Mbunge Musukuma acha kiherehere cha kutusemea watu wa Kanda ya Ziwa

Mbunge Musukuma acha kiherehere cha kutusemea watu wa Kanda ya Ziwa

Kanamusi

Member
Joined
Apr 9, 2020
Posts
22
Reaction score
65
Mbunge Musukuma sisi wakazi wa kanda ya ziwa hatukukutuma na hatujawahi kukuchagua kuwa msemaji wetu kwa jambo lolote.

Sisi wazee na watu wa kanda ya ziwa hatukukutuma kusema hayo unayoita mapigo ya kumjibu Antony Diallo na kama ulikuwa na nia ya kujibu mapigo ungemjibu kwa utashi wako au kwa niaba ya wananchi wa jimbo lako la Geita vijijini lakini sio kutuhusisha watu wa kanda ya ziwa kwenye maugomvi yako binafsi na kusema kwamba sisi ndio tumekutuma ukatusemee.

Sisi wazee wa kanda ya ziwa ni watu wenye busara na hekima, kama kuna jambo linaenda ndivyo sivyo tuna njia zetu za kuwasilisha maduku duku yetu ikiwemo kujisemea wenyewe na sio kutuma kijana mropokaji kama wewe.

Kuhusu kifo cha hayati Magufuli unasema tuliofiwa ni watu wa kanda ya ziwa. Kimsingi hii ni kauli ya kijinga kabisa kutolewa na kiongozi wa wananchi kama wewe kwa sababu Rais Magufuli hakuwa Rais wa kanda ya ziwa bali alikuwa ni Rais wa watanzania wote wa kanda za mikoa yote nchini. Sasa unaanzaje kusema kwamba tuliofiwa ni watu wa kanda ya ziwa pekee?

Huoni kama kauli yako inalenga kutugawa watu wa kanda ya ziwa na watu wa kanda zingine?

Kwa mara nyingine mbunge Musukuma usituhusishe tena wazee na watu wa kanda ya ziwa kwenye ugomvi wako binafsi wa kutafuta umaarufu wa kisiasa na sifa za kishamba na UKOME kabisa kutusemea kwa sababu hata sisi tuna midomo ya kujisemea.

Message sent & delivered
 
Kuna kiongozi kutoka makao makuu CCM anaitwa kanali wasiasa zakimataifa. Alijibu vizuri na kwabusara sana.

Nanukuu

"CCM haijafanya tathimini ya marais waliopita, hayo ni mawazo/maoni ya Diallo".

Sasa huu ushamba wakilamtu kuwa msemaji na ujuaji nikuongeza umarufu wa maneno ya Diallo.

UVCCM wawe namipaka kimatamko.
 
Mbunge msukuma sisi wakazi wa kanda ya ziwa hatukukutuma na hatujawahi kukuchagua kuwa msemaji wetu kwa jambo lolote.

Sisi wazee na watu wa kanda ya ziwa hatukukutuma kusema hayo unayoita mapigo ya kumjibu Antony Diallo na kama ulikuwa na nia ya kujibu mapigo ungemjibu kwa utashi wako au kwa niaba ya wananchi wa jimbo lako la geita vijijini lakini sio kutuhusisha watu wa kanda ya ziwa kwenye maugomvi yako binafsi na kusema kwamba sisi ndio tumekutuma ukatusemee.

Sisi wazee wa kanada ya ziwa ni watu wenye busara na hekima, kama kuna jambo linaenda ndivyo sivyo tuna njia zetu za kuwasilisha maduku duku yetu ikiwemo kujisemea wenyewe na sio kutuma kijana mropokaji kama wewe.

Kuhusu kifo cha hayati magufuri unasema tuliofiwa ni watu wa kanda ya ziwa. Kimsingi hii ni kauli ya kijinga kabisa kutolewa na kiongozi wa wananchi kama wewe kwa sababu Rais magufuri hakuwa Rais wa kanda ya ziwa bali alikuwa ni Rais wa watanzania wote wa kanda za mikoa yote nchini. Sasa unaanzaje kusema kwamba tuliofiwa ni watu wa kanda ya ziwa pekee?

Huoni kama kauli yako inalenga kutugawa watu wa kanda ya ziwa na watu wa kanda zingine?

Kwa mara nyingine mbunge msukuma usituhusishe tena wazee na watu wa kanda ya ziwa kwenye ugomvi wako binafsi wa kutafuta umaarufu wa kisiasa na sifa za kishamba na UKOME kabisa kutusemea kwa sababu hata sisi tuna midomo ya kujisemea.

Message sent & delivered
Na ww acha kiherehere cha kuja jf kutusemea watu wa kanda ya ziwaaa..tuwacheee musukuma kasema anavyaomn yeye na wale anaowaongoza ndio walimtuma kusema hivyo ww ni unaongoza nani zaid ya mkeo na wanao? Hata hata jf huna cheo..tuliaa ww..
 
Wewe ni mpumbavu pia, kwa nini umpangie Musukuma cha kusema? kila siku mpo hapa kusema watu wawe huru kutoa mawazo yao leo hii unakuja hapa kutuaminisha unachoaamini wewe.Bila shaka wewe ni mhanga wa utawala wa Magufuli kama ilivyo member wengi wa humu jamii forum, kwa hiyo jitahidi sana kuvumilia wenzako kama wewe unavyotaka uvumiliwe.
Serikali imeweka utaratibu wa kila mwanasiasa kufanya siasa katika jambo lake sasa yeye kinachomtoa huko jimboni kwake vijijini na kuja kuturopokea kwenye jiji letu ni nini?? Kwani hawezi kuropokea kwenye jimbo lake?

Kama anataka kupandikiza ukabila kwenye kanda yetu mwambie huo ujinga aupeleke kwenye jimbo lake sisi watu wa kanda ya ziwa hasituhusishe kabisa na akome.
 
Serikali imeweka utaratibu wa kila mwanasiasa kufanya siasa katika jambo lake sasa yeye kinachomtoa huko jimboni kwake vijijini na kuja kuturopokea kwenye jiji letu ni nini?? Kwani hawezi kuropokea kwenye jimbo lake?
Wewe hujui kuwa Msukuma anakaa mwanza maeneo ya kirumba karibu na kitangiri hapo. Unafikiri Musukuma mwanza kaja juzi? Usikariri maisha mkuu jipange upya geita ni asili yao tu ila yeye na familia yake anakaa mwanza na ananyumba nyingi tu hapo town.
 
Mbunge msukuma sisi wakazi wa kanda ya ziwa hatukukutuma na hatujawahi kukuchagua kuwa msemaji wetu kwa jambo lolote.

Sisi wazee na watu wa kanda ya ziwa hatukukutuma kusema hayo unayoita mapigo ya kumjibu Antony Diallo na kama ulikuwa na nia ya kujibu mapigo ungemjibu kwa utashi wako au kwa niaba ya wananchi wa jimbo lako la geita vijijini lakini sio kutuhusisha watu wa kanda ya ziwa kwenye maugomvi yako binafsi na kusema kwamba sisi ndio tumekutuma ukatusemee.

Sisi wazee wa kanada ya ziwa ni watu wenye busara na hekima, kama kuna jambo linaenda ndivyo sivyo tuna njia zetu za kuwasilisha maduku duku yetu ikiwemo kujisemea wenyewe na sio kutuma kijana mropokaji kama wewe.

Kuhusu kifo cha hayati magufuri unasema tuliofiwa ni watu wa kanda ya ziwa. Kimsingi hii ni kauli ya kijinga kabisa kutolewa na kiongozi wa wananchi kama wewe kwa sababu Rais magufuri hakuwa Rais wa kanda ya ziwa bali alikuwa ni Rais wa watanzania wote wa kanda za mikoa yote nchini. Sasa unaanzaje kusema kwamba tuliofiwa ni watu wa kanda ya ziwa pekee?

Huoni kama kauli yako inalenga kutugawa watu wa kanda ya ziwa na watu wa kanda zingine?

Kwa mara nyingine mbunge msukuma usituhusishe tena wazee na watu wa kanda ya ziwa kwenye ugomvi wako binafsi wa kutafuta umaarufu wa kisiasa na sifa za kishamba na UKOME kabisa kutusemea kwa sababu hata sisi tuna midomo ya kujisemea.

Message sent & delivered
Wewe umekuwa lini mzee wa Wasukuma?
Alichosema Msukuma ndo msimamo wa Kanda ya Sukuma gang mnayoizodoa Kila siku mtandaoni.
 
Sijamkataza kufanya siasa lakini afanyie kwenye jimbo lake sisi watu wa kanda ya ziwa hatujawahi kumchagua mahali popote pale kuwa msemaji wetu. Aache kiherehere
Wewe unamkataza musukuma kuwasemea watu wa ziwa mbona hatujakaa kikao kama wana ziwa tukakutuma wewe ukanushe hayo ya musukuma.kimsingi musukuma yuko sawa dialo kakosea sana.
 
Tumemvumilia vya kutosha, pumba anazoongea anazijua mwenyewe.
Kiboko yake ni yule RPC wa Geita, Alijifanya kumletea majungu siku alipoingia kwenye 18 zake, akitegemea aliyekuwa akimsifia jiwe kuwa angeingilia kati wapi!!yaani jamaa anajipendekeza hadi bosi ana kasirika!!!na siku zote agenda zake huwa ni za kikabila tu,
 
Back
Top Bottom