Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa, Mhe. Juliana Didas Masaburi katika kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Jijini Dodoma amehoji Wizara ya Nishati kuhusu utekelezaji wa Miradi ya REA III awamu ya Pili Katika Mkoa wa Mara
Maswali yote yalijibiwa na Naibu Waziri Wizara ya Nishati Mhe. Wakili Stephen Byabato na kuelezea mipango na mikakati mbalimbali ya Wizara kuisimamia REA ili kufikisha Umeme kwenye kila Kitongoji
"Je, Ni lini mradi wa Kilomita mbili (02) za nyongeza katika Mradi wa REA III awamu ya pili utaanza kutekelezwa katika Mkoa mzima wa Mara?" - Mhe. Juliana Didas Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa
"Tunatarajia Ijumaa ya Wiki hii REA watakaa na wakandarasi, wameshapewa idhini ya kuendelea na maeneo ya kutekeleza kilomita mbili, wakishasaini Mikataba mwishoni mwa Wiki hii tunatarajia mwanzoni mwa mwezi unaokuja kazi itaanza na mwa kuwa kazi ni ndogo tunatarajia itakamilika pamoja na kazi kubwa mwezi disemba mwaka huu kwasababu ni kupeleka Line ndogo za kuwasha Umeme katika Vijiji vyote ambavyo vilikuwa katika REA III awamu ya pili kwa maana ya kuongeza kilomita mbili kwa kila Kitongoji" - Mhe. Wakili Stephen Byabato, Naibu Waziri Nishati
Maswali yote yalijibiwa na Naibu Waziri Wizara ya Nishati Mhe. Wakili Stephen Byabato na kuelezea mipango na mikakati mbalimbali ya Wizara kuisimamia REA ili kufikisha Umeme kwenye kila Kitongoji
"Je, Ni lini mradi wa Kilomita mbili (02) za nyongeza katika Mradi wa REA III awamu ya pili utaanza kutekelezwa katika Mkoa mzima wa Mara?" - Mhe. Juliana Didas Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa
"Tunatarajia Ijumaa ya Wiki hii REA watakaa na wakandarasi, wameshapewa idhini ya kuendelea na maeneo ya kutekeleza kilomita mbili, wakishasaini Mikataba mwishoni mwa Wiki hii tunatarajia mwanzoni mwa mwezi unaokuja kazi itaanza na mwa kuwa kazi ni ndogo tunatarajia itakamilika pamoja na kazi kubwa mwezi disemba mwaka huu kwasababu ni kupeleka Line ndogo za kuwasha Umeme katika Vijiji vyote ambavyo vilikuwa katika REA III awamu ya pili kwa maana ya kuongeza kilomita mbili kwa kila Kitongoji" - Mhe. Wakili Stephen Byabato, Naibu Waziri Nishati