Hapana, hao wanaoleta mrejesho wanatokea maeneo ambako kuna Kilimo cha mahindi ndiyo maana wanazungumza habari ya kuweka mbolea! Mavuno waliyozungumzia ni ya kawaida kabisa! Wilaya ya Tanganyika wanalima bila mbolea lakini hawakosi magunia 15-20 kwa ekari. Changamoto ya kubwa ni udhibiti wa post harvest losses, mazao mengi yanapotea wakati wa uvunaji. Unakuta mahindi yanaoza kutokana na wingi wa mvua!Pole sana,hawaweki wazi changamoto ya hali ya hewa.
Kilimo cha mezani.Mzee we umefanya?
Kilimo cha kwenye karatasi safiii Sana
Hujataja ghalama za Mbolea. Heka moja inahitaji wastani kilo 200 za mbolea. Mfuko wa kilo 50 unauzwa wastani 100,000 x 4 = 400,000.Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-
Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-
Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Shukrani bro...barikiwa sana...Wakuu Saluti,
Ngoja niwape experience yangu ya Kilimo cha Mahindi Mkoa wa Ruvuma kwa Wilaya ya Mbinga.
1. Kukodi shamba 50,000 - 100,000 inategemea mahali na mahusiano na mwenye shamba.
2. Kulima kwa trekta 60,000, Kwa kutumia vibarua ni kadiri ya makubaliano lakini ni kuanzia 45,000 hadi 70,000
3. Mbegu inategemea na aina ya mbegu ila Mbinga maarufu ni Mbegu aina ya Tembo ya Zambia gharama ni kuanzia 15,000 hadi 20,000 kwa paketi, hapa utahitaji paketi 6.
4. Kupanda, zipo njia mbili. Kwa kutumia vibarua ambapo ni kati ya 4000 -7000 kwa kibarua au kwa kutumia mashine ya kupandia ambapo utalipa kati ya 20,000 hadi 25,000
5. Mbolea hapa utaweka mifuko 5 - 6 kwa awamu mbili (2.5 - 3 kwa awamu). Mbolea maarufu huku ni UREA 70,000/= CAN 65,000/= na SA 55,000/= kwa bei ya ruzuku. Au kama utapata mbolea aina ya YaraMila Cereals hiyo ina mchanganyo wa mbolea zote hizo tatu.
6. Kuweka mbolea, utalipa vibarua kwa kila awamu kwa gharama ya vibarua ambazo ni kati ya 4000 - 7000
7. Palizi ni 30,000 hadi 45,000 kwa hekari. Au unaweza kupiga dawa hapa gharama itategemea aina ya magugu yaliyopo shambani ndio ita-determine gharama ya dawa na bei zake.
Shida ya dawa kuna probability ya kurudia kupiga tena in case haijakubali vizuri na kama mtaalamu ameshindwa kukushauri aina ya dawa kulingana na aina ya magugu lakini pia changamoto nyingine unaweza ukaunguza mazao kunahitajika umakini wakati wa upigaji dawa.
8. Kuvuna na kukusanya mahindi utalipa vibarua in daily basis kwa rate ya 4000 hadi 7000.
9. Kupukuchua mahindi gharama ni 1000 kwa kila kiroba.
10. Matokeo kwa hekari moja kama utafuata hatua zote hizo hapo juu na ukawa haujaathirika na mvua na ardhi ni nzuri hautakosa kupata kuanzia gunia 18 hadi 33.
Gunia moja halitapungua kilo 120 hadi 135 na bei itategemea soko limekaaje. Ila kwasasa bei ni kuanzia 650 hadi 800 kwa kilo.
NB. Bado gharama za usafirishaji, ushonaji wa viroba, kupandisha na kushusha, chakula cha vibarua na gharama za kwenda na kurudi shamba hazijajumuisha.
The higher the expectations the Greater the disappointment. But all in all Mahindi kwa Ruvuma it's a hell of business na kama una mtaji wa kutosha achana na kwenda shambani kulima nenda vijijini weka mzani nunua mahindi.
I hope umepata kitu cha kujifunza.
Nimenote kitu hapamkuu kg 12 za mbegu ni sawa na miche 24,000 kwny eka moja inawezekana japo wengi tupo kwny miche 17,000 kwa spacing ya 30x90cm
Kitu tunachokosea mara kwa mara ni mbolea, kama tuna ambiwa kila mche tuweke grams 5 ya kila mbole meaning 5x24,000= 120,000gm ya mbolea sawa na 120kg = sawa na mifuko miwili na nusu kwa maana hiyo kwa eka 1 utahitaji jumla mifuko 5 ya mbolea.
Hata kwa miche 17,000 bado utahitaji kilo 170 ya mbolea jumla ni karibia mifuko 3.5 Ukiachilia mbali mvua pia nadhan tunashindwa kufanya vzr kwny kilimo kwa kukosa taarifa muhimu zinazopelekea kupata mazao hafifu.
Na anza rasmi kulima mwaka huu ntajitahidi kufata maelekezo yote ya kitaalamu pamoja na kushare taarifa kwa wanavijiji lilipo shamba ili kubalance stories nitajitahidi kuweka hapa jukwaa pendwa
Safi hio ni specific kwa eneo gani na wilaya ipi?
hizo hesabu umepigaje hapo?Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-
Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-
Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Utaelewa tuhizo hesabu umepigaje hapo?
KILIMO cha upupuMchanganuo wa kilimo cha .... Kwa heka Kulima elfu 60 mbegu kilo elfu30 yaitajika kilo 5 kupanda elfu20 kupalilia elfu 30 kuvuna elf50 ikiuza jumla unapata m19 kwa hekar moja unajua kilimo cha nn hicho tulia tunalima wachache
Siku za usoni nitakua mgeni wakoRukwa boss
Kahama kwa mahindi hamna Huwa yanaungua sana labda mpunga ni freshNgoja niweke kambi hapa nawaza huu mwaka ishu za kilimo nifanye,
Kuna mwenye uzoefu wa Kahama kuhusu mvua
Faida ya Tsh 600000 kwa ekari igawe kwa muda uliotumia kusubiri pesa yako irudi.Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-
Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-
Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Kiufupi mbolea lazima mifuko 3 Kwa kiwango Cha chini kabisa ,dawa za Wadudu na wastani wa gharama Kwa ekari 1 ni Kati ya 650k-700k ila una guarantee ya kuanzia gunia 25 kwenda Juu.Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-
Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-
Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Wacha kutisha watu.Ekari 10 zinakupa faida nzuri,hapo ni gunia minimum 250 *50,000=12,500,000 ambapo gharama zote sio zaidi ya 5,500,000.Faida ya Tsh 600000 kwa ekari igawe kwa muda uliotumia kusubiri pesa yako irudi.
Kuanzia mwezi wa kulima (mwezi wa 12 kwa Songwe) mpaka muda ambapo bei ingalau imepanda (Mwezi wa 8)
600000 / 9 = 67,000 TSH (Hii inamaanisha kila mwezi ulikuwa ukiingiza Tsh 67,000 tu ambayo haitoshi kulisha familia).
Ili ufaidike kwenye kilimo cha mahindi inabidi uingize ingalau Tsh 2500000 kwa mwezi
2500000/67,000 = 37 ekari
Inabidi ulime ingalau ekari 35 za mahindi ndo uone faida na kusomesha watoto shule nzuri!
Aksante
Kama unalima Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na Magharibi kuanzia Kagera mvua ni uhakika haijawahi Goma hata siku Moja.Mvua ni ya kwako? Wadudu? Palizi?
Plus Kigoma na Kusini ya MorogoroKwa haraka haraka naweza sema mikoa kama Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya, Rukwa, Katavi, Songwe, Kagera, Kilimanjaro, Arusha, Tanga mvua huwa haisumbui sana