Mbunge Sebastian Kapufi: Tanzania Tuna Wakia Milioni 45 ya Akiba ya Dhahabu Leo Tunasomeka Kati ya nchi Masikini Duniani

Mbunge Sebastian Kapufi: Tanzania Tuna Wakia Milioni 45 ya Akiba ya Dhahabu Leo Tunasomeka Kati ya nchi Masikini Duniani

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Mbunge Sebastian Kapufi: Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ kwa ujumla wake tuna Wakia Milioni 45 ya akiba ya dhahabu lakini leo tunasomeka ni kati ya nchi Masikini Duniani

"Hotuba ya Waziri Mkuu Imezungumzia Maji, Misitu, Madini, Kilimo. Kuna Nchi Haina Msitu ni Jangwa. Kwa Nchi Yetu ya Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ Kila Kitu Kipo, Kwanini Tunaangukia Kwenye Nchi Masikini, Ni Wapi Tumekosea?" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Namshukuru Mama Samia. Pale kwetu Katavi kulikuwa na shida kubwa ya Suala la uchujaji damu kwenye Figo. Wapiga kura wamehamia Mbeya, Dar es Salaam, Mwanza kwaajili ya Suala la uchujaji damu kwenye Figo maana kwa Wiki moja alikuwa anachuja damu mara tatu, hawezi kukaa Mpanda" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Mama Samia Suluhu Hassan amenileteq fedha Mpanda kwa kuanzia Shilingi Milioni 196 kwaajili ya kujenga chumba cha kusaidia wagonjwa wa uchujaji wa damu. Ule mradi kwa ujumla wake ni Shilingi Milioni 400. Nashukuru sana katika hilo" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Skimu ya umwagiliaji maji ya Mwamkuru tumeletewa Shilingi Bilioni 31, Skimu kasi yake ni ndogo lakini naomba Wataalam waongeze kasi. Tuna mradi wa TACTIC ulikuwa na shida kidogo lakini Wataalam wamefanya utafiti tuna kilomita 8.2 za lami kwaajili ya Mji wa Mpanda na miji 28 kutatuliwa tatizo la maji katika mji wa Mpanda" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Mheshimiwa Waziri Mkuu, Kuna fidia kwa wananchi wa Bwawa la Mirara na fidia ya wananchi waliopisha ujenzi wa barabara kutoka Starike kuja Mpanda Mjini. Tunaomba sana fidia ya maeneo hayo" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini.

"Biashara ya Kaboni (Misitu na Uoteshaji Misitu) ni chanzo kikubwa cha mapato. Tunapotengeneza Madampo ya kisasa tufikirie kuhusu Biashara ya Kaboni. Kamati tulishauri elimu ya Kaboni iwafikie wabunge wote" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini.

"Miradi ya Barabara, Reli, Viwanja vya Ndege na Bandari. Ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) Dar es Salaam - Morogoro - Dodoma - Tabora - Mwanza - Kigoma ni jambo jema sana lakini kipande cha Kaliua - Mpanda - Karema kisomeke. Kutoka Mpanda - Dar es Salaam kwa Treni ya kawaida ni siku tatu, kwa Ndege ni masaa mawili. Katika hili Naishukuru Serikali" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini.

"Ghana ๐Ÿ‡ฌ๐Ÿ‡ญ ni ya kwanza kwa uzalishaji dhahabu Africa ๐ŸŒ inazalisha Tani 117. Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ inashika nafasi ya Nne kwa uzalishaji. Duniani; China ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ณ (370 Metric Tons), Australia ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡บ (310 Metric Tons), Russia ๐Ÿ‡ท๐Ÿ‡บ (310 Metric Tons), Canada ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฆ (200 Metric Tons) na United States of America ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ธ (170 Metric Tons).

_MG_2236cvbgtyh.jpg
 
Tanzania tuna rasilimali ghafi ila akili ziro.
 
Kwenye hilo suala la kuwa na madini mengi ni moja ni pamoja na kuwa na utaalamu wa kuyachimba na kufanya processing kuipata hiyo product ambayo itaingia sokoni he hao wataalamu wapo na mazingira yao ya Nazi yakoje! nahisi tukiwajali kwanza hao wataalamu na wakaona hayo madini no yao na yananufaisha taifa kwa masoko yalio wazi na hata kwa kuingia ubia wenye mtazamo chanya kikubwa kibaki hapa kilichochimbwa na kufanyike masoko huru hapa waje kununua hapa kwani faida kubwa itabaki hapa hakika hapo tutanufaika na utajiri wetu huo tuliopewa na Mungu na kupunguza kama sio kutoa siasa kwenye mambo ya msingi!!
Nawasilisha!!
 
Tatizo uchawa.hatuambiani ukweli.mbunge mwenyewe anataka kujua sababu ya umasikini lakini hapohapo anaamza kushukuru rais.sasa unashukuru umasikini au Nini?kama anafanya kazi nzuri kwanini Sasa utuulize sisi tumekosea wapi kuwa watu masikini
 
Tz tumekosa waziri wa fedha mbunifu ndio maana ya haya yote!
Kazi ni kusaini mikataba ya mikopo kila uchwao ila ubunifu hakuna!
Mama tafuta waziri wa fedha mwenye maono na ubunifu akusaidie!
 
Mbunge Sebastian Kapufi: Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ kwa ujumla wake tuna Wakia Milioni 45 ya akiba ya dhahabu lakini leo tunasomeka ni kati ya nchi Masikini Duniani

"Hotuba ya Waziri Mkuu Imezungumzia Maji, Misitu, Madini, Kilimo. Kuna Nchi Haina Msitu ni Jangwa. Kwa Nchi Yetu ya Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ Kila Kitu Kipo, Kwanini Tunaangukia Kwenye Nchi Masikini, Ni Wapi Tumekosea?" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Namshukuru Mama Samia. Pale kwetu Katavi kulikuwa na shida kubwa ya Suala la uchujaji damu kwenye Figo. Wapiga kura wamehamia Mbeya, Dar es Salaam, Mwanza kwaajili ya Suala la uchujaji damu kwenye Figo maana kwa Wiki moja alikuwa anachuja damu mara tatu, hawezi kukaa Mpanda" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Mama Samia Suluhu Hassan amenileteq fedha Mpanda kwa kuanzia Shilingi Milioni 196 kwaajili ya kujenga chumba cha kusaidia wagonjwa wa uchujaji wa damu. Ule mradi kwa ujumla wake ni Shilingi Milioni 400. Nashukuru sana katika hilo" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Skimu ya umwagiliaji maji ya Mwamkuru tumeletewa Shilingi Bilioni 31, Skimu kasi yake ni ndogo lakini naomba Wataalam waongeze kasi. Tuna mradi wa TACTIC ulikuwa na shida kidogo lakini Wataalam wamefanya utafiti tuna kilomita 8.2 za lami kwaajili ya Mji wa Mpanda na miji 28 kutatuliwa tatizo la maji katika mji wa Mpanda" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Mheshimiwa Waziri Mkuu, Kuna fidia kwa wananchi wa Bwawa la Mirara na fidia ya wananchi waliopisha ujenzi wa barabara kutoka Starike kuja Mpanda Mjini. Tunaomba sana fidia ya maeneo hayo" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini.

"Biashara ya Kaboni (Misitu na Uoteshaji Misitu) ni chanzo kikubwa cha mapato. Tunapotengeneza Madampo ya kisasa tufikirie kuhusu Biashara ya Kaboni. Kamati tulishauri elimu ya Kaboni iwafikie wabunge wote" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini.

"Miradi ya Barabara, Reli, Viwanja vya Ndege na Bandari. Ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) Dar es Salaam - Morogoro - Dodoma - Tabora - Mwanza - Kigoma ni jambo jema sana lakini kipande cha Kaliua - Mpanda - Karema kisomeke. Kutoka Mpanda - Dar es Salaam kwa Treni ya kawaida ni siku tatu, kwa Ndege ni masaa mawili. Katika hili Naishukuru Serikali" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini.

"Ghana ๐Ÿ‡ฌ๐Ÿ‡ญ ni ya kwanza kwa uzalishaji dhahabu Africa ๐ŸŒ inazalisha Tani 117. Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ inashika nafasi ya Nne kwa uzalishaji. Duniani; China ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ณ (370 Metric Tons), Australia ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡บ (310 Metric Tons), Russia ๐Ÿ‡ท๐Ÿ‡บ (310 Metric Tons), Canada ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฆ (200 Metric Tons) na United States of America ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ธ (170 Metric Tons).

View attachment 2965195
Hayo mambo alitakiwa akaulize wakiwa kwenye vikao vyao vya sisiemu kwa nini wanatufanyia hivi sisi wananchi?Ukiyakosoa yanakuja kukuambia sio uzalendo,sasa unasimama vipi na mwenyekiti ile hali chama kinafukarisha wananchi?
 
Hatuna uongozi na usimamizi bora wa rasilimali zetu

Ova
 
Back
Top Bottom