Mbunge Magesa akemea upotoshaji mradi wa maji Chamkolongo

Mbunge Magesa akemea upotoshaji mradi wa maji Chamkolongo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MHANDISI MAGESA AKEMEA UPOTOSHAJI MRADI WA MAJI CHANKOLONGO

Mbunge wa Jimbo la Busanda, Mhandisi Tumaini Magesa amewatoa hofu wananchi wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Katoro juu ya mradi wao wa maji wa Chamkolongo unaondelea kutelekelezwa kwani umefikia hatua za mwisho kumalizika na kupuuza maneno ya watu yalioenezwa kuwa mradi ulianzishwa kukidhi mbio za mwenge peke yake.

Magesa amesema hayo wakati akikabidhi kompyuta mpakato kwa viongozi pamoja na wafanyabiashara wa Katoro ambayo ni moja ya ahadi yake ya mwaka 2021 baada ya kuingia madarakani.

Amesema walichokifanya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Geita (GEUWASA) ni sahihi kitalaamu na kwa mjibu wa mkataba na wala mradi na si kwa ajili ya mbio za mwenge.

"Rais ameendelea kuleta fedha kwenye mradi huu lengo ni kuwa Katoro pawe na maji ya uhakika na salama" Amesema Mhandisi Magesa.

WhatsApp Image 2023-05-02 at 10.05.15(1).jpeg
 
Sawa lakini Geita miaka nenda rudi licha ya kuwa na migodi kadhaa ya dhahabu maji safi na salama majumbani imekuwa tatizo sugu hii ni fedheha kubwa mwekezaji nina hakka anatoa pesa kwa jamaii (CSR) toka kitambo kwanini zisitatue matatizo ya msingi kama upatikanaji wa maji safi na salama miongoni mwa mengi au ndio tuseme midomo mingi ya walaji?
 
Back
Top Bottom