Mchengerwa: Rais ameridhia kuipandisha hadhi Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji. Soko kubwa na Stendi kuanza kujengwa

Mchengerwa: Rais ameridhia kuipandisha hadhi Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji. Soko kubwa na Stendi kuanza kujengwa

Vijana jifunzeni kumpelekea moto vizuri mutoto wa mamamkwe...
Maisha so magumu ila pia muoe penye rutba muache ulofa (in mukapa voisi)
 
Mkuu ... Yote hii ni double standard... Mchengerwa anataka tu kulazimisha Sababu ni waziri anayehusika na mambo hayo na mkaazi wa Eneo hilo....

Na wenyewe hukohuko Rufiji wanavutana kwa iwe Ikwiriri au Utete.....

Bora hata Chalinze iwe Wilaya kuliko hiyo Rufiji kupambaniwa....
Ok. Labda kama ni Political Games.
Ila Chalinze tayari ni Wilaya tangu December 2020
 
Halafu hawaoni hata aibu kusema mitano tena ya nini kwa utaratibu wa upendeleo wa kimaendeleo kwa rasilimali za Nchi si sawa kabisa. Maadili ya Viongozi yameishia wapi jamani?

Inasikitisha na kushangaza mno aisee !
 
Duh hii nchi mahali ilipofikia Mungu atusaidie.
 
Hahaha kwanini Chalinze isiwe MKOA, na Msoga liwe jiji? Hilo nalonendeni mkaliangalie.
 
Hapana.... Chalinze ni Halmashauri.... Ni sehemu ya Wilaya ya Bagamoyo... Au ulikuwa hulijui hili?....????
Ninafahamu hilo kuwa ni Halmashauri na ilianza rasmi 2016 baada ya maeneo kutengwa 2015. Ila Mchakato wa kuifanya iwe Wilaya ilikuwa December 2020; naona haikufanikiwa.
 
makao makuu ya wilaya ya rufiji yapo utete
 
Kwa mujibu wa Waziri wa Tamisemi bwana Mohammed Mchengerwa amenukuliwa akisema kuwa Rais Samia Ameridhia Iliyokuwa Halmashauri ya Rufiji kupewa Hadhi ya Mji ambapo Jengo kubwa la Makao Makuu la zaidi ya Bilioni 10 litajengwa Ikwiriri.

Kana kwamba haitoshi,ikumbukwe kwamba Mkuranga imeomba kuwa Manispaa ambapo Stendi kubwa ya Mabasi inaendelea na Ujenzi.👇👇
=======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Kujenga soko kubwa la kisasa pamoja na Kituo kikuu cha Mabasi wilayani Rufiji Mkoani pwani mara baada ya kuipandisha hadhi wilaya hiyo na kuwa Halmashauri ya Mji wa Rufiji.

Kulingana na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara Ikwiriri wilayani humo, amesema utekelezaji wa miradi hiyo mikubwa unatarajiwa kuanza rasmi mwanzoni mwa Mwezi Novemba mwaka huu 2024.

Mhe. Mchengerwa amewaambia wananchi wa Rufiji kuwa ujenzi wa soko hilo litakalokuwa na maduka zaidi ua 122, Vizimba zaidi ya 100 na vibanda vya wafanyabiashara ndogondogo utagharimu fedha taslimu shilingi Bilioni 14 huku pia Serikali ya awamu ya sita ikiahidi kujenga Jengo la Utawala katika Halmashauri hiyo ya Mji litakalokuwa la Ghorofa tatu zenye Ofisi zaidi ya 50 na kugharimu takribani shilingi Bilioni 10.

My Take
Halmashauri zilizokidhi vigezo na kuwasilisha maomba mapema kabla ya kina Rufiji nazo zipandishwe hadhi pia mfano Mbalizi Kwa Mwamposa.


Pia soma: Rais Samia akataa ombi la kuipandisha hadhi Mbalizi kuwa Halmashauri ya mji

View: https://x.com/Jambotv_/status/1867627948863594579?t=KyUmIvaK4s-j5jvqNaF9Mw&s=19
 
Back
Top Bottom