Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 23,620
- 52,790
Leo tuwakumbuke mafundi wa mpira ambao walikuwa wana uwezo mkubwa sana wakiwa dimbani enzi za uhai wao kabla ya kutangulia mbele ya haki.
Mimi naanza na huyu Said Nassoro Mwamba Kizota. Huyu jamaa mpira aliujua sana ila pia ubabe pia aliumudu mno. Toka anacheza mshambuliaji kisha baadae kurudi kucheza beki.
Enzi anacheza straika mabeki wengi walikuwa wanamuogopa, pia aliporudi kucheza beki, washambuliaji wengi wakawa wanamuogopa. Aliweza kucheza kwa kiwango cha juu sana kwa muda mrefu. Kama hujawahi kumuona enzi za uhai wake, anacheza kama anavyocheza Sergio Ramos.
Alijitengenezea sifa na umaarufu jinsi alivyomudu kumzuia mshambuliaji matata wa miaka hiyo, marehemu Majid Musisi wa Sports Club Villa kwenye klabu bingwa Afrika mashariki pale Kampla mwaka 1993 bila shaka.
Kwako wewe, ni mchezaji gani ulimkubali enzi ya uhai wake?
Mimi naanza na huyu Said Nassoro Mwamba Kizota. Huyu jamaa mpira aliujua sana ila pia ubabe pia aliumudu mno. Toka anacheza mshambuliaji kisha baadae kurudi kucheza beki.
Enzi anacheza straika mabeki wengi walikuwa wanamuogopa, pia aliporudi kucheza beki, washambuliaji wengi wakawa wanamuogopa. Aliweza kucheza kwa kiwango cha juu sana kwa muda mrefu. Kama hujawahi kumuona enzi za uhai wake, anacheza kama anavyocheza Sergio Ramos.
Alijitengenezea sifa na umaarufu jinsi alivyomudu kumzuia mshambuliaji matata wa miaka hiyo, marehemu Majid Musisi wa Sports Club Villa kwenye klabu bingwa Afrika mashariki pale Kampla mwaka 1993 bila shaka.
Kwako wewe, ni mchezaji gani ulimkubali enzi ya uhai wake?