Mbunge Luhaga Mpina ndoto yako ya kuwa mbunge maarufu Tanzania imetimia

Alikuwepo Lucas Selelii, Sasa hivi Yuko kalala kwenye makaburi ya kisiasa, na alikuwa na hoja kweli, acha huyo masulupwete
 
Nani ataziba pengo? HAYUPO maana CCM ndio Ina wabunge 95% na wote hao wako pale sababu ya kulinda maslahi ya serikali. Ni kheri tutegemee hata wanaharakati, waandishi wa habari kupaza sauti kwenye matatizo yetu ila sio mbunge wa CCM wanatuchora tu wale maana wametugeuka sana Kila tulipowaamini.
 
Hamna kitu, mbona Mpina wamemkata ujumbe wa NEC mkoa na kitaifa ila hakuna madhara yoyote? Hamna kitu atafanya hata aligombea upinzani wataiba kura na maisha yataendelea. Kwa katiba hii hakuna wa kumchallenge mwenyekiti wa CCM
 
Leo hii ukiulizwa mbunge maarufu Tanzania kwa kujenga hoja zenye mantiki hutakosa kumtaja mbunge Mpina.

Amezichanga karata vizuri akatumia nafasi yake vizuri katika kipindi hichi wala hakuchagua kuketi upande wa walamba asal...
Huyu angekuwa mbunge wa kuteuliwa leo hii tungesikia kapewa ubalozi Zimbabwe.
 

Alipogusia katiba mpya nikamuona wa maana. Namuunga mkono kwenye Hilo.
 
Hamna kitu, mbona Mpina wamemkata ujumbe wa NEC mkoa na kitaifa ila hakuna madhara yoyote?
Kwa sasa yes it's true Mpina hana madhara, lakini 2025, it's not!.
Hamna kitu atafanya hata aligombea upinzani wataiba kura na maisha yataendelea.
Kuna vitu kiongozi mwanaume anaweza kufanya lakini Mwanamke hawezi, Mwanamke hawezi kuwa mwizi!, ni aibu!.
Kwa katiba hii hakuna wa kumchallenge mwenyekiti wa CCM
It's true na sio tuu kumchallenge Mwenyekiti bali Tanzania hatuna upinzani wa kui challenge CCM!.
P
 
Kazi kwako mheshimiwa wa Mbozi, jimbo linataka kukuponyoka hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…