Mchakato Katiba Mpya: 44% wanasema maoni yao hayakuwekwa kwenye Katiba iliyopendekezwa

Mchakato Katiba Mpya: 44% wanasema maoni yao hayakuwekwa kwenye Katiba iliyopendekezwa

Hilo bunge lilikuwa mkusanyiko wa taasisi na mafisadi wa CCM, wakitetea wizi wao kina Chenge.
Polepole leta mezani rasimu bora ya Mzee Warioba.
Tengeneza katiba bora ya Watanzania.
Hila mbinu chafuu
hazitatusaidia!!
Sawa kabis unavyosema lakini hiyo ndio mshahara wa watu wanaosusa susa kama watoto wakike au wadogo. Waliosusiwa wameamua kufanya vile kutokana na mawazo yao na kile wanachokitaka. Hata ingekuwa wewe.
Wale wana haki ya kutoa maoni yao hata kama wengine hawayakubari, sababu mchakato ule ulikuwa unawapa uhuru huo na kumbuka haikusemwa mawazo ya wananchi yatakuwa ya mwisho.
So, hao unao washutumu wewe naona wapo sahihi kwa upeo wao ulipoishia kuliko wale walio susa na kutoka nje.
 
Kama ni kuendelea pale bunge la katiba lilipoishia, yaani kupigia kura katiba iliyopendekezwa na bunge la katiba, bora kuachana na kitu kicho kabisa,
Kinachotakiwa ni kurudi nyuma kabisa:
Kwanza tufute mabadiliko ya sheria ya mchakato wa mabadiliko ya katiba - mabadiliko ambayo yaliiondoa tume ya Warioba kusimamia kura ya maoni na kuipa tume ya uchaguzi madaraka hayo (mabadiliko hayo yalilenga kuficha matokeo halisi ya kura za wananchi kwa kuwa tume ya uchaguzi si tume huru)
Pili, katika sheria ya mwanzo ilikuwa kama wananchi wataikataa katiba waliyopelekewa kuipigia kura, basi tume ya Warioba ilitakiwa irudi tena kwa wananchi kuwauliza ni kwanini wameikataa katiba hiyo na marekebisho gani wanayataka, Hivyo marekebisho yaliyofanywa kuwa wananchi wakiikataa katiba watakayokuwa wapelekewa waipigie kura basi Katiba ya zamani iendelee, yafutwe (Mabadikliko haya yalilenga kuwalazimisha wananchi kuikubali katiba mpya hata kama ina mapungufu mengi, vinginevyo wataendelea na katiba ya zamani, Hiki ndicho kiini cha kuchomeka vipengele visivyofaa katika katiba pendekezwa!)
Tatu, bunge la katiba lisihusishe wabunge wa bunge la kawaida maana hao wamechaguliwa kwa utashi wa vyama vyao na hivyo wanatumiwa kulinda maslahi ya vyama badala ya maslahi mapana ya wananchi.
Nne, wajumbe wa bunge la katiba wawekewe masharti magumu ya kugombea uongozi wa kikatiba baada ya kupatikana katiba mpya, hii itasaidia wabunge hao kutopitisha katiba kwa maslahi binafsi, Nakumbuka kuna nchi wajumbe wa bunge la katiba na familia zao na ndugu wa karibu walizuiwa kugombea nafasi za kikatiba kwa muda fulani
 
kasome tena mchakato wakatiba ulivyo!

hiyo iliyopendekezwa ikikataliwa, bunge linaitishw atena then wanakwenda kukubaliana, then kura tena, ikkataliwa basi tunarudi ya zamani.
Na hapo ndipo upuuzi ulipo,wananchi wakiikataa siyo kurudishwa tena bungeni, Inabidi wananchi waulizwe sababu za kuikataa na wapendekeze marekebisho wanayohitaji; baada ya hapo irudishwe kwa wananchi kwa kura.
Kuna mantiki gani eti wakiikataa katiba mpya basi warudi ya zamani - kwani maoni yao walitoa ya nini? Hapa ndipo kuwachezea wananchi yaani wanatuletea katiba pendekezwa mbovu iliyochakachua maoni yetu ili tukiikataa wabaki na ya zamani - shame kwa wote waliobadilisha sheria
 
Na hapo ndipo upuuzi ulipo,wananchi wakiikataa siyo kurudishwa tena bungeni, Inabidi wananchi waulizwe sababu za kuikataa na wapendekeze marekebisho wanayohitaji; baada ya hapo irudishwe kwa wananchi kwa kura.
Kuna mantiki gani eti wakiikataa katiba mpya basi warudi ya zamani - kwani maoni yao walitoa ya nini? Hapa ndipo kuwachezea wananchi yaani wanatuletea katiba pendekezwa mbovu iliyochakachua maoni yetu ili tukiikataa wabaki na ya zamani - shame kwa wote waliobadilisha sheria


Mpoka ikataliwe mara mbili na wananchi.
 
Christina Kamili(Jukwaa la Katiba): Katiba ya Warioba ilibeba maslahi mapana ya wananchi hasa mgawanyo wa mihimili 3 ya Serikali [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Mchakato wa marekebisho ya Katiba ulipitia awamu 3. Awamu ya kwanza ilikuwa ya kuundwa Tume ya marekebisho chini ya Jaji Warioba
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Miongoni mwa mambo yaliyopendekezwa ktk rasimu hii ni kubadilisha muundo wa sasa wa Serikali 2 na kuanzisha muundo wa Serikali 3
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Bunge Maalumu la [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] lilipitisha rasimu hii Oktoba 2014, pasipo kujali kujiondoa kwa wajumbe waliounda umoja uliojulikana kama UKAWA

93% ya Watanzania wameshawahi kusikia kuhusu Katiba, lakini kati yao 58% hawafahamu Katiba ni nini
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

22% - Ni mkusanyiko wa kanuni zitumikazo kuongoza nchi
12% - Ni azimio la kisheria litumikalo kuongoza nchi
1% - Azimio la haki za wananchi


Uelewa wa Katiba ni mkubwa miongoni mwa wenye elimu ya Sekondari na ya juu(49%) kuliko ambao hawajahitimu elimu ya msingi(22%)

Uelewa wa Katiba ni mkubwa miongoni mwa wenye umri > miaka 50(45%) kuliko wenye < miaka 30(29%) - Matajiri(40%); masikini (28%)

Uelewa wa Katiba kati ya wanaume na wanawake: 47% ya wanaume waliweza kueleza maana ya Katiba, ukilinganisha na 22% ya wanawake

44% wanasema [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] iliyopo inatekelezwa ipasavyo, 46% wanasema inatekelezwa “kwa kiwango fulani”. 4% tu wanasema “haitekelezwi ipasavyo”


Waliosema [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] inatekelezwa ipasavyo walisema ni kwa sababu sheria zinafuatwa (22%) au kutokana na kwamba uongozi ni mzuri (12%)
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Waliosema “inatekelezwa kwa kiwango fulani” walieleza kuwa kuna baadhi ya vipengele vya Katiba(15%) au Sheria(12%) ambavyo havifuatwi
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

71% ya wananchi wanafahamu kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa [HASHTAG]#Tanzania[/HASHTAG] ilianzisha mchakato wa mabadiliko ya [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] yake
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Uelewa wa mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] ni mkubwa miongoni mwa wanaume (81%) ukilinganisha na wanawake (61%) [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]


Uelewa wa mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] ni mkubwa miongoni mwa wenye miaka zaidi ya 50 (81%) kuliko wenye umri chini ya miaka 30 (63%)
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Wananchi 2 kati ya 3(67%) wanasema maoni ya wananchi hayajatokea kwenye rasimu ya [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] iliyoandaliwa na Bunge Maalum la Katiba [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]


23% ya wananchi wanasema mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] kwa kiasi kikubwa ulikuwa ni
kuwapa taarifa kuliko kuruhusu wananchi kutoa maoni yao
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

44% ya wananchi waliona mchakato huo uliwapa fursa wananchi kutoa maoni yao, lakini hayakutumika kwenye rasimu ya [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

59% ya wananchi wanasema Bunge Maalumu la [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] liliwawakilisha vema watanzania ktk mchakato huo
- 38% hawakubaliani na kauli hiyo
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Mwananchi mmoja kati ya wanne(23%) wanaunga mkono UKAWA kususia Bunge Maalumu la Katiba na kugomea mchakato wa kupitia [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]
[HASHTAG]#szw[/HASHTAG]


56% ya wananchi wanasema kutoka nje kwa UKAWA hakubatilishi mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] ; 41% wanasema kitendo hicho kinabatilisha mchakato
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

48% ya wananchi wanasema njia nzuri ya kufufua mchakato wa mabadiliko ya Katiba ni kuanza mchakato huo upya na tume mpya
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]


Wananchi hawakubaliani na mabadiliko mengi yaliyofanywa na Bunge la katiba chini ya M/Kiti kamati ya uandishi [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG], Ndugu Chenge
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

79% hawakubaliani na kuondolewa kifungu kinachotaka mawaziri kupitishwa/kukataliwa kwa kura bungeni baada ya kuteuliwa na Rais
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]


Ado Shaibu kutoka Chama cha ACT-Wazalendo: Kwa Ripoti hii ya Sauti za Wananchi iliyotolewa na TWAWEZA ni dhahiri kuwa wananchi wanahitaji [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]


Ado Shaibu(ACT): Rais Magufuli hakusema mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] haufai bali alionesha wazi kuwa si kipaumbele cha Serikali Awamu ya 5
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Ado Shaibu: Utafiti huu umebainisha kuwa kuna pengo kubwa kati ya Wanawake na Wanaume katika uelewa wa mambo nchini
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG] [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Ado Shaibu: Mchakato mzima wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] unaonesha [HASHTAG]#SautiZaWananchi[/HASHTAG] zimezimwa
- Wananchi wametaja vipengele walivyopendekeza na vikatolewa

Ado Shaibu: Wapinzani tunafanya makosa ktk kujifungamanisha na Wadau wakuu ambao ni wananchi
-Wananchi wengi hawaijui UKAWA
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG] [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]


Polepole(CCM): Watanzania kwa takwimu hizi za Twaweza wanataka kuona Ukatiba(constitutionalism) kuliko Katiba(constitution) nchini

Polepole: Watu wa kawaida wanataka viongozi waadilifu, wasiokula rushwa, wanaojua cheo ni dhamana; huo ndio Ukatiba [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Polepole: Ukatiba ni kuwekeana mifumo hata kama haikuandikwa mahali. Kila mtu akielewa hii mifumo hakutokuwa na tatizo
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Polepole: Tunaweza kuandaa Katiba na kuiweka kwenye kitabu lakini bila Ukatiba hakuna atakayeifuata
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Mchakato wa katiba uko na hatua tatu:
1. Kukusanya maoni na kuandaa rasimu;
2. Rasimu kujadiliwa na Bunge la Katiba na;
3. Kaiba Pendekezwa kupigiwa kura na wananchi wapiga kura.
Sijui ni kwa nini baadhi ya watu wanataka tuanze moja! Je, ni kwa sababu UKAWA walisusia mjadala kwenye Bunge La Katiba? Je, ni kwa sababu kipengele cha ulaji na kuwagawa Watanzania kwa kuwa na serikali tatu kiliondolewa? Je, ni kwa sababu wasaka tonge walikwamishwa kwa kipengele cha ghiriba na fitina cha kuwaondoa wabunge, eti kwa sababu ya kutokuwatumikia wananchi vyema ndani ya muhula wa utumishi wao?
Kama alivyosema Ndugu Polepole, cha msingi ni namna ya kuwa na viongozi wenye sifa zilizotukuka za kutumikia wananchi hata bila ya Katiba. Hebu tafakari kwa mfano, tunazo sheria nzuri dhidi ya uhalifu wa ulaji rushwa au uhujumu uchumi, je, ni kwa namna gani zimezuia watu kutoa na kupokea rushwa au kuhujumu uchumi wa nchi?
Kimsingi, nadhani ni vyema mchakato ukaendelea ulikoishia. Kumbukeni kwamba, kuna kipindi cha miaka minne ya matazamio baada ya kupitishwa ambacho kinaweza kutumika kutathmini mapungufu na kuifanyia maboresho!
 
Mimi nimeshangaa sana kuhusu kujua na kueleza maana ya katiba kati ya wanaume na wanawake, kumbe wanawake uelewa wao uko chini hivyo. Pia, wale wenye elimu ya darasa la saba, uelewa ni mdogo MNO wa katiba. Nilichofurahi ni kuwa WETU wengi kama 67% wanasema mambo mengi yaliachwa kwenye
 
Maoni ya TWAWEZA huwa yanachkuliwa toka kwa watu gani maana sijawahi sikia mtu mtaani kahojiwa na na hao watu ila kila siku wanatoa tafiti zao
 
Tunahitaji Katiba Mpya, hapa tulipokwama hakuna kiongozi au mtu mmoja anaweza kutukwamua.

Rais Magufuli ni mtawala mwenye nguvu katika mfumo dhaifu....na hilo litaweza kupata suluhu kwenye Katiba.
 
Kumpunguzia madaraka Rais ni kuruhusu nchi 'kuliwa' zaidi... Leo hii nchi imefikia pabaya sio kwa sababu ya udhaifu wa katiba bali ubinafsi.. Acha kidogo hiki chuma kinyooshe mambo then tutazungumza upya kuhusu hiyo rasimu pendwa tukishakaa mguu sawa!
Katiba mpya inahitajika japo siyo leo jiulize nani wenye akili ya kimungu wa kutengenezea katiba itakayo lipeleka taifa mbele kwa karne nyingi? Leo ukitaka maoni ya wanaoitwa wananchi utakuta siyo wananchi bali akili zao ziko kivyama.
 
Mimi nimeshangaa sana kuhusu kujua na kueleza maana ya katiba kati ya wanaume na wanawake, kumbe wanawake uelewa wao uko chini hivyo. Pia, wale wenye elimu ya darasa la saba, uelewa ni mdogo MNO wa katiba. Nilichofurahi ni kuwa WETU wengi kama 67% wanasema mambo mengi yaliachwa kwenye
Usomeshe wanao wa kike mkuu. Gepu kati ya gender mbili ni kubwa sana...
 
Back
Top Bottom