Elections 2010 Mbunge wa Arusha apigwa hadi kuzirai na jeshi la polisi

Elections 2010 Mbunge wa Arusha apigwa hadi kuzirai na jeshi la polisi

Heshima kwenu wanjamvi,

Ni kweli Mbunge wa Arusha Mheshimiwa Godbless Lema kapigwa sana na polisi [FFU].
Jana iliamuliwa kikao cha kumchagua Meya wa Jiji la Arusha kifanyike leo saa 3 asubuhi,kikao cha jana kilishindwa kumchagua Meya kwasababu CCM walitaka kumchomeeka mjumbe kutoka Tanga ili kuwasaidia kwenye mchakato wa kupiga kura pamoja na mizengwe ya kumchomeka mjumbe wa Tanga lakini bado CHADEMA walikuwa na nafasi ya kushinda kwakuwa diwani wa TLP Mheshimiwa Kivuyo alikuwa akiwaunga mkono CHADEMA.

Maajabu yalianza kujitokeza hiyo saa 3 asubuhi badala ya wajumbe wa CHADEMA kwenda kwenye kikao cha kumchagua Meya waliamua kufanya kikao Hotel Ikweta mkabala na ukumbi wa manispaa ya Arusha.Mheshimiwa Kivuyo baada ya kuona wajumbe wa CHADEMA hawaingii kwenye mkutano aliamua kuwafuata Ikweta Hotel kuwasihi wahudhurie kwenye kikao kwakuwa bado walikuwa na nafasi ya kushinda kiti cha umeya lakini juhudi zake hazikuzaa matunda wajumbe wa CHADEMA waliendelea kususia kikao cha uchaguzi wa Meya.

Mwenyekiti wa kikao cha uchaguzi wa Meya Bwana E Chang'ah aliamua kufanya mawasiliano na ofisi ya waziri mkuu.Waziri wa nchi Tawala za mikoa na serekali za mitaa alitoa maagizo sheria zifuatwe kwa kuwa idadi ya wajumbe ilifikia nusu mchakato wa uchaguzi ukaendela bila ya wajumbe wa CHADEMA kushiriki kwenye kikao.Wajumbe wa CHADEMA wakajulishwa Meya tayari kachaguliwa wakaamua kuingia kwenye kikao wakiongozwa na Mheshimiwa Mbunge G Lema.Zilitokea purukushani za hapa na pale Lema akachomoa bastola FFU wakmvamia na kumpokonya na kumpiga vibaya sana.

Wanajamvi CHADEMA hawakuwa na sababu za kutoingia ndani ya kikao cha uchaguzi wa Meya.Meya alipochaguliwa wajumbe wa CHADEMA wakaamua kuingia sijui waliingia kufanya nini ?.Lema hakutakiwa kutoa bastola yake wakati askari wa usalama walikuwepo eneo la tukio sijui alitaka kumpiga nani ?.Ikumbukwe Lema ana kesi ya kutishia kuuwa Mkurugenzi wa Jiji.

Ngongo,

Nashukuru kwa taarifa hii mana imejibu baadhi ya maswali. Unaweza kumpata mmoja wa madiwani wa CDM wakaelezea sababu?

Hili la Lema kuwa na kesi ya kutishia hailalalishi kutotoa bastola, something is not right here mana wangemnyang'anya tu basi sio mpaka kumpiga.

Alhaji ANS
 
Hiyo ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI waliona ni sawa tu kwa ccm kuleta diwani toka tanga kimagumashimagumashi tu? Hizo taratibu zinawahusu CDM peke yao lakini ccm wanaweza kuzivunja maana wako juu yake?

Sishangai kitendo cha Lema kupoteza uvumilivu maana naona ni wakati mwafaka sasa kama hupati haki stahili yako inabidi utumie nguvu tu kuinyang'anya.

Pole lema and I wish you a quick recovery!

Shame on you ccm idiotoz!
 
Ngogo mbona sababu ya CDM kutoingia kwenye kikao iko wazi! Taratibu zinaruhusu kujiongezea wajumbe ili kushinda uchaguzi?
 
Kweli hawa jamaa wanataka madaraka hata kwa Kumwaga damu...tunaomba muendee kutuhabarisha.
 
Ngongo asante kwa taarifa, ngoja 2subiri na vyombo vya habari vitasemaje.
 
Ni budi Watanzania tuwaambie polisi kuwa imetosha, hawawezi kuendelea kutumika na CCM kama chombo cha kugandamiza Raia. Vyama vya Siasa, wanaharakati, wasomi, na wananchi wote wenye mapenzi mema, kwa vitendo kama hivi tutoe kauli kuwa adui mkubwa wa haki ya Mtanzania ni CCM na polisi. Kila mahali watu watakapoiona CCM na polisi na viashiria vyake wajue wamemwona adui yao. Hata bila ya kufanya chochote, bila ya kufanya vurugu, hiyo itaosha. Hatuwezi kuwazuia kufanya uovu lakini hawawezi kutulazimisha kuwapa ushirikiano wa aina yeyote.

Kama serikali haiwezi kuchukua hatua dhidi ya polisi hao, na tuna uhakika kuwa mfumo wetu wa mahakama hauwezi kutenda haki, basi matukio haya na yanayofanana nayo yaanze kuchukuliwa ushahidi wa kutosha, na mashtaka yafunguliwe kwenye mahakama ya kimataifa dhidi ya Rais kwa kutumia vibaya vyombo vya dola na kushindwa kulinda haki ya Raia wote kwa haki.
 
Kwanini Lema amepigwa? Naomba tupe details zaidi of what really happened.
 
na sikia alikuwa ametoa mil 200 kwa ajili ya kuhakikisha meya anatoka CCM, hasa ukizingatia vitega uchumi vyake viko arusha..

Hii ndiyo hasa sababu ya mchezo mchafu wote huu!..Walijaribu kwENYE uBUNGE WAKACHEMSHA...Sasa wanatumia kila hila, ikiwa ni kumwaga fedha ili kupindisha uhalali wa uchaguzi.
Nawaunga mkono CHADEMA...
nGONGO BADO TUTATOFAUTIANA SANA KWA USHABIKI WAKO KUWALAUMU CHADEMA BILA KUTIZAMA SUALA HILI KWA KUINGIA KWENYE VIATU VYAO.
 
Akili yako haina akili...una ushaidi wowote wa kututhibitia hilo la ujuaji..hasa kupelekea kupigwa kwake? Nadhani unamatatizo ya akili wewe. Dawa yenu haiko mbali.
 
Heshima kwenu wanjamvi,

Ni kweli Mbunge wa Arusha Mheshimiwa Godbless Lema kapigwa sana na polisi [FFU].
Jana iliamuliwa kikao cha kumchagua Meya wa Jiji la Arusha kifanyike leo saa 3 asubuhi,kikao cha jana kilishindwa kumchagua Meya kwasababu CCM walitaka kumchomeeka mjumbe kutoka Tanga ili kuwasaidia kwenye mchakato wa kupiga kura pamoja na mizengwe ya kumchomeka mjumbe wa Tanga lakini bado CHADEMA walikuwa na nafasi ya kushinda kwakuwa diwani wa TLP Mheshimiwa Kivuyo alikuwa akiwaunga mkono CHADEMA.

Maajabu yalianza kujitokeza hiyo saa 3 asubuhi badala ya wajumbe wa CHADEMA kwenda kwenye kikao cha kumchagua Meya waliamua kufanya kikao Hotel Ikweta mkabala na ukumbi wa manispaa ya Arusha.Mheshimiwa Kivuyo baada ya kuona wajumbe wa CHADEMA hawaingii kwenye mkutano aliamua kuwafuata Ikweta Hotel kuwasihi wahudhurie kwenye kikao kwakuwa bado walikuwa na nafasi ya kushinda kiti cha umeya lakini juhudi zake hazikuzaa matunda wajumbe wa CHADEMA waliendelea kususia kikao cha uchaguzi wa Meya.

Mwenyekiti wa kikao cha uchaguzi wa Meya Bwana E Chang'ah aliamua kufanya mawasiliano na ofisi ya waziri mkuu.Waziri wa nchi Tawala za mikoa na serekali za mitaa alitoa maagizo sheria zifuatwe kwa kuwa idadi ya wajumbe ilifikia nusu mchakato wa uchaguzi ukaendela bila ya wajumbe wa CHADEMA kushiriki kwenye kikao.Wajumbe wa CHADEMA wakajulishwa Meya tayari kachaguliwa wakaamua kuingia kwenye kikao wakiongozwa na Mheshimiwa Mbunge G Lema.Zilitokea purukushani za hapa na pale Lema akachomoa bastola FFU wakmvamia na kumpokonya na kumpiga vibaya sana.

Wanajamvi CHADEMA hawakuwa na sababu za kutoingia ndani ya kikao cha uchaguzi wa Meya.Meya alipochaguliwa wajumbe wa CHADEMA wakaamua kuingia sijui waliingia kufanya nini ?.Lema hakutakiwa kutoa bastola yake wakati askari wa usalama walikuwepo eneo la tukio sijui alitaka kumpiga nani ?.Ikumbukwe Lema ana kesi ya kutishia kuuwa Mkurugenzi wa Jiji.

I see! Asante kwa info.
 
Kwanini Lema amepigwa? Naomba tupe details zaidi of what really happened.
Ati kisa katoa Bastola kwaajili ya kujilinda...walimpa bastola ya nini kama si ya kupambana na watu washenzi wanaompiga mtu hadi azimie!..Kwanza alitakiwa ampe mmoja ya ugoko!
 
I see! Asante kwa info.
Very sided-Info...Ni ya kishabiki zaidi, na haiko balanced!...Habari za NGONGO kila siku ni za kashfa kwa CHADEMA, NA anafurahia sana lolote baya linaloipata...
Baada ya CHADEMA kushinda Ubunge Arusha, ngongo ALIPOTEA KABISA mtandaoni..na ndio anaibuka sasa ili kuripoti tatizo hili!...
I never trust him as far as political ideologies are concerned, japokuwa ni rafiki yangu wa karibu!
 
Heshima kwenu wanjamvi,

Ni kweli Mbunge wa Arusha Mheshimiwa Godbless Lema kapigwa sana na polisi [FFU].
Jana iliamuliwa kikao cha kumchagua Meya wa Jiji la Arusha kifanyike leo saa 3 asubuhi,kikao cha jana kilishindwa kumchagua Meya kwasababu CCM walitaka kumchomeeka mjumbe kutoka Tanga ili kuwasaidia kwenye mchakato wa kupiga kura pamoja na mizengwe ya kumchomeka mjumbe wa Tanga lakini bado CHADEMA walikuwa na nafasi ya kushinda kwakuwa diwani wa TLP Mheshimiwa Kivuyo alikuwa akiwaunga mkono CHADEMA.

Maajabu yalianza kujitokeza hiyo saa 3 asubuhi badala ya wajumbe wa CHADEMA kwenda kwenye kikao cha kumchagua Meya waliamua kufanya kikao Hotel Ikweta mkabala na ukumbi wa manispaa ya Arusha.Mheshimiwa Kivuyo baada ya kuona wajumbe wa CHADEMA hawaingii kwenye mkutano aliamua kuwafuata Ikweta Hotel kuwasihi wahudhurie kwenye kikao kwakuwa bado walikuwa na nafasi ya kushinda kiti cha umeya lakini juhudi zake hazikuzaa matunda wajumbe wa CHADEMA waliendelea kususia kikao cha uchaguzi wa Meya.

Mwenyekiti wa kikao cha uchaguzi wa Meya Bwana E Chang'ah aliamua kufanya mawasiliano na ofisi ya waziri mkuu.Waziri wa nchi Tawala za mikoa na serekali za mitaa alitoa maagizo sheria zifuatwe kwa kuwa idadi ya wajumbe ilifikia nusu mchakato wa uchaguzi ukaendela bila ya wajumbe wa CHADEMA kushiriki kwenye kikao.Wajumbe wa CHADEMA wakajulishwa Meya tayari kachaguliwa wakaamua kuingia kwenye kikao wakiongozwa na Mheshimiwa Mbunge G Lema.Zilitokea purukushani za hapa na pale Lema akachomoa bastola FFU wakmvamia na kumpokonya na kumpiga vibaya sana.

Wanajamvi CHADEMA hawakuwa na sababu za kutoingia ndani ya kikao cha uchaguzi wa Meya.Meya alipochaguliwa wajumbe wa CHADEMA wakaamua kuingia sijui waliingia kufanya nini ?.Lema hakutakiwa kutoa bastola yake wakati askari wa usalama walikuwepo eneo la tukio sijui alitaka kumpiga nani ?.Ikumbukwe Lema ana kesi ya kutishia kuuwa Mkurugenzi wa Jiji.

Unaonekana ulikuwa karibu na yaliyokuwa yakitokea. Tupe majibu kuhusu yafyatayo:
1. Huyo anayeitwa mjumbe kutoka Tanga aliingiaje kwenye kikao? Kikao cha madiwani kinafahamika kuwa wajumbe wake ni wepi? Hiyo bado kwangu haitoshi kama ni sababu ya kuahirisha kikao.
2. Una ukweli gani kuwa Chadema walikuwa kwenye maeneo ya Hoteli ya Ikweta? Hilo la diwani wa TLP kuwafuata lilikuwa agizo la mwenyekiti wa kikao au kwa uamuzi wake?
3. Mawasiliano kati ya mwenyekiti wa kikao na TAMISEMI yalifanyika kwa njia ya simu au njia nyingine? maagizo ya simu yanatosha kutumiwa katika jambo kama hilo.
4. Je mwenyekiti hakufahamu kitu cha kufanya kiasi cha kufanya mawasiliano na TAMISEMI wakati amepewa jukumu la kusimamia uchaguzi?
5. Hujui Lema alitaka kumpiga nani, lakini tuambie kama polisi walishamkamata Lema na kumnyang'anya bastola kwanini bado walimpiga? unajua sababu za polisi kumpiga Lema.

Ninavyoona maelezo yako inaonekana wewe ulikuwa sehemu ya mpango wa kilichotendeka au ulijiandaa kutoa habari uliyoitoa katika namna ya mpango siyo kuripoti tukio.
 
Sasa Umuhimu wa Tundu Lissu na Mabere Marando inabidi uonekane......... Nadhani itakuwa bora hawa jamaa watinge huko Arusha......
 
Ccm bwana, wameshindwa hata kujifunza kwa yanayotokea kwa jirani zetu wakenya! Labda wanakuwa na jeuri kwa kuwa mali zetu zote wanawahonga hao wakubwa wa dunia.
 
Mwenyekiti wa kikao cha uchaguzi wa Meya Bwana E Chang'ah aliamua kufanya mawasiliano na ofisi ya waziri mkuu.Waziri wa nchi Tawala za mikoa na serekali za mitaa alitoa maagizo sheria zifuatwe kwa kuwa idadi ya wajumbe ilifikia nusu mchakato wa uchaguzi ukaendela bila ya wajumbe wa CHADEMA kushiriki kwenye kikao.Wajumbe wa CHADEMA wakajulishwa Meya tayari kachaguliwa wakaamua kuingia kwenye kikao wakiongozwa na Mheshimiwa Mbunge G Lema.Zilitokea purukushani za hapa na pale Lema akachomoa bastola FFU wakmvamia na kumpokonya na kumpiga vibaya sana.
Ngongo

Nusu gani ya wajumbe unayoisema imetimia tunachojua wanaopiga kura ni madiwani ambapo CCM hawafiki nusu yake au unahesabu na polisi waliokuwepo na huyo diwani wa Tanga tunayeambiwa. Nafikiri hii taarifa iko biased nashauri tusiifuate tusubiri taarifa ya mtu aliye nuetral.
 
Hayo mambo ya kutoa bastola ni uongo, kwani nani atasema hakutoa bastola? Ukiwa na silaha kama hiyo whether uitoe au la unaweza kusingiziwa chochote kile. Kisheria swala liwe aliitumia bastola hiyo kuua kama alivyofanya Dito? Vinginevyo hayo ni mazingaombwe tu. swala jingine ilikuwaje Polisi na FFU wawe tayari kwenye mazingira kama hayo ambayo sidhani kama walihitajika. Je kulikuwa na plan in place kutimiza walichopanga?

Nafikiri watanzania watakubaliana na mimi kwamba Rais wa nchi anapokuwa Mwizi inakuwa ni kama kilema kila Tom, Dick and Harry atakuwa Mwizi. Yaani rais hawezi kukemea kile ambacho yeye mwenyewe anakifanya.
 
UMEYA ARUSHA, tatizo ni Katibu wa CCM Mkoa Mary Chatanda vigogo wamelazimisha apige kura ya kumchagua Meya wa Jiji la Arusha wakati yeye ni mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Tanga tena anawakilisha wilaya ya Korogwe.

Baada ya kipigo kwa sasa taarifa zinasema Lema mbunge amepelekwa hospital yupo hoi.
 
Back
Top Bottom