Mbunge Kwagilwa Nhamanilo: Wananchi Wapo pamoja na Rais Samia

Mbunge Kwagilwa Nhamanilo: Wananchi Wapo pamoja na Rais Samia

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
"Kwenye ziara za Viongozi na matamko ya Viongozi tumekuwa tukiambiwa barabara zitajengwa za Handeni - Kimirashi - Kiteto - Kondoa - Singida. Handeni - Tuliani - Morogoro lakini haikuwahi kutokea. Leo nasimama hapa kuthibitisha kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameleta mkandarasi kampuni ya China 🇨🇳 inafanya kazi usiku na mchana" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Leo inajengwa barabara ya lami kutoka Handeni - Kimirashi - Kiteto - Kondoa - Singida kilomita 434. Inajengwa barabara kutoka Magore - Tuliani - Mziha - Negelo - Kanata - Kwamagome - Kidereko - Handeni Mjini" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Toka mwaka 1961 tangu tunapata Uhuru tumekuwa na Hospitali ya Wilaya ilihali siyo Hospitali ya Wilaya, zaidi ya miaka 50 imechakaa, watu wakienda kutibiwa wananyeshewa. Amekuja Rais Samia Suluhu Hassan ametoa Milioni 900 na anaendelea kutoa Milioni 900 kila mwaka kufanya ukarabati wa Hospitali na kujenga majengo mapya na Kazi Inaendelea sasa hivi" - Mhe. Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Tumeshafumua mabati yote ya zamani, tumepiga mabati mapya. Mwaka huu tuna Milioni 900, sasa hivi tunaendelea na Jengo la Dharura (Emergency) la kisasa, tutajenga majengo mengine 21 kwa kadiri ambavyo Mheshimiwa Rais atazidi kutupatia fedha" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Katika mazingira hayo, Rais wa namna hiyo anatokea mtu anambeza tu. Mbezeni Rais wetu lakini Wananchi wapo pamoja naye Rais Samia Suluhu Hassan" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini.

 
Tutanataka kuona utekelezaji kwa vitendo na sio ahadi zisizotekelezeka tangu Uhuru.

Chisokela suwe [emoji57][emoji57]
 
Handeni Ndiyo Wilaya ilochoka mbaya na yenye mzunguuko Mdogo sana wa pesa kuliko Wilaya zote za mkoa wa Tanga [emoji108]

Ni matumaini yangu kuwa iwapo utekelezaji wa vitendo ukifanyika na miradi hiyo kukamilika itafungua maendeleo ndani ya Wilaya ya Handeni kwa kuwa junction ya kutokea Kilindi na huko Tuliani.

Ngoja tuone isijekuwa hadithi hadithi tu.

Maana ahadi hazijaanza leo [emoji108]
 
Vipi kuhusu tatizo la Maji Handeni mmelipatia ufumbuzi gani?
 
Mie du hisokela Chaka na via ukeva asokele Hana ntulwe nanga nikaule I dibulodoza dikasenga msanga aho ne nimanye kindedi idibarabara dyanga dilwe ilami
 
Kwani mnakwama wapi kutoa Maji Ruvu hapo hata kwa mguu unafika na kusambaza Wilaya ya Handeni yote?

Vino mwatakuona vihi?! [emoji57]
 
"Kwenye ziara za Viongozi na matamko ya Viongozi tumekuwa tukiambiwa barabara zitajengwa za Handeni - Kimirashi - Kiteto - Kondoa - Singida. Handeni - Tuliani - Morogoro lakini haikuwahi kutokea. Leo nasimama hapa kuthibitisha kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameleta mkandarasi kampuni ya China 🇨🇳 inafanya kazi usiku na mchana" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Leo inajengwa barabara ya lami kutoka Handeni - Kimirashi - Kiteto - Kondoa - Singida kilomita 434. Inajengwa barabara kutoka Magore - Tuliani - Mziha - Negelo - Kanata - Kwamagome - Kidereko - Handeni Mjini" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Toka mwaka 1961 tangu tunapata Uhuru tumekuwa na Hospitali ya Wilaya ilihali siyo Hospitali ya Wilaya, zaidi ya miaka 50 imechakaa, watu wakienda kutibiwa wananyeshewa. Amekuja Rais Samia Suluhu Hassan ametoa Milioni 900 na anaendelea kutoa Milioni 900 kila mwaka kufanya ukarabati wa Hospitali na kujenga majengo mapya na Kazi Inaendelea sasa hivi" - Mhe. Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Tumeshafumua mabati yote ya zamani, tumepiga mabati mapya. Mwaka huu tuna Milioni 900, sasa hivi tunaendelea na Jengo la Dharura (Emergency) la kisasa, tutajenga majengo mengine 21 kwa kadiri ambavyo Mheshimiwa Rais atazidi kutupatia fedha" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Katika mazingira hayo, Rais wa namna hiyo anatokea mtu anambeza tu. Mbezeni Rais wetu lakini Wananchi wapo pamoja naye Rais Samia Suluhu Hassan" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini.

View attachment 2728440
Huu uhuni wa CCM wanaotuletea. Yaani kila Rais akibadilika wanakuja na jipya. Wakati wa JPM tulisikia mengi. Leo Maza kaja wanaendelea as if ni new government..... CCM ni ile ile. Miaka 62 sasa. Hatudanganyiki.
 
Back
Top Bottom