Mbunge Morogoro Awakaribisha Watanzania Wote kwenye Mei Mosi Morogoro

Mbunge Morogoro Awakaribisha Watanzania Wote kwenye Mei Mosi Morogoro

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE MHE. ABOOD ANAWAKARIBISHA WATANZANIA WOTE KATIKA SHEREHE ZA MEI MOSI MOROGORO

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini MHE. DKT. ABDULAZIZ M. ABOOD anawakaribisha Watanzania wote kutoka kila Eneo la Nchi yetu kwa ajili ya Sherehe za Mei Mosi zitakazofanyika tarehe 01.05.2023 Morogoro Mjini kwenye Uwanja wa Jamhuri.

Mhe. Abood anawakaribisha kwa Upendo mkubwa na amesema Morogoro sisi ni wakarimu Sana, mkaribie na mjisikie mpo Nyumbani.

Aidha, Mhe. Abood amesema hata mkimaliza Shughuli za Mei Mosi muendelee kuwepo ili mtembelee Vivutio vya kitalii tulivyonavyo Kama Mlima Uluguru, Waterfalls, Kanisa la Kale, Makaburi ya Kale, Ndege wenye rangi za kuvutia, Wanyama wa aina yake n.k

Pia, Mhe. Abood anasema Msiache kutembelea Miradi mikubwa iliyotekelezwa na inazoyotekelezwa kwa Fedha alizozitoa MAMA Mhe. Dkt. SAMIA SULUHU HASSAN Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mathalani Vituo vikubwa vya Afya,
✅ Kituo cha Afya Tungi
✅ Kituo cha Afya Lukobe.
✅ Hospitali ya Wilaya

Shule Mpya za Sekondari Sita pamoja na Ofisi za Utawala, Maabara na Maktaba zake ambazo ni:-
✅ Mindu Sekondari
✅ Lukobe Juu Sekondari
✅ Mazimbu Sekondari
✅ Tungi Sekondari
✅ Mbuyuni Sekondari
✅ Mkundi Sekondari.

Ujenzi wa Zahanati sita za Kata, Miradi Mikubwa ya Maji Tank kubwa la Mgulu wa Ndege la Lita Milioni Mbili, Substation ya Maji, Miradi kamilifu ya Maji (Mradi wa Maji Bigwa-Kilakala, Kasi ya Ujenzi wa Mradi mkubwa wa SGR Morogoro

Mhe. Abood anawakaribisha Sana Sana, uwepo wenu ndani ya Jimbo la Morogoro Mjini, ni furaha kubwa Sana kwa Wananchi wa Jimbo la Morogoro Mjini.

KARIBUNI SANA
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-04-30 at 09.04.08.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-30 at 09.04.08.jpeg
    58.6 KB · Views: 2
Kitaifa au Kimkoa? Kweli abood ndio Morogoro kwa sasa....hakuna Karogeres wala Kalalambe wala familia Khan
 
Mwambie apambane na changamoto ya maji. Wananchi wake wanaishi kama wapo sudan huko.

Moro vyanzo vingi vya maji lakni wananchi wanateseka kupata maji ya uhakika.
 
Muheshimiwa Mbunge Abood kongole kwako, ata kama Morogoro Mjini kuna changamoto bado, lakini Mji unakua vyema sana kwa miundombinu,biashara, elimu na nguvukazi. Treni ya SGR ikianza kazi Morogoro itakua hesabu nyingine kwa biashara, Utalii na Elimu. Muheshimiwa Mbunge jitaidi kuweka mazingira ya viwanda vidogo vidogo vya kuchakata mazao ya kilimo (startup), ili kuwezesha Morogoro kuweza kubakisha nguvukazi ilioelimika kutoka vyuo vingi vilivyopo hapo, na kuifanya Morogoro Mjini kuwa mji wa wawekezaji wadogo wa ndani walioelimika(literate).
 
Kama vile wafanyakazi wamejitambua..hata mada za mei mosi naona hazishobokewi sana.
 
Back
Top Bottom