Mchanganuo wa gharama ya kulima ekari moja ya mahindi

Mchanganuo wa gharama ya kulima ekari moja ya mahindi

Pole sana,hawaweki wazi changamoto ya hali ya hewa.
Hapana, hao wanaoleta mrejesho wanatokea maeneo ambako kuna Kilimo cha mahindi ndiyo maana wanazungumza habari ya kuweka mbolea! Mavuno waliyozungumzia ni ya kawaida kabisa! Wilaya ya Tanganyika wanalima bila mbolea lakini hawakosi magunia 15-20 kwa ekari. Changamoto ya kubwa ni udhibiti wa post harvest losses, mazao mengi yanapotea wakati wa uvunaji. Unakuta mahindi yanaoza kutokana na wingi wa mvua!
 
Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-

Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-

Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Hujataja ghalama za Mbolea. Heka moja inahitaji wastani kilo 200 za mbolea. Mfuko wa kilo 50 unauzwa wastani 100,000 x 4 = 400,000.

Jumlisha 600,000 + 400,000 = 1000,000/= hiyo ndiyo ghalama halisi ya kuihudumia ekari moja ya zao la Mahindi.
 
Wakuu Saluti,
Ngoja niwape experience yangu ya Kilimo cha Mahindi Mkoa wa Ruvuma kwa Wilaya ya Mbinga.

1. Kukodi shamba 50,000 - 100,000 inategemea mahali na mahusiano na mwenye shamba.

2. Kulima kwa trekta 60,000, Kwa kutumia vibarua ni kadiri ya makubaliano lakini ni kuanzia 45,000 hadi 70,000

3. Mbegu inategemea na aina ya mbegu ila Mbinga maarufu ni Mbegu aina ya Tembo ya Zambia gharama ni kuanzia 15,000 hadi 20,000 kwa paketi, hapa utahitaji paketi 6.

4. Kupanda, zipo njia mbili. Kwa kutumia vibarua ambapo ni kati ya 4000 -7000 kwa kibarua au kwa kutumia mashine ya kupandia ambapo utalipa kati ya 20,000 hadi 25,000

5. Mbolea hapa utaweka mifuko 5 - 6 kwa awamu mbili (2.5 - 3 kwa awamu). Mbolea maarufu huku ni UREA 70,000/= CAN 65,000/= na SA 55,000/= kwa bei ya ruzuku. Au kama utapata mbolea aina ya YaraMila Cereals hiyo ina mchanganyo wa mbolea zote hizo tatu.

6. Kuweka mbolea, utalipa vibarua kwa kila awamu kwa gharama ya vibarua ambazo ni kati ya 4000 - 7000

7. Palizi ni 30,000 hadi 45,000 kwa hekari. Au unaweza kupiga dawa hapa gharama itategemea aina ya magugu yaliyopo shambani ndio ita-determine gharama ya dawa na bei zake.

Shida ya dawa kuna probability ya kurudia kupiga tena in case haijakubali vizuri na kama mtaalamu ameshindwa kukushauri aina ya dawa kulingana na aina ya magugu lakini pia changamoto nyingine unaweza ukaunguza mazao kunahitajika umakini wakati wa upigaji dawa.

8. Kuvuna na kukusanya mahindi utalipa vibarua in daily basis kwa rate ya 4000 hadi 7000.

9. Kupukuchua mahindi gharama ni 1000 kwa kila kiroba.

10. Matokeo kwa hekari moja kama utafuata hatua zote hizo hapo juu na ukawa haujaathirika na mvua na ardhi ni nzuri hautakosa kupata kuanzia gunia 18 hadi 33.

Gunia moja halitapungua kilo 120 hadi 135 na bei itategemea soko limekaaje. Ila kwasasa bei ni kuanzia 650 hadi 800 kwa kilo.

NB. Bado gharama za usafirishaji, ushonaji wa viroba, kupandisha na kushusha, chakula cha vibarua na gharama za kwenda na kurudi shamba hazijajumuisha.

The higher the expectations the Greater the disappointment. But all in all Mahindi kwa Ruvuma it's a hell of business na kama una mtaji wa kutosha achana na kwenda shambani kulima nenda vijijini weka mzani nunua mahindi.

I hope umepata kitu cha kujifunza.
Shukrani bro...barikiwa sana...
 
Ili kulima kitaalamu kwanza inatakiwa kujihakikishia upatikanaji wa maji yawe ya mvua au kumwagilia.

Pili ni ardhi inayokubali hilo zao liwe la Mahindi au lingine.

Tatu shamba lilimwe kwa Trekta kwakuwa katika ekari moja ukilima matuta ya jembe la mkono linatoa matuta 70 hadi 75 hiyo ndio mistari au matuta ya kupanda Mahindi yako.

Shamba likilimwa kwa trekta linatoa mistari 120 hadi 130 kama mistari ya kupanda Mahindi yako.

Shamba hilo likipata maji, mbolea na palizi sahihi katika muda sahihi.
Shamba la kulima kwa mkono linatoa gunia za kilo 120 kuanzia 15 hadi 25.

Shamba la kulima kwa Trekta linatoa gunia za kilo 120 kuanzia 25 hadi 35.

Hivyo Basi Kama nilivyoeleza pale juu kuwa wastani Ekari moja ya Mahindi kitaalamu kabisa inahudumiwa kwa ghalama ya Tsh 1000,000/=

Na kwa wastani Kama soko la Mahindi litakuwa la kawaida Mwenye kulima kwa jembe la mkono atatarajia kupata wastani wa shilingi 1500,000/= hadi 2,000,000/= kwa ekari moja.

Yule wa Trekta atatarajiwa kupata shilingi 2000,000/= hadi 3,000,000/= kwa ekari moja.
Shamba linatakiwa kuwa chini ya uangalizi kwa masaa 24 Kama mtoto mchanga.

Kasoro yoyote inayojitokeza inapaswa kuhudumiwa mala moja na kwa utaalamu wa kilimo.
Ni vema kulima kalibu na chanzo cha maji ili mvua ikiwa ya mashaka Basi limwagiliwe na maji yaliyokalibu.

Hivyo Mota japo ya Mchina iwe inawaka na inamafuta muda wote.

Jambo lolote likifanywa kitaalamu linaleta tija.
 
mkuu kg 12 za mbegu ni sawa na miche 24,000 kwny eka moja inawezekana japo wengi tupo kwny miche 17,000 kwa spacing ya 30x90cm
Kitu tunachokosea mara kwa mara ni mbolea, kama tuna ambiwa kila mche tuweke grams 5 ya kila mbole meaning 5x24,000= 120,000gm ya mbolea sawa na 120kg = sawa na mifuko miwili na nusu kwa maana hiyo kwa eka 1 utahitaji jumla mifuko 5 ya mbolea.
Hata kwa miche 17,000 bado utahitaji kilo 170 ya mbolea jumla ni karibia mifuko 3.5 Ukiachilia mbali mvua pia nadhan tunashindwa kufanya vzr kwny kilimo kwa kukosa taarifa muhimu zinazopelekea kupata mazao hafifu.
Na anza rasmi kulima mwaka huu ntajitahidi kufata maelekezo yote ya kitaalamu pamoja na kushare taarifa kwa wanavijiji lilipo shamba ili kubalance stories nitajitahidi kuweka hapa jukwaa pendwa
Nimenote kitu hapa
 
Mchanganuo wa kilimo cha .... Kwa heka Kulima elfu 60 mbegu kilo elfu30 yaitajika kilo 5 kupanda elfu20 kupalilia elfu 30 kuvuna elf50 ikiuza jumla unapata m19 kwa hekar moja unajua kilimo cha nn hicho tulia tunalima wachache
 
Safi hio ni specific kwa eneo gani na wilaya ipi?
Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-

Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-

Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
hizo hesabu umepigaje hapo?
 
Mchanganuo wa kilimo cha .... Kwa heka Kulima elfu 60 mbegu kilo elfu30 yaitajika kilo 5 kupanda elfu20 kupalilia elfu 30 kuvuna elf50 ikiuza jumla unapata m19 kwa hekar moja unajua kilimo cha nn hicho tulia tunalima wachache
KILIMO cha upupu
 
Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-

Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-

Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Faida ya Tsh 600000 kwa ekari igawe kwa muda uliotumia kusubiri pesa yako irudi.
Kuanzia mwezi wa kulima (mwezi wa 12 kwa Songwe) mpaka muda ambapo bei ingalau imepanda (Mwezi wa 8)
600000 / 9 = 67,000 TSH (Hii inamaanisha kila mwezi ulikuwa ukiingiza Tsh 67,000 tu ambayo haitoshi kulisha familia).

Ili ufaidike kwenye kilimo cha mahindi inabidi uingize ingalau Tsh 2500000 kwa mwezi

2500000/67,000 = 37 ekari

Inabidi ulime ingalau ekari 35 za mahindi ndo uone faida na kusomesha watoto shule nzuri!

Aksante
 
Huu hapa ni mchanganuo wa kulima ekari moja ya mahindi kwa sasa hivi
1. Kukodi shamba ekari 1 - 70,000/-
2. Kulima shamba mara 2 - 60,000/-
3. Mbegu pakiti 6 sawa kg 12 - 72,000/-
4. Kupanda mahindi - 30,000/-
5. Mbolea 2 - 140,000/-
6. Palizi 2 - 60,000/-
7. Kuweka mbolea - 30,000/-
8. Kuvuna/kupukuchua/mifuko - 100,0000/-

Jumla ya gharama huwa ni 550,000/- ~ 600,000/-

Mavuno
Mara nyingi mavuno hutegemea ubora wa ardhi na matunzo ya mazuri ya mazao, lakini mara nyingi ekari moja ya mahindi hutoa gunia 15 ~ 25, sasa ukipata kiwango cha chini gunia 15 ukauza kwa bei ya sasa 80,000/- unapata Tsh 1,200,000/- faida ya Tsh 600,000 kwa ekari.
Kiufupi mbolea lazima mifuko 3 Kwa kiwango Cha chini kabisa ,dawa za Wadudu na wastani wa gharama Kwa ekari 1 ni Kati ya 650k-700k ila una guarantee ya kuanzia gunia 25 kwenda Juu.
 
Faida ya Tsh 600000 kwa ekari igawe kwa muda uliotumia kusubiri pesa yako irudi.
Kuanzia mwezi wa kulima (mwezi wa 12 kwa Songwe) mpaka muda ambapo bei ingalau imepanda (Mwezi wa 8)
600000 / 9 = 67,000 TSH (Hii inamaanisha kila mwezi ulikuwa ukiingiza Tsh 67,000 tu ambayo haitoshi kulisha familia).

Ili ufaidike kwenye kilimo cha mahindi inabidi uingize ingalau Tsh 2500000 kwa mwezi

2500000/67,000 = 37 ekari

Inabidi ulime ingalau ekari 35 za mahindi ndo uone faida na kusomesha watoto shule nzuri!

Aksante
Wacha kutisha watu.Ekari 10 zinakupa faida nzuri,hapo ni gunia minimum 250 *50,000=12,500,000 ambapo gharama zote sio zaidi ya 5,500,000.

Unavyolima ekari nyingi ndivyo unit cost inapungua
 
Mvua ni ya kwako? Wadudu? Palizi?
Kama unalima Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na Magharibi kuanzia Kagera mvua ni uhakika haijawahi Goma hata siku Moja.

Huko kwingine Sina uzoefu ila ni tia maji tia maji.
 
Kwa haraka haraka naweza sema mikoa kama Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya, Rukwa, Katavi, Songwe, Kagera, Kilimanjaro, Arusha, Tanga mvua huwa haisumbui sana
Plus Kigoma na Kusini ya Morogoro
 
Back
Top Bottom