Baraka Mina
JF-Expert Member
- Sep 3, 2020
- 586
- 590
Mbunge wa viti Maalum (CCM) mkoa wa Rukwa Ndg. Irene Ndyamkama amefariki dunia leo tarehe 24 Aprili 2022 katika hospitali ya Tumbi mkoani Pwani alikokuwa akipatiwa matibabu.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson ametangaza kifo hicho na kutuma salamu za pole kufuatia msiba huo.
“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mheshimiwa Irene Alex Ndyamkama, Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, waheshimiwa wabunge na wananchi wa Mkoa wa Rukwa. Mwenyenzi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu,” amesema Spika Tulia.
Mipango ya mazishi ya Ndg. Ndamkama inaratibiwa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya marehemu na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson ametangaza kifo hicho na kutuma salamu za pole kufuatia msiba huo.
“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mheshimiwa Irene Alex Ndyamkama, Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, waheshimiwa wabunge na wananchi wa Mkoa wa Rukwa. Mwenyenzi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu,” amesema Spika Tulia.
Mipango ya mazishi ya Ndg. Ndamkama inaratibiwa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya marehemu na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.