejesha tz.
 
Juzi Museveni alitangaza kupiga risasi Mfugaji yeyote wa Kenya atakaevuka boda, Wakenya kimyaa, sipati picha kama Jiwe angetoa hilo Tamko.
Tanzania ilipiga mnada Ng’ombe wengi wa Uganda, Kenya na Rwanda, Ng’ombe wa Rwanda na Uganda ndio walikuwa wengi sana ajabu UG na RW walijua wamekosea wakakaa zao Kinya, ila vile Vilio wakenya walilia nahisi hata mzee Kenyatta alisikia huko ahera.
Ni km vile waganda jaguar kawataja lkn jamaa hawaku mind...lkn ccm..weeee...mpka bungeni[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Wewe nawe umekurupuka baada ya kuvimbiwa ubwabwa, serikali gani imekaa kimyaa, tangu jana serikali imetoa tamko na kumkana mbunge huyu, pia amekamatwa leo na kuwekwa lock up https://www.kenyans.co.ke/news/41074-jaguar-arrested-outside-parliament-buildings

Ungekuwa una akili ungejua kuwa tatizo sio kilichoongelewa tu bali ni nani ameongea. Jaguar anajulikana bongo kitambo na juzi tu alikuwa Tanzania, kwa mtu kama yeye kutoa hate speech inashangaza na ukitaka kulijua hili; hata celebrities wa Tanzania wameliongelea pia na si kwa sababu ni KENYA bali limetamkwa na mtu ambaye hawakumtarajia.

Usitafute sababu za ku-play victim. Jamaa kazingua pamoja na hao wakenya waliomshangilia yaani wameonesha dhahiri walivyo xenophobic. Just swallow your Kenyan Ego and pride for once in your life time mkuu
 
Edit: Habari za hivi punde, mbunge Jaguar amekamatwa na polisi https://www.kenyans.co.ke/news/41074-jaguar-arrested-outside-parliament-buildings
-----------------
Muda wowote mbunge Jaguar atajipeleka kwenye kituo cha polisi baada ya uchunguzi kuanza kufanywa ili kubaini sheria ipi alivunja alipotoa matamko ya kuwatishia wageni. Kwa kweli alichokifanya ni mbaya zaidi na anafaa achukuliwe hatua za kisheria, ila nauliza tu, mbona humo alitaja raia wa kutokea mataifa mengine wakiwemo Waganda, lakini wote hao wapo kimya ila kwa Tanzania jana bunge halikua linakalika, mpaka hata waziri mkuu alilazimika kutoa tamko.

Siku zote nilijua Watanzania hawana haja ya kuja Kenya, na kwamba wao husema kwao huko ni nchi ya asali na maziwa. Iweje siku Watanzania walichinjwa Afrika Kusini walipiga kimya, Watanzania mamia wamefurushwa na kuteswa Msumbij hapo jirani wao, pia kimyaaa.... lakini hapa mbunge kwa kunywa gongo/chang'aa yake akabwatuka na kutaja taja wageni wa mataifa tofauti, lakini imeongelewa Bongo yote wamelia sana.

Hii iwe funzo kwa jirani zetu mnaopenda kiburi, sote ni ndugu, tunategemeana kwa njia moja au nyingine, mna desturi ya kuonyesha chuki dhidi ya Wakenya huko kwenu mkijiona kama kwamba nyie ndio kila kitu, lakini mwenye akili kati yenu akaombe takwimu za uhamiaji aone Watanzania wangapi wanakesha wakija huku Kenya.
-------------------------

Developing: Starehe MP Jaguar to present himself at parliament police station over xenophobic remarks. More details to follow on #TheDailyBrief.
D9-NZffX4AAlG5Q.png



Wala hatuna haja ya kuja kenya,kilichotufanya tukomalie ni kwamba tulishapata sababu ya kutimua nyang'au wote walioko TZ,yan ingekua raha sana
 
Tunajua chuki ya wakenya kwa watz. Hivo hao wengine walikuwa wametajwa tu kuzuga ila hapo mlengwa ni mbongo. Ni Kama ilivyo south, wageni wanapigwa lkn mlengwa mkuu ni mnaijeria
 
Back
Top Bottom