TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

katika Vitabu vitakatifu Mungu amekuwa akitoa ishara nyingi nyingi sana. Na hii leo anasema na Watanzania kwa namna tofauti kabisa ya kuondokewa na mwanasiasa mwenye chachu kabisa katika Siasa za Vyama vingi. Hebu kaa dakika moja mkumbuke Mch.Mtikila, Kumbuka siasa za Mtanganyika, Kumbuka siasa za --------- na mengine mengi.

Mungu anasema kwa ishara mabalimbali kipindi hiki cha uchaguzi, matukio mengi sana yametokea hapa Tanzania na duniani yakitukumbusha sisi ni mavumbi tu. Nikipindi ambacho Tunakumbushwa kurudi Miskitini na makanisani kusiliza sauti ya Mungu na kuzitambua ishara hizi kwa unyeyekevu mkubwa. Mungu anatukumbusha kujali maskini,Watu wenye njaa, na wagonjwa mbalimbali. Mungu anatukumbusha si kwa akili zetu tumepata dhamana kuliongoza taifa hili bali yeye mwenyewe ndio kafanya yote haya.

Mungu anatukumbusha Gas Mafuta na madini ni mali yake na vitumie kwa utukufu wake kwa kuhudumia watu wenye mahitaji zaidi. Mungu anatukumbusha Mikataba ya madini/Gas iwekwe wazi ili iwafikie walengwa wake. Mungu anatukumbushaTuache rushwa na ufisadi,Tutubu zambi zetu na Tujenge taifa kwa kizazi kijacho.

Mungu ameota ishara hizi ila kila mwanadamu apate kumjua yeye ndie Mungu Muumba wa Taifa hli.
1.Lowassa Kuhama CCM
2.Magufuri kuwa Mgombea Urais
3.Lipumba Kuacha siasa
4.Dr Slaa kuacha Siasa
5.Halima mdee na Mbatia kwenye Jukwaa moja.
6.Tanzania kuwa giza wakati wa uchaguzi
7.Vyama vinne kusimamisha mgombea
8.Rais kupiga campaign
9.Hotuba za Nyerere kutamba katika jukwaa la upinzani.
10.Kwa mara ya kwanza Watanzania hawajui nani atashinda uchaguzi.
11.Campaign bila kept.Komba.
ukiangalia kwa mbali utaona ni vitu vidogo sana lakini ukirudi utakuta mabadiliko makubwa sana katika radha ya siasa za Tanzania. kwa ujumla kifo cha mtikila ni pigo zito sana katika radha ya siasa ya vyama vingi. R.I.P

Halafu wee kama nakufahamu vile...
Arusha member? Umesoma arusha sec?
 
Maisha ya mwanadamu nikama mshumaa na upepo, wakati unawasha mshumaa kupata mwangu hujui kama utazima punde upepo utakapo pita. Siku zote usipende kuingilia majukumu ya Mungu kuwa ww ndio unapangia wenzio vifo kana kwamba utaishi milele, sote tu wasafiri hatujui siku wala saa ya kufa tunajua siku ya kuja duniani tu ila siku ya kuondoka bado ni fumbo zito alilokuwa nalo mungu pekee. Wale wote wanao mnyooshea Lowassa kidole kimja kuwa ni mgonjwa wajiulize vidole vingapi viinawageukia wao, hakuna mtu anayependa kuwa na maradhi usimhukumu mtu kwa maradhi yake. Mfano mzuri ni ule wimbo wa Enzi zile kipindi cha RTD salamu kwa wagonjwa kila j2 saa 3 asubui :"WAKATI UMEWADIA KWA SALAMU KWA WAGONJWA LEO TUNAWAPA POLE... AJUAYE BWANA MUNGU KUWA MZIMA KUWA MFU NA MGONJWA KUWA SALAMA LEO TUNAWAPA POLE" kamwe kuugua sio kufa na kufa sio kuugua. Hope wenye kujifunza watakuwa wamejifunza jambo
 
mungu hutujalia afya na uhai....mungu hapendi kazi zake zidhihakiwe na mwanadam.......mtikila aliingilia mambo ya afya ambayo tunajaliwa na MUNGU. nI MUNGU PIA AMBAYE AMEAMUA KUMWITA MTIKILA MAPEMA tusimdhihaki kama yeye alivyotidhihaki alipokuwa hai na buheri wa afya
 
Kama huwezi kujibu kwa ustaarabu bora upite tu, hujui kama alifungua kesi na kama angeshinda angerudishwa kugombea?
Kabla hujamwaga uharo wako mbele ya kadamnasi jaribu kuwa unauliza jirani zako kwanza!
 
Wajuzi wa sheria hebu tufahamisheni kuhusu hili, baada ya kifo cha Mchungaji mtikila ambae alikuwa mgombea urais wa chama cha DP je sheria inasemaje kuhusu uchaguzi? Utaakhirishwa au inakuwaje?

Nakumbuka miaka ya nyumba alipofariki Marehemu Dr Omar Ally Juma aliekuwa mgombea mwenza wa ccm uchaguzi uliakhirishwa vipi kuhusu la mtikila?

Wewe nawe akili yako sijui ikoje? Nani alikwambia kwamba kuna mtu anaitwa Mtikila kwenye orodha ya wagombea u-Rais? Uchaguzi uko pale pale!! Naona mleta mada ulikuwa bado unanyonya wakati Dr. Omary Ally Juma akifariki! Maana kipindi hicho hapakuwa na uchaguzi wowote! Elimu yetu ina shida mahali!!
 
[COLOR=#ff0000 said:
Mr Hero[/COLOR];14217162]Wajuzi wa sheria hebu tufahamisheni kuhusu hili, baada ya kifo cha Mchungaji mtikila ambae alikuwa mgombea urais wa chama cha DP je sheria inasemaje kuhusu uchaguzi? Utaakhirishwa au inakuwaje?

Nakumbuka miaka ya nyumba alipofariki Marehemu Dr Omar Ally Juma aliekuwa mgombea mwenza wa ccm uchaguzi uliakhirishwa vipi kuhusu la mtikila?
Wewe ni Mr. Hero au Zero?!!
 
Marehemu mtikila angekuwepo yupo hai na hili swala la kifo lingetokea kwa mgombea mwingine hakika pangechimbika na angeenda mahakamani yule mzee enzi za uhai wake alipenda sana kesi.
 
Mwana wew unapost kutoka antactic ukiwa umezungukwa na penguin! Sio bure hii
Wajuzi wa sheria hebu tufahamisheni kuhusu hili, baada ya kifo cha Mchungaji mtikila ambae alikuwa mgombea urais wa chama cha DP je sheria inasemaje kuhusu uchaguzi? Utaakhirishwa au inakuwaje?

Nakumbuka miaka ya nyumba alipofariki Marehemu Dr Omar Ally Juma aliekuwa mgombea mwenza wa ccm uchaguzi uliakhirishwa vipi kuhusu la mtikila?
 
Ni ukweli unaouma sana kuondokewa na mtu ambaye pamoja na mapungufu yake lakini mimi nilikubaliana nae katika harakati zake za kuirejesha Tanganyika huru na kuvipa uhuru visiwa vya Zanzibar kutoka kwa mamumiani walioko Zanzibar na huku bara kwa kuvididimiza kimaendeleo visiwa vya Zanzibar kwa muungano usio na kichwa wala nyayo. Pamoja na hayo natanguliza neno;kapumzike kwa amani Mch. Christopher Mtikila kwani sote tutapita njia hiyo hiyo japo kwa style mbalimbali. Niliangalia na kusikiliza siku ndugu yetu akihojiwa na kituo cha Startv kuhusiana na mgombea wa UKAWA. Aliyoyaongea hakika kama angelikuwa ashawahi kusikia kibao matata chenye ujumbe wa kuogopesha kiitwacho; Yellow Card cha Freddy Ndala Kasheba (marehemu) hakika ndugu yetu marehemu Mtikila asingegusia hata kidogo mstakabari wa afya ya binadamu aliyeumbwa na mungu. Ndala Kasheba anasema; zamani niliimba dunia msongamano leo naimba dunia matatizo, miaka ya 80 walitangaza nimekufa mwaka 2000 wamesema niko mahututi Kishansha!, nimeshazoea, kila kukicha kusikia bwana maarufu ana matatizo! Magojwa yote ya dunia nimepachikwa mimi, wafurahi wao, wenye uhakika wa afya njema ooohh,wataishi mileleeee........................ (Anaendelea) yote nakubali namwachia mungu aliyeniumba anajua mwisho wa maisha yangu, mungu ndiye mwamuzi, atanipa kadi, yellooooow kadi itakuwa ni onyo na kama red kadi niondoke duniani yote ni yamungu..…..................... Eti jamaa yuko hoi,hamalizi mwaka anaondoka huyo,tumpeleke tumpelekeeee. Watoto yatima,walemavu wasiojiweza mlo mmoja hawapati.....................kufa kwa binadamu hupagwa na mungu.......dunia msongamano. hata nikifa sitamaliza vifo wala kujaza ardhi, nitakwenda kwenye kaburi langu mwenyewe, usiwe na wasiwasi nawe lakwako lipo,sababu na wewe ni marehemu mtarajiwa linakusubiriiii. (anaendelea)...amekufa masiha,wamekufa mitume na masultani watawala wenye sifa kubwa na pesa nyingi, sembuse mimi na wewe viumbe dhaifu,jamani tuhurumiane!! Dunia maajabu!! Ina matatizoeeee. DUNIA NI HII HII
 
Alisema jamaa atafia ikulu akataka kumshtaki, hivi na mimi nikisema jamaa atafia kwenye gari naweza kumshtaki?
 
Ni vigumu kuamini! Mchungaji! Christopher Mtikila aliyefariki dunia juzi usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha Msolwa Wilayani Bagamoyo, Pwani jumatano ya iliyopita aliyembelea ofisi za gazeti hili(IJUMAA), Bamaga, Mwenge na kuzungumza na wandishi wa gazeti hilo,
Alipoingizwa chumba cha maongezi hakuwa tayari kufanyiwa mahojiano maalum kwa siku hiyo akasema atapanga siku ya kufanya hivyo baada ya kujiandaa.
Alipotakiwa aseme neno kuhusu uchaguzi ujao alisema:
"Napenda kusema jambo moja muhimu: MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI, JAJI DAMIAN LUBUVA NA MGOMBEA URAIS WA CHADEMA, EDWARD LOWASSA NI MTU NA MKWEWE. REGINA LOWASSA NI MTOTO WA KAKA YAKE JAJI LUBUVA, HIVYO LOWASSA NI MKWE WAKE, HILI WATU WANAPASWA KULIJUA"
Hata hivyo , Jaji Lubuva alipoulizwa na mwandishi wetu kama madai hayo yana ukweli au la alisema, NI KWELI YEYE NA REGINA LOWASSA WANATOKA SEHEMU MOJA, KONDOA MKOANI DODOMA lakini AKASHINDWA KUKUBALI AU KUKANUSHA kuhusu taarifa hizo kama wana undugu.
Source: Ijumaa

20151005_090229.jpg
 
Mengi yatafichuka. Damu ya Mtikila haiwezi kumwagika bure
 
sasa tufanye hatuna uwezo wakumrudisha tena ndiyo kashaondoka jumla kifo ni lazima na siyo hiyari !!!
 
Kila jiwe litageuzwa mwaka huu lakini yaliyoandikwa lazima yatimie na yatimie kwa wakati sahii na pahala sahii...
MTEULE ANAKUJA TANZANIA YENYE NEEMA INAKUJA.
 
Mimi nilifika eneo la tukio jamani ni ajali tena mbaya. Gari lilipinduka wakati dereva anajaribu kuzuia asigongane uso kwa uso na gari jingine baada ya Ku overtake kimakosa...
 
Kweli mwacheni Mungu aitwe Mungu, yeye anaijua kesho yako na aliijua kesho yetu watanzania na ndio maana akafanya vyovyote mtikila akakosa kugombea urais kwa kukosa mgombea mwenza, nimejiuliza sana inamaana nakumchoka kote huku kikwete na ccm yake tungelazimika kuongeza mda wa kukaa madarakani kikwete wa siku 90? ee mwenyezi Mungu ahsante kwa kugundua watanzani tumechoka na utawala huu dhalim na tunataka kuupumzisha haraka iwezekanavyo
 
Kaka yangu Lizaboni, huyu Mtikila ninayemjua mimi na alivyokuwa na majina ya ajabu toka pande zenu mbili za kisiasa (UKAWA na CCM) leo kawa shujaa kiasi hiki? Tusubiri na wenzako wa upande mwingine wanasemaje!! Watanzania na ifike hiyo 25 October tupumzike.

Mengi yatafichuka. Damu ya Mtikila haiwezi kumwagika bure
 
Back
Top Bottom