Mbunge wa Tandahimba kupitia CUF, Katani Katani ajiuzulu na kujiunga CCM

Mbunge wa Tandahimba kupitia CUF, Katani Katani ajiuzulu na kujiunga CCM

1582346705648.png


Mbunge wa Tandahimba, Katani Ahmed (CUF) amejiuzulu kiti chake na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Ijumaa, Februari 21, 2020. Ahmed ametangaza kujiunga na CCM akiwa katika mkutano wa ndani wa chama hicho tawala katika Jimbo la Nanyamba mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally.

Huu ni mwendelezo wa viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani kutangaza kuhamia CCM wakieleza kuwa ni kutaka kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano.

Mapema wiki hii, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji alitangaza pia kuhamia chama tawala akieleza sababu kuwa ni kuchoshwa na malumbano yasiyoisha ndani ya chama kikuu cha upinzani. Aliyekuwa Mbunge wa Ndanda, (Chadema) Cecil Mwambe pia alitangaza kujiuzulu uanachama wa chama hicho kikuu cha upinzani na kuhamia CCM wiki iliyopita.
 
Ni wazi wengi wa hawa wanaohama hama sasa wanatambua kuwa hawataweza kugombea katika uchaguzi ujao kutokana na ile sheria iliyolitishwa na serikali ya kikaburu chini ya ccm ile ya kutimiza mwaka mmoja chamani. Je, hawataki tena kuwa wabunge? Ni wazi wanataka, ila hawaamini kuwa kaburu huyu ataruhusu uchaguzi wa huru na wa haki kwani mifano ya chaguzi ndogo na ule wa serikali za mitaa wanayo.

Kwa nini wanafanya haya ya kuhama? Ni wazi kuwa wanafahamu kuwa kaburu huyu haheshimu sheria au anaweza kutunga sheria nyingine ya kikaburu kuwapa favour hawa wahamaji au kuwakumbuka katika teuzi zake za UDC, uRAS na kila aina ya teuzi zinazoendelea kila uchao.
 
Kwanini wasifanye utaratibu wa kukieneza chama na itikadi yao kwa wananchi ili maelfu wakikikubali chama na kujiunga nacho?

Hii ya mtu mmoja ama wabunge 3 au 10 tu kujiunga na CCM why be a big deal?

CCM inahitaji support ya wananchi zaidi ili iache tabia ya kuiba kura na kutumia vyombo vya dola (polisi, TISS, mahakama na JWTZ) nyakati za chaguzi kupora kwa nguvu ushindi wa washindani wao...

This strategy is not sustainable and surely, soon it might not function anymore. Your end (CCM) is disgraceful coming to an end....!!
 
Yaani eti MTU kama huyu Leo anaunga mkono ukandamizaji huo huo uliomtoa machozi majuzi bungeni? Ni dalili kuwa hana jina lingine linalomfaa zaidi ya laghai na kahaba wa kisiasa.
Hii ni aibu kwake, mkewe na familia nzima. Na sio ajabu kuna siku hata wao wanaweza kuja kumkana kabisa mtu laghai kama huyu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom