Pre GE2025 Mbunge wa Covid 19, Nusrat Hanje atangaza kugombea jimbo la zamani la Tundu Lissu, Singida Mashariki

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nadhani Mbowe aongee na wapiga kura wa jimbo la Hai, kama wanataka agombee ubunge au asigombee ubunge.

Na kama agombee, je ni kupitia chadema au ccm. Kama kupitia chadema ok. Kama kupitia ccm, basi ajiunge na ccm. Na akishinda ubunge, na ccm ikishinda uchaguzi, saa100 anaweza kumteua Mbowe kuwa waziri mkuu wa Tanzania.

Wengine wanaoweza kuwa waziri mkuu wa Tanzania ni Mkenda, Mwigulu, Kabudi, au mbunge mmoja atakae toka eneo la usukumani (kabila lake awe ni msukuma, na sio mtu wa mkoa wa Mara).

Waprotestanti wapewe preference kwenye nafasi ya uwaziri mkuu, kama hakuna mprotestanti anaefaa, basi waziri mkuu awe mkatoliki (kama Mkenda). Waziri mkuu atoke mbali na kusini, as Nchimbi makamu wa rais mtarajiwa anatokea kusini tayari.

Majaliwa anaweza kuendelea kuwa waziri, na sio waziri mkuu. Kimei anaweza kuteuliwa kuwa naibu waziri wa wizara fulani.

Mtu yeyote wa chadema ambaye, anaona kwamba hata fikia potential yake chini ya uongozi mpya wa chadema, anaweza akawa mpole au anaweza akahamia ccm. Ccm isiwatumie watu wanao hamia kutoka chadema, kama nyenzo ya propaganda mbaya, dhidi ya wenzao waliobaki huko chadema.

Vuguvugu la uzalendo limeongezeka, hususan baada ya Tundu Lissu kushinda chadema. Inaelekea kanisa katoliki limeongeza uwekezaji wao huko chadema. Naona pia mkoa wa Mara umeongeza uwekezaji wao huko chadema.

Inabidi Saa100, kama anaweza, a renegotiate mikataba yote mibovu na aifanye iwe na maslahi na ustawi mzuri kwa watanzania.

Abalance vizuri uzalendo, haki za binadamu na demokrasia, huku akiendelea kuwa na mahusiano mazuri na mataifa yenye nguvu duniani. Awe pia na mahusiano mazuri na mikoa yote ya Tanzania. Awe pia na mahusiano mazuri na wachagga.

Saa100 pamoja na bunge, wanaweza wakapitisha sheria ya kuruhusu urais kuwa term tatu, za miaka mitano kila term. Au urais kuwa term mbili, za miaka sita kila term. Wabunge na madiwani wawe na terms za miaka sita, na sio mitano kama ilivyo sasa.

Kwa sasa hii inawezekana, as karibia bunge lote ni ccm. Term za miaka 6, zitapunguza gharama za uchaguzi mkuu.

Miaka saba hapana, ni mingi sana.

TZ diaspora walio acha uraia wa Tanzania, wapewe muhuri wa permanent resident (au permanent leave to remain), kwa urahisi sana, kwenye passport zao mpya za kigeni. Wanaweza pia wakapewa special status, ambayo pia ita include hayo hapo juu.

Umri wa kukana au kuchagua uraia kwa watoto wa kiTZ wenye fursa ya uraia wa zaidi ya nchi moja, uwe ni miaka 30, na sio miaka 18 kama sasa.

Hii itawawezesha watoto hao wa kiTZ kunufaika na elimu nzuri na ya gharama nafuu hadi chuo kikuu, huko ughaibuni.

Umri wa chini wa kuruhusiwa kufanya vitu ambavyo sio vizuri, upandishwe kutoka miaka 18 hadi miaka 21, kama matumizi ya pombe/alcohol, sigara/tobacco/shisha, kamari/sportsbetting/casino/lottery, kwenda disco/nightclub, cinema za miaka 18 huko nje, hapa ziwe ni miaka 21.

Pia shisha au na aina zote za kamari, ziwe regulated au banned, kama vimekuwa out of control.

Umri wa kupiga kura ushushwe na uwe ni miaka 15. Umri wa kufanya kazi nyepesi uwe ni miaka 15. Umri wa kufanya kazi nzito uwe ni miaka 21.

Umri wa kuruhusiwa kujiunga na majeshi uwe ni miaka 21; wakati wa vita, umri huo unaweza kushuka na kuwa miaka 18.

Umri wa kuoa au kuolewa, na wa kuruhusiwa kufanya mapenzi uwe ni miaka 21. Watu wenye umri wa miaka 18, wataweza kuoa au kuolewa kwa ridhaa ya wazazi.

Umri wa kuendesha gari uwe ni miaka 18 (class B na D). Umri wa kuendesha magari makubwa uwe ni miaka 21.

Saa100, inabidi aendelee na concept ya TZ as a developmental state.
 
Tapeli wa kisiasa tu huyo
 
Nahukuru kwa vile umenisaidia kujibu, mimi nilisoma nikamdharau.

Watu wa kaskazini wana ukabila wa kijinga sana ( wengi wao wachaga lkn sio wote)
 
Ushauri wa kijinga, huzingatii uwezo wa mtu bali dini
 
Mbunge hapeleki maendeleo jimboni acha upotoshaji.
 
Amenyoa kwanza? Sio anasimama kwenye hadhara ya watu huku na afro.
 
CCM ilimvua uanachama mzee Duni Haji na hayati Seif Sharrif Hamad....

Ikaendelea kwa akina Sofia Simba na Madabida's.....ukifanya makosa makubwa ya kudhalilisha malengo makubwa ya chama kamwe hawakuwachi uendelee kuwa mwanachama....kosa liko wapi hapo ?!!

Kufanya ukaidi wa kukosoa mambo ya ndani ya chama ukiwa nje kwa wasiohusika na vikao vya chama ni kosa kubwa mno.....

CCM wanakosoana ndani na si nje....huko ni kukosa nidhamu na uungwana......

Mwenyezi Mungu aendelee kumlinda na kumhifadhi mwenyekiti wa chama aliye na kofia mbili ,aaamin aaamin !!
 
Reactions: Tui
Muulize Tulia Ackson
Uongozi wa TL utakuwa wa kifukara haswa....ule umoja wa kisiri wa kukusanya fedha kutoka kwa wafanyabishara wa Kkoo kila mwezi umeanza kutikisa.....wako wanaosema hawawezi kukusanya fedha zao kukipatia chama kinachoongozwa na mtu asiyejua malengo makubwa ya kuanzishwa CDM...ha ha ha ha
 
Sasa unaanza kuja kwa adabu na tunaweza kuzungumza kidigo,

Huyu dr Malisa aliesema wazi kwamba uchaguzi wa kumpititisha mgombea wenu wa ccm ni batili na umevunja katiba ya chama chenu ,mmemfukuza kwa lipi?

Ccm mnazidiwa na vichaa wanao zurula mitaani , safari hii mtajua hamjui , kajichagueni sasa tuone
 
Lissu hapendagi dharau anaweza kuamua kugombea ubunge amgaragaze🤣🤣🤣
 
Umenikaribisha na kunisifu halafu unanitukana kuwa ninazidiwa na vichaa wa huko majalalani ,duuh....

Alifukuzwa hayati Bernard K.Membe kwa hayo hayo aliyoyafanya Dr.Malissa.....

Alifukuzwa balozi Dr.Ali Karume kwa kumdhalilisha na kumbagua Rais Dr.Hussein Mwinyi....

Narudia tena ,Dr.Malissa alitakiwa kukosoa akiwa ndani ya vikao husika....na si kitendo kisicho na uungwana huku nje kwa wasiohusika ... .
 
Wrong Calculation: Jana Katibu Mkuu Balozi Dkt Nchimbi katoa ONYO, Leo Yeye anatumia sherehe kufanya yaliyokatazwa alafu wakati huo hata kadi ya Chama hana, CCM sio nyepesi kiivyo anavyodhani. CCM sio Kila mtu kambare.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…